Msoto wa maisha Dar es Salaam ulivyonifanya nitamani kuwa mwizi na mhujumu uchumi

Msoto wa maisha Dar es Salaam ulivyonifanya nitamani kuwa mwizi na mhujumu uchumi

Ushauri wangu kwa vijana graduates waache uvivu na kujiona wana elimu kubwa hivyo kuchagua kazi.
Utakuta graduate anatumia muda mwingi kwenye mitandao ya kijamii au kutext marafiki bila kufikiri hiyo mitandao (internet) inaweza kuwa chanzo cha yeye kupata pesa.
Utakuta kijana anaishi kwa wazazi au ndugu muda wote anatumia kuangalia Tv (movies & series & football) kichwa hakiwazi nje ya box kuhusu maisha.
Usharibaro mwingi sana kwa graduates huku wakiwa watupu mifukoni.
Nawaasa wawaze maisha na kufanya kazi yeyote halali kwa bidii,hizo kazi za ndoto zao professional zao zitakuwa muda ukifika ila wakati bado wanazitafuta wajichanganye kila eneo.
Pia wawe na heshima kwa wakubwa zao utakuta kijana kwa kuwa ana ndevu/mavuzi/matiti hasalimii mtu hata majirani kama sio ndugu hawajui kuwa adabu na heshima kwa watu ndio tiketi ya kufikia ndoto zao na kufurahia mema ya dunia.
Umeongea ukweli Sana natamani kila graduate aione hii
 
Hii sehemu nitaongea kwa ufupi saana.

Huwa napenda sehemu zenye mchanganyiko maana huwa naamini pesa zipo.

Nilipita pale Karume nikaona watu wanaosha viatu kuna jamaa rafudhi yake alikua anaongea nikaona huyu wa nyumbani, tuliongea nae haswaa akawa Ananipa kazi ya kuosha viatu pc 1000 ananipa 5000 in short nikapiga kazi pale nikaanza kuzoeleka baada ya mwezi nikawa na hela kidogo ya kuchukua mzigo Kama 80,000 nikawa naingia mule ndani nachukia viatu vya watoto kwa 800 naosha then nauza kuanzia 3000.

Hapo pia msoto wake sio wa mchezo maana tunaanza kuuza viatu saa 8 usiku pale karume kwa nje, tunauza mpaka saa 12 asubuhi ikifika saa 1 asubuhi migambo wanazingua so tunaweka mzigo store mpaka saa 12 jioni ndio tunamwaga barabarani mpaka saa 3 usiku, hebu fikiria hiyo daily routine kwa kijana graduate Kama Mimi na wapo vijana wengi Sana wanaofanya hivyo mahangaiko ni makubwa but kinachopatikana ni kidogo, Mama akinipigia namwambia kila kitu kipo sawa.

Kwenye harakati ya kujichanganya na watu nikapata hili deal ambalo sitalizungumzia sana na ndilo lilinifanya niondoke Dar es Salaam na kusema sitorudi tena

Nilipata deal la kuuza Mafuta ya petrol na diesel kutoka kwa madereva wa mafusso na lorry wakienda huko wanarudi na mafuta tunakubaliana bei then mimi najua nitauzaje

Dah kwa Mara ya kwanza nikashika hela ambazo sikuwahi kushika maana nilikuwa napigiwa simu kila mahali demand ilikuwa kubwa lakini sikuweza ku-play smart nikakamatwa na polisi, huu msala ulikuwa mkubwa saana nahisi nilichomwa sikuwahi kulala polisi hapo kabla nikaambiwa nitapewa kesi ya uhujumu uchumi wakati Mimi nina mwezi tu tokea nianze kuuza mafuta😁😁....kwa ufupi msala uliisha japo haikuwa rahisi sitaongea mambo mengi hapa maana sikuwahi kuwaambia mtu hata mzee hakuwahi kujua Kama nilikamatwa nilipambana mwenyewe nikatoka!...

Nilitoa akiba yoote niliyokusanya kupitia hiyo biashara haramu nikachomoka...

Baada ya hapo nikaenda home Tabora sikukaa muda nikapata ajira, nikasema tokea moyoni sitorudi tena Dar maana kwa jinsi watu wanavyoishi ule ufahari unaweza Kufanya mambo maovu ili u survive. Unashangaa vijana hawana kazi lakini wanamiliki pesa chafu,

Vijana
Usitamani maisha ya mtu always kua wewe, hujui watu wanapatia utajiri.
Usije/usitamani kufanya biashara haramu zina hela sawa lakini ukibananishwa unaweza ukawa ndio mwisho wa ndoto zako humu duniani.

Kijana ukitoka nyumbani kwenda kupambana hakikisha unafikia kwa ndugu yako mtu mzima mwenye familia ili akusitiri kwa vitu vidogo Kama chakula, malazi huku wewe unaendelea kufikiri utafanya nini,

Kwa msoto niliopitia Dar ulinifanya kuwa mgumu na kuwaza kufanya biashara yoyote haramu ili nipate pesa but niliamua kuchomoka na kurudi kwa Mungu.

Tusisahau kupambana huku tukimuomba Mungu maana yeye ndiye mpaji wa vyote.

Lakini bado naamini humu duniani Kama umezaliwa familia maskini kutoboa kufika hatua ya kumiliki pesa sio rahisi kwakweli

Hapa simaanishi pesa ya nyumba na gari namaanisha pesa haswaaaa.
Tumeelimika mkuu hakuna mafanikio yanayokuja kirahisi lazima tukubali kuteseka.....
 
Safi sana mkuu kwa kutupatia kitu asubui leo ya leo wenye akili tutajifunza kitu.
 
Hapo ndio mwisho ninaomba watu wazima kidogo watoe ushauri kwa vijana wanaopitia kipindi kizito au kigumu au graduate kuishi kwa namna bora ya kufanya taifa letu liwe bora zaidi.
Note mpaka Leo nina alama ya sehemu ya kichwa iliyopasuka nilikia nafuga nywele lakini hiyo sehemu nywele hazioti, nimekua naona huruma kwa wapambanaji Sana maana nakumbuka nilipotokea.
Mkuu uoga wako umepelekea uwe lofa mpaka Leo, usiogope mapambano ndani ya kazi ya hatari . Umekimbia mapema sana hapa jijini.
 
Back
Top Bottom