...nadhani hii pia inatokana na kasi ya maisha,...kwa sasa hatuna muda wa kukaa chini ya mwembe kusubiria dodo lianguke, au alfajr unaamkia chini ya miembe kutafuta yaliyoanguka usiku...Kizazi hiki ni cha kukimbilia Shoprite au Imalaseko kununua Mango juice ya Azam, tamu kuliko tunda lenyewe... yaani tunaishi maisha ya short cuts kibao,...na siku hazigandi vile vile...Tukubali mabadiliko. Zama za kuandikiana barua, niifukizie poda na marashi, kisha niitume kwa posta mpaka ikufikie wakati kuna emails/sms leo hii nitaonekana sijali muda.
Hizi theories, kusoma vitabu, au kubandika post JF upate msaada wa mawazo ni kiashiria kwamba hatuna muda wa kukaa na wazee wetu, mashangazi na wajomba kupata busara zao juu ya maisha kwa ujumla. Kama mnakumbuka ile Topik ya Wheel of Life?, kuna wengi waliipinga kwamba muda hautoshi kabisa. Twendeni na wakati kabla wakati haujatuacha tukabakia tunashangaa...
...Mzee DC bado anashangaa shangaa haya mambo tunayoongelea,....kwani kuzaa na mtu lazima muwe mlipendana nae kiviiile? Vile vile kuna zile One night stands ambazo mw'mke ana conceive kisha anachukulia mtoto kama bakora ya kukuchapia. Mwanaume unaishia kulambishwa kimtego mtego, ....mtoto hupewi, kwa mkeo hajulikani,....uhakika wa mtoto mwenyewe kama ni wako au sio wako hujui...ukijifanya kusahau unakumbushiwa...almuradi unachezeshwa makida-makida tu... mnh, maisha haya, misukule ipo ya aina nyingi!