"Msukule" wa Mapenzi...

ROV na MR ROCKY nimewakkubali......asanteni sana, huku nilipo tunasema ucku mwema,cjui mlipo, kidalo poo...
 
Reactions: Mbu
Natumaini utafanikiwa...nasubiria hiyo feedback kama pilau la xmass!!!

mwali hulali? hahahha ucnikumbushe pilau coz xmac uchagani ni ndizi na nyama kwa wingi....hahhahaha tusubiri mae.
 
mwali hulali? hahahha ucnikumbushe pilau coz xmac uchagani ni ndizi na nyama kwa wingi....hahhahaha tusubiri mae.
Uwiiii pilau na ndizi jamani...

Ahhhh haya bana urae kisha mae...!!!
 

my broda hapo shida inakuja kwa waliotuacha kumbe b ado walitutaka,walituaacha kwa matamanio fulani ya wengine wamekuja kugundua kumbe sio so wanajitahidi kurudi kwa waliowaonakwamba wangekuwa sawa kwao,wanakuta nafac zimejaa bac ni visa vya madenge vinapoanzia,2takomaa mpaka kieleweke......
 

mie amemnitonesha kidonda! Mbu na makusudi yake...yaani jamani hata kovu halijapona Mbu kasahlitibua...haya bwana!
 

sasa kwa mie niliopo kwenye hili vuguvugu, naweza kulcal jamani kuuliza kinachoendelea? coz kaniambia mamake mgonjwa sana, naanzaje?nina huruma na mama sana sana but nahic ndio ataona amepata urahic wa anachokusudia?a mhhh ngoja nilale jamani ntazeeka kabla ya cku mie.
 
Reactions: Mbu
.....wangapi mmesha experience haya? Kuna wengine wana suffer abuses bila kujitambua...


...jichunguze kama ushawahi experience Mojawapo au zaidi kwenye Circle hii;



...shituka usingizini!

Wewe ni "msukule!" iwapo aliyekutenda yote haya bado anakujia na alinacha za 'hapo zamani za kale...mimi bado nakupenda, sitaki kukuacha!' Ilhali anajua usha move on na maisha yako.

 
Mbu, you are an honest-to-goodness love and relationship savant. I admire your oracular wisdom in this realm. Super big up.
 
Jamani mimi sijaelewa,

Hivi ex-BFs/GFs ni mashirika ya kutoa misaada kwamba ndo yawe kimbilio mtu anapokuwa na matatizo yake? Sihitaji kuwa karibu naye wala kujua matatizo yake ya kila siku. Kuendekeza huruma ndo mwisho wake unapoteza vyote..Anakuharibia ndoa na kuanza kukucheka!


Watu wa namna hiyo wana nia mbaya sana..ni devils!!
 

Dada,

Hayo yanawezekana ila walio wengi tunakuwa na kisebusebu tu. Na pia tunajua kuwa huo ndo mlango rahisi sana wa kupandia daladala!!

Si nasikia wengi wanaamini kuwa, Ex-GF/BF ni wako hadi kiama???!!!
 
Reactions: Mbu
Mbu, you are an honest-to-goodness love and relationship savant. I admire your oracular wisdom in this realm. Super big up.

Mkuu NN,

Hapo unamaanisha nini? Wengine tu akina Maimuna!!

Umepotelea/potezewa wapi Bro?

Mzee DC
 

Ushauri mzuri sana Eiyer na natamani ningeweza kufanya haya ila nimejitahidi lakini ukweli ni kwamba siwezi ishi bila furaha ya kukopa kutoka kwa huyu mtoto kwani yeye pekee ndie rafiki wa kweli, ndugu wa kweli na kila kitu kwangu. Unajua binadamu tuna maudhi sana na mtu anaweza kukuudhi kwa makusudi kabisa haijalishi ni mpenzi/mume au ndugu ila huyu mrembo ananifurahisha tu wakati wote wala huwa sioni maudhi yake ya kunikosesha raha kama wanavyoweza fanya wengine yaani huyu ndio maisha yangu mpedwa. Halafu nikifikiria nilivyomzaa zaa ni kama maigizo tu nilipoteza muda wangu mwingi kwa ajili yake kifupi mambo mengi sana nilifupisha kwa ajili yake. so siwezi kumuachia kirahisi labda yeye aamue kuniacha.

