Msolla, uongozi bora kwenye mpira ni vikombe vingi

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Mzee Kikwete aliusifia uongozi wa akina Msolla kuwa anaongoza vizuri klabu ya Yanga. Je, hii ni kweli?

Miaka 4 hujapata kombe lolote ispokuwa Mapinduzi Cup huo ni uongozi bora?
 
Ujinga una rangi nyingi!
Club ya mpira ni taasisi yenye idara nyingi za ndani na nje ya uwanja.

Mkwabi na Sasa Mangungo sijui nani wanapata makombe Simba lakini akili yako inakushawishi kuona hawa nj viongozi wazuri?

Timu ngapi EPL, La Liga zimechukua ubingwa ama zina uwezo wa Kubeba ubingwa? Je uongozi wao ni mbaya?

Ubingwa Yanga utakuja bila shaka, wacha watengeneze misingi imara ya kujitegemea na kujiendesha na sio kutegemea hisani ya mtu mmoja ambaye akiondoka system mzima ina collapse
 
Unachosema ni kweli kakini kina kasoro nyingi. Hata huo mfumo wa kampuni bado ni tegemezi, lazima tajiri atie mkono wake mfukoni kuipa yanga. Ina maana pale simba mo akijitoa kunabaki nini? Tuache kuaminishana yasiyokuwepo, wewe mwanachama utaambulia makombe na tajiri ataambulia fedha ya faida.

Hata kama ungekuwa na uongozi mzuri kama malaika lakini kama hakuna makombe you are nothing. Arsenal ilikuwa na uongozi bora sana usiokuwa na madeni chini ya Wenger Arsene, lakini ukame wa mataji ulimfukuza, hayupo. Wanachama kumshangalia Manji mbele ya Msolla na GSM hawakuwa wapumbavu.
 
Ndugu soma vizuri nilichoondika.
Simba hawajaanza kuendesha timu kwa mfumo sahihi ya kampuni. Kwa hiyo ni mfano mbaya.
Mo anafadhili anaweza kujitoa muda wowote.

Yanga wamesoma "lesson" kutoka kwenye mchakato wa Simba wanaenda kwenye mabadiliko kwa njia sahihi na sio mihemko

Ni bora kupata dose sahihi ya kutibu ugonjwa kuliko kumeza panadol ili kupata nafuu ya haraka!
Nauliza katika timu zilizopo ligi kuu nne za ulaya ngapi zina uwezo wa kubeba makombe?

Je, simply utalaumu uongozi uliopo kwa Norwich city kushindwa kubeba ubingwa!!!
 
Kama Yanga ilivyocolapse alipoondoka Manji.
 
Mzee Kikwete aliusifia uongozi wa akina Msolla kuwa anaongoza vizuri klabu ya Yanga. Je, hii ni kweli?

Miaka 4 hujapata kombe lolote ispokuwa Mapinduzi Cup huo ni uongozi bora?
Hivyo vikombe vitakunaje bila uongozinora
 
Ndiyo maana hizo timu zisizopata vikombe zinauzwa kwa matajiri wa hata nje ya uingereza. Kule ulaya timu zote zinanufaika kwa ama kuchukua vikombe, kumaliza top four au hata kusalia kwenye ligi kuna magao. Lakini timu ndogo pia zinauza wachezaji kwa timu kubwa hiyo ni faida pia. Lakini bila kuchukua kombe au angalau kumaliza top four you are nothing.

Kama huamini, wacha timu iwe kampuni kisha hakuna vikombe watauona moto wake.
 
Ukiangalia kwa umakini jamaa wamepaniki,wanajua Yanga kama itafanikiwa kwenye hili la mabadiliko watapiga hatua kubwa sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…