Msione uvivu kuhesabu fedha mnazolipwa na ‘Teller’ wa benki

Msione uvivu kuhesabu fedha mnazolipwa na ‘Teller’ wa benki

Nilitoa pesa KCB buguruni ,sikuzigusa nikakuta 10,000

Hapo hapo buguruni sheli mble ya KCB bank kuna mpesa ndogo nilitoa pesa pia si kuouta 10,000
Hii tabia mbaya
Watu waridhike na wanachokipata kama unataka zaidi waende kuchimba dhahabu baharini
 
Sio kuhesabu tu hata kukuchomekea pesa bandia,nikiwa nasoma bibi alitoa 1.5M crdb kisha tukaenda deposit nmb na zile bank zinatizamana, kufika pale Mara tunaambiwa 20000 ni bandia tukachukua Ile pesa yote na kurudi pale crdb yule teller akasema yeye hajui,bibi akasema naomba nielekeze ofisi ya manager nikazunguze nae yule teller alitoka kule ndani faster na kuomba msamaha kwa bibi kisha akampa Ile alfu 20 tunaondoka
Hii imewahi nikuta mara 3.
Jana nimetoka kupata lalamiko kwa "chomachoma" mmoja hapa Newala ninayemtumia kukusanya korosho,kuwa kaka yake kapigwa 380,000 bandia kati ya 7 milioni aliyopewa.
 
Hivi karibuni mara kadhaa ninavyokuwa napokea pesa nyingi kutoka Bank (zile ambazo sio sealed) nikifika ofisini nakuta kuna pisi zinakua zinapungua

Mwanzo nilikuwa nikipata changamoto hii kwenye bundles za 10,000 na 5,000 ila karibuni hata hizi za 2,000 na 1,000

Rai yangu kwenu mnaopokea pesa nyingi kutoka Bank muwabe Bank tellers zile pesa ambazo wamepanga kukulipeni wazifungue wazipitishe kwenye mashine huku mkiwa mnaziona kama vile ambavyo tunavyowapelekea pesa wanazifungua na kuzihesabu mbele yetu.
Hiyo michezo ipo sana hela iliyoko kwenye bundle iliyo salama ni zile bundle za bulk na zenye sealed tu. Hizi za milioni moja moja wewe mwambie teller atoe rubber band apitishe kwenye mashine ukijifanya wa kishua utapigwa kila siku.
Wakati mwingine hata zile zenye seal wanapiga, mbinu wanayotumia ni kwamba wanachukua pencil ya round, inaingizwa katika ya noti, ina roll na noti moja halafu inavutwa. Mchezo kwisha.
 
Back
Top Bottom