Msumbiji Wamekodisha Bandari ya Nacala Kwa Malawi & Zambia Kwa Miaka 100. Tanzania Kupoteza Mteja namba 2 wa Dar Port

Msumbiji Wamekodisha Bandari ya Nacala Kwa Malawi & Zambia Kwa Miