Msuguano baina ya Spika na Rais ni ulevi wa madaraka

Msuguano baina ya Spika na Rais ni ulevi wa madaraka

Ngongo

Platinum Member
Joined
Sep 20, 2008
Posts
20,654
Reaction score
35,887
Upo msuguano wa dhahiri baina ya Spika na Rais. Spika ni kiongozi wa Bunge “Bunge” na Rais ni Kiongozi wa Serekali “Executive”. Wote ni Wakuu wa mihimili hapa anakosekana Jaji Mkuu ambae ni Mkuu wa Mahakama.

Ukizitazama kwa makini misuguano baina ya Rais na Spika utaona dhahiri kila mmoja anapenda kuonyesha ukuu wake na matamanio ya madaraka.

Tukiirejelea Katiba yetu ambayo Rais karundukiwa madaraka mengi,sioni ni namna gani Spika ataweza kupambana na Rais.

Rais anateuwa Mawaziri, Makaribu Wakuu,Wakuu wa Mikoa, Makatibu tawala wa mikoa, Wakuu wa Wilaya, Mabalozi, Majaji, Wakuu wa Mashirika ya Umma na Wenyeviti wa bodi za mashirika ya umma & Wakuu wote wa vyombo vya ulinzi na Usalama na mwisho kabisa anateuwa Wabunge kumi katika bunge la JMT.

Spika wetu yeye anateuwa Wenyeviti wa Kamati za Bunge na Wabunge 19 wasiokuwa na chama. Sasa kama ni mpambano Spika si lolote si chochote. Wateuzi wake wote hawana impact ya moja kwa moja kwa wananchi.

Spika Ndugai lazima atamke nimekosa nimekosa Mama nihurumie.

1641324375226.jpeg


Ni hayo kwa leo

Ngongo kwasasa Kibanda Maiti.
 
Nasimama na Spika

Ukisimama na Spika hakuna uteuzi kashamaliza Wenyeviti wa Kamati na wale Covid 19.

Mimi nasimama na Rais naweza kulamba uKuu wa Mkoa au hata unaibu Waziri.Au unajufanya hujasikia Mama anaunda upya baraza la Mawaziri mimi naomba walau nipate uNaibu Waziri TAMISEMI.Nakagua madarasa nafoka foka naingiza siku.
 
Rais ambae hataki mihimili mingine iwe huru na ifanye kazi zake ni hopeless fool.
View attachment 2068660
MAGOGONI MODERN TAARAB
wametoa Album Mpya ina Ngoma Sita zote Kali
1.Mtu na akili yako unahoji tozo na Mkopo
2.Stress za 2025
3.Serikali ya Mpito
4. Watakao kusumbua ni Shati ya Kijani wenzio
5.Kuna Mawaziri Mmeanza Makundi Makundi yenu
6.kuna watu nitawapumzisha Wakajiandae 2025

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Upo msuguano wa dhahiri baina ya Spika na Rais. Spika ni kiongozi wa Bunge “Bunge” na Rais ni Kiongozi wa Serekali “Executive”. Wote ni Wakuu wa mihimili hapa anakosekana Jaji Mkuu ambae ni Mkuu wa Mahakama.

Ukizitazama kwa makini misuguano baina ya Rais na Spika utaona dhahiri kila mmoja anapenda kuonyesha ukuu wake na matamanio ya madaraka.

Tukiirejelea Katiba yetu ambayo Rais karundukiwa madaraka mengi,sioni ni namna gani Spika ataweza kupambana na Rais.

Rais anateuwa Mawaziri, Makaribu Wakuu,Wakuu wa Mikoa, Makatibu tawala wa mikoa, Wakuu wa Wilaya, Mabalozi, Majaji, Wakuu wa Mashirika ya Umma na Wenyeviti wa bodi za mashirika ya umma & Wakuu wote wa vyombo vya ulinzi na Usalama na mwisho kabisa anateuwa Wabunge kumi katika bunge la JMT.

Spika wetu yeye anateuwa Wenyeviti wa Kamati za Bunge na Wabunge 19 wasiokuwa na chama. Sasa kama ni mpambano Spika si lolote si chochote. Wateuzi wake wote hawana impact ya moja kwa moja kwa wananchi.

Spika Ndugai lazima atamke nimekosa nimekosa Mama nihurumie.

Ni hayo kwa leo

Ngongo kwasasa Kibanda Maiti.

Ndugai anaweza kumtoa rais kwa kuhamasisha kura ya kutokuwa na imani naye.

Udhaifu wa siasa zetu za upinzani wa kushindwa kutambua hakuna adui wala rafiki wa kudumu bali agenda ni mzigo.
 
Hivi vijembe ndio tulivimiss, hatutaki Rais aliyepoapoa kama maji mtungini.

Nchi ilipoa sana toka mwendazake asepe.
 
Nadhani ni muda Sasa nafasi ya speaker iheshimiwe. Speaker anapokosea lazima kuwepo na formal communication kati ya mihimili na sio hii style ya kutubu hadharani na kushambuliwa hadharani baada ya kuomba msamaha. Hi sio Jambo zuri kwa afya ya siasa na maendeleo kwa ujumla. Kama speaker anashambuliwa hivyo na maoni yanaonekana Ni uchu wa madaraka je mbunge wa kawaida ana hali gani?. Tunaenda kutengeneza bunge bubu litakalo ogopa kumuudhi Rais na Mwenyekiti wa chama tawala.

Pia speaker wetu Ndugai ameyataka yote haya, amekuwa anatetea serikali na chama bila kujua yeye Ni mkuu wa mhimili wa dola, na Wala hayupo pale kwa niaba ya chama au serikali. Kumbuka speaker Ndugai alivyoshughulikia suala la wabunge wa viti maalum CUF kipindi Cha Maalim Seif na kumbuka alivyoshughulikia suala la wabunge 19 wasiotokana na CHADEMA. Hivyo ili Bunge lirejeshe heshima yake, inabidi tupate speaker mpya asiyekuwa na uchama na atakaye fahamu yeye Ni mkuu wa mhimili na sio mkereketwa wa chama na serikali.
 
Rais anawashambulia wenzake hadharani sana. Waziri wa Kilimo yalishamkuta haya juzi tu. Leo ilikuwa zamu ya Ndugai na Kassim.

Ndugai na Kassim wakijaribu kumjibu,watakumbana na matusi kila kona watajitokeza UVCCM watavurumishia meneno ya kejeli kabla hali haijatulia Wenyeviti wa Mikoa watakuja na azimio la kuwavua uanachama.

Kama wana akili nzuri inabidi watulie wasutwe hadi wakome na waone umuhimu wa Katiba mpya.
 
MAGOGONI MODERN TAARAB
wametoa Album Mpya ina Ngoma Sita zote Kali
1.Mtu na akili yako unahoji tozo na Mkopo
2.Stress za 2025
3.Serikali ya Mpito
4. Watakao kusumbua ni Shati ya Kijani wenzio
5.Kuna Mawaziri Mmeanza Makundi Makundi yenu
6.kuna watu nitawapumzisha Wakajiandae 2025

Sent using Jamii Forums mobile app
Hapo kwenye Serikali ya mpito ametajwa huyu jamaa kuwa ndiye engineer👇🤣🤣🤣
AIWU7u.jpg
 
Back
Top Bottom