Msumbiji Wamekodisha Bandari ya Nacala Kwa Malawi & Zambia Kwa Miaka 100. Tanzania Kupoteza Mteja namba 2 wa Dar Port

Mozambique wameshamaliza hiyo, Umoja wa Ulaya wametoa meli ya kwanza hapo kwa kukata utepe, Mama Ursula Van De Layan alikuja hapo kushuhudia meli ya kwanza inatoka, tofauti na Tanzania, Mozambique hawana mbwembwe za kujisifu sana kwa wanasiasa wao kuhusu miradi. Kumbuka sisi tulianza kushimba gas ukanda huo wa Cape Delgado (Mnazi bay to Palmas/Ruvuma River Delta) na kuzalisha umeme, wao wenzetu wamewapa total kwa share, wanzalisha gas ya kupikia majumbani. Ebu google uone. Tanzania inasua sua sana kwenye gas ya kupikia ambayo ndio ela ilipo duniani.
 
Mozambique
 

..Tanzania tunayo bandari kavu eneo la ISAKA mahsusi kwa ajili ya Rwanda ilijengwa miaka ya 80 na Mwalimu Nyerere.
 
Vipaumbele vyetu Kama nchi hatuko strict kivile,ile bandari ya mtwara,halafu pasua SGR mwambao ule kuelekea kuungana na Tazara na kuelekea kuungana DRC,lazima tuwe patriotic na Mambo yetu,halafu DP world mzigo ukipungua bandarini Dar,huo uwekezaji utakuwa white elephant project,serikali andaeni watu walio na sensitive na uchumi na masuala ya nchi,kuliko Hawa politicians,they normally seek their personal stakes
 
Leo Ni miaka 50 stori za liganga na mchuchuma nimeanza kuzisikia tangu mwaka 1980 Hadi lao hakuna kitu
 
Mipango kupewa wanasiasa haitekelezeki ,maana wao mkwamo wa mradi kwao ndo mtaji,ona Sasa tumeanza kupigwa bao
 
Umeandika kitu cha kufikirika. Lengo la hiyo inland terminal huko Kigali wala si ulivyosema ndio maana baada ya miaka mitatu, mwaka Jana Rwanda waliwekeza dry port naivasha ili kurahisisha zaidi kutumia bandari ya mombasa
 
Umetoa lawama bure tu, Tanzania tuna hectare 60 za dry port huko DRC. Pia kwa Zambia tayari Kuna Tazara dry port huko kapili mposhi. Haya umezungumza yapo tayari na mengine yanaendelea

Labda kama ulikua hujui, na kama ulikua hujui hukupaswa kulaumu
 
Umeandika kitu cha kufikirika. Lengo la hiyo inland terminal huko Kigali wala si ulivyosema ndio maana baada ya miaka mitatu, mwaka Jana Rwanda waliwekeza dry port naivasha ili kurahisisha zaidi kutumia bandari ya mombasa
Sio cha kufikirika ni kweli hiyo ya Naivasha na ile iliyofunguliwa na Kagame mbele ya hao waarabu zina malenga tofauti.

Samia asingekubali kuipoteza hii biashara. Upinzani ulikuwa mkali sana kwake mpaka Hamza Johari aliyeandaa mkataba huu kwa upande wa Tanzania akaitwa mbele ya kikao maalum cha CCM kufafanua kwa kina kitu gani kinakwenda kufanywa katika huo uwekezaji..

Logistics zote za hi biashara kuanzia huko Rwanda na Burundi zinafanywa na wao DPW ndio sababu ya kupewa hii biashara, sio kwamba wanaishia kuendesha hayo magati hapo TPA wanauchukua mzigo. Umiliki wao wa hayo magati ni sehemu ya biashara pana na wanaopinga uendeshaji wao wa TPA hawaelewi biashara nzima ipo vipi.
 
Watakaoumia ni wale wanaojinufaisha na Bandari ya Dar es salaam wakiwemo mafisadi na wapiga Dili...
 
Ili bandari zetu Zi operate zaidi mfano ya mtwara inabidi wajenge reli kutoka mtwara hadi kuunganisha Na ya TAZARA makambako ambayo kwa Sasa inaenda kuboreshwa na makambako waweke dry port kubwa ili watu wafanye option ya kuchagua mzigo upitie bandari ipi ya dar au mtwara Uzuri tayar RELI ya TAZARA inaenda kuwa chini ya wachina na Hawa eneo la makambako na mafinga wamewekeza viwanda vya kutosha vya product za miti na Sasa wanawekeza vya chuma makambako baada ya kuingia mkataba wa kuchimba chuma liganga ko hii itasaidia kuziteka nchi za EAC NA SADC KIUCHUMI ili wakibaki na wazo lao la kujenga reli ya mtwara mbamba bay kwa Sasa ni Bora wabadili GIA upepo umeyumba
 
Ni kweli kabisa unachokisema na wameshaimaliza ile yard pale, mimi binafsi sijajua nini kinatusumbua ktk fikira za viongozi wetu maana hatuna mipango ya muda mrefu wala hatuna mpango wa kama Nchi tusimame na nini ili kilete faida kwa kizazi hadi vizazi vijavyo.
 
Unajua kwanini mkataba WA TAZARA lazima Mkurugenzi Mkuu stoke Zambia, kile kilikuwa ni mikakati WA kiniashara , Kwa kutoa KAZI Kwa wazambia kupitia hiyo reli na Sisi kujihakikishia biashara ya mizigo kupitia Bandari. Sasa Sisi na ujinga wetu tukaendekeza wizi rushwa ndani ya TAZARA na hao Ndugu zetu WA Zambia matokeo yake ndio hayo ya nacala . lobito NK
 
One of the best thread I ever come across here... Well narrated. Kudoz
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…