Msimshangae Msigwa: Mvuvi ndiyo huamua samaki auzwe au aliwe supu

Msimshangae Msigwa: Mvuvi ndiyo huamua samaki auzwe au aliwe supu

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2011
Posts
21,470
Reaction score
40,593
Kuna baadhi ya watu wanashangaa ukengeufu wa Msigwa. Wengine wanahoji kama ana utimamu wa akili ama kawehuka.

Lakini lazima tukubaliane kuwa sote kama watanzania tunao ujinga wa kihalaiki.

Ujinga wetu mkubwa ni kuwategemea sana wanasiasa kusimamia maslahi yetu bila sisi kuwasimamia wao.

Matokeo yake ni wanasiasa ndiyo wanapanga watupe nini badala ya sisi kuwataka watupe tunachotaka.

Ndani ya vyama vyote vya siasa kujiunga na chama ni hiyari kama ilivyo kutoka.

Lakini hizo zinazoitwa Kamati Kuu huwa zinajiamulia mambo kuhusu vyama vyao bila ya kuwashirikisha wanachama wao na milango ya kuhoji kwa wanachama wa kawaida ama imefungwa au iko mbali sana kufikiwa.

Sasa Msigwa amekuwa kama samaki aliyevuliwa na Kamati Kuu ya CCM.

Kamati Kuu ya CCM Sasa ndiyo inayoamua imtumieje Msigwa dhidi ya CHADEMA na wala si wanachama wa kawaida.

Kama kwenye "makubaliano" yao Msigwa atapewa nafasi fulani basi hakuna mwana CCM anayeweza kuzuia au kukataa.

Kwa ivo mvuvi ndiyo huamua kama samaki auzwe au aliwe supu.
 
Kuna baadhi ya watu wanashangaa ukengeufu wa Msigwa. Wengine wanahoji kama ana utimamu wa akili ama kawehuka.

Lakini lazima tukubaliane kuwa sote kama watanzania tunao ujinga wa kihalaiki.

Ujinga wetu mkubwa ni kuwategemea sana wanasiasa kusimamia maslahi yetu bila sisi kuwasimamia wao.

Matokeo yake ni wanasiasa ndiyo wanapanga watupe nini badala ya sisi kuwataka watupe tunachotaka.

Ndani ya vyama vyote vya siasa kujiunga na chama ni hiyari kama ilivyo kutoka.

Lakini hizo zinazoitwa Kamati Kuu huwa zinajiamulia mambo kuhusu vyama vyao bila ya kuwashirikisha wanachama wao na milango ya kuhoji kwa wanachama wa kawaida ama imefungwa au iko mbali sana kufikiwa.

Sasa Msigwa amekuwa kama samaki aliyevuliwa na Kamati Kuu ya CCM.

Kamati Kuu ya CCM Sasa ndiyo inayoamua imtumieje Msigwa dhidi ya CHADEMA na wala si wanachama wa kawaida.

Kama kwenye "makubaliano" yao Msigwa atapewa nafasi fulani basi hakuna mwana CCM anayeweza kuzuia au kukataa.

Kwa ivo mvuvi ndiyo huamua kama samaki auzwe au aliwe supu.
Nafikiri Msigwa atatumika hivi
 

Attachments

  • IMG-20200403-WA0003.jpg
    IMG-20200403-WA0003.jpg
    12.9 KB · Views: 2
Ndivyo ilivyo. Anayemlipa mpiga zumari ndio anayechagua nyimbo. Msigwa ameonyesha udhaifu mkubwa sana. Kuna makaburi yake yamefukuliwa huko mitandaoni mpaka aibu naona mimi.
Njaa mbaya sana.
 
Ndivyo ilivyo. Anayemlipa mpiga zumari ndio anayechagua nyimbo. Msigwa ameonyesha udhaifu mkubwa sana. Kuna makaburi yake yamefukuliwa huko mitandaoni mpaka aibu naona mimi.
Njaa mbaya sana.
Ameyatimba. Njaa imemuondolea weledi kabisa ameamua kuwa kama kibaka wa kawaida tu.
 
Sasa hapo ndio cjui mana tangu uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi wao wanalalamika kuibiwa kura tuu.
Hata historia ya siasa za nchi hii huijui. Uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi ulifanyika mwaka 1994.

Onesha ni wapi CHADEMA ililalamika kuhusu uchaguzi huo!?
 
Hata historia ya siasa za nchi hii huijui. Uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi ulifanyika mwaka 1994.

Onesha ni wapi CHADEMA ililalamika kuhusu uchaguzi huo!?
Sasa muda huo kulikuwa na Chadema wapinzani au Chadema wanaojitafuta hata mambo ya uchaguzi enzi hizo hawajui
 
Back
Top Bottom