Huwa saa nyingine naamua muache amchukue zikipita siku mbili weeeeeeeeeee wapi, uchungu wa mwana bana asikwambie mtu
 
S

Sawa kabisa Lizzy nakubaliana na suggestions zako ila tu nina wasiwasi kama mtu mwenyewe ni mkorofi. Kwa hiyo option ya kwanza kuwa nimpe simu Mr anipokelee......ah kama Ex ni mkorofi anawezamporomoshea matuc au maneno ya kashfa Mr wangu bure....kitu ambacho sitapenda kabisa kitokee. Yaani Mr atukanwe, dharauliwe kwa kosa langu la kumchagua kichaa awe mpenzi wangu? Ehee ni pysch case hii kabisa. Nitampa tu taarifa Mr kama atahitaji kuaminishwa nitamuaminisha kwa kuweka loud speaker ayasikir maongezi ya hilo ji-ng'ang'anizi. Otherwise nitadeal naye mwenyewe (kwa msaada wa Mr).

Option ya pile its a big YES to me.
 

Mbu.............................Aksante
 
Reactions: Mbu
Kama anakupigia simu usiku anakuambia "naumwa"mwambie kwani mimi daktari?Halafu umsikie kama hajatoka nduki fasta an never look back!!

Hii post imenifanya nicheke bila kupenda. We Elyer eti atoke nduki kwa kijibu cha kitoto kama hiki? Hujakutana na ving'ang'anizi wewe!

Afadhali huyo atasema anaumwa, mwingine anapiga kisha anakwambia amelewa na hajui atafikaje nyumbani! sasa sijui mie trafik au anapiga nimepata pancha!!- zamani wakati ndo niko kwenye siti ya mbele kabisa ya hilo li-coaster asemalo Mbu alikuwa akipiga hivyo natoka nduki mtoto wa kike vruuuum mpaka alipo namchukua tunarudi nyumbani!! ah sasa hivi nahisi fyuzi za button ile zimeshaungua!
 

Mkuu..Thanks again for sharing... Ningefurahi kuona reaction ya kina dada kwa hilo gurudumu kwani naliona limeweka bayana udhaifu wetu wanaume kwa hawa viumbe..

Binafsi naamini sisi wanaume tume- inherit elements za ubinafsi ambazo zinatupa kichwa na kujiona tunahitaji power and control albeit kwa kumdidimiza mwanamke. Ni nature ambayo hatuwezi kupinga ila kama tunajua hilo ya kuwa sisi viumbe adimu (kutokana na matatizo yetu na roho mbaya) tunaweza kupunguza impact za ubinafsi huo wa kujitakia.

Samahani naenda nje kidogo ya mada yako ya gurudumu la msekule, lakini naona ni vizuri kuona chanzo. Mimi naamini ubinafsi huu ambao tumezaliwa nao..ndio unatufanya tuamini yale yote tunayotenda ni sahihi hadi siku ile tutakapojitambua.

Kwa upande wa pili pamoja na kuwa na nguvu za maumbile tulizojaliwa naamini wanaume tuko soft na weak sana.. na ndiyo maana tunaficha weakness zetu kwa kutaka power na control. Vitu hivi na ukichanganya mambo ya utamaduni, mila na faith ..basi wanaume tunakuwa mazezeta wa ubinafsi hadi tunashindwa kujitambua ..kwani nature inahalalisha maovu yetu bila kujijua.. Kwa mtego huu na mingine niliyosema kwenye comment yangu ya jana..mwanamke anakuwa tayari ameshaingia kwenye msekule bila kujijua..Sisi tutaendelea ku-push mabaya tukidhani tuko sawa..

Tabibu wa ugonjwa huu wa ubinafsi na udhaifu wa mwanaume ni Mwanamke mwenyewe. Mke wangu asiponiambia na kunikaripia yale mambo mabaya ambayo namfanyia mimi nitaendelea kuugua bila kujijua ugonjwa mbaya wa ubinafsi.. Lakini kama yeye akisimama kidete ..na kunipa "live" bila kuchoka basi kuna chance kubwa ntaamka kwenye usingizi mzito na kujijua kuwa nafanya mabaya na kujirekebisha... Umri wa mwanaume unachangia pia kasi ya kujijua.

Binafsi naamini Men mature at the age of 40..kuna watakaopinga ..lakini..binafsi naamini hivyo. Kupona ugonjwa wa ubinafsi katika age ya 40 & above ni rahisi kuliko ukiwa na umri kati miaka 25 and 39.
 

Tulizo nakubaliana na wewe kwa asilimia kubwa. Ubinafsi wetu na unyonge wetu Tuna ubinafsi sana kwa kujiona sisi ni sisi na kila tunachokifanya kiko bora na ni kizuri hata kama ni pumba au cha kijinga ila tutapenda kionekane ni kizuri
Pia unyonge kwa kuwa tunajijua kuwa mbele ya mwanamke sisi ni kama sisimizi ni lazima tujifanye wababe hata kama ubabe wenyewe haupo ili tuwafanye wenza wetu watuone kuw atuna nguvu ilhali ukweli ni kuwa hakuna na hatusemi kitu inapokuja issue ya kuwa mbele ya mwanamke.
 
Reactions: Mbu
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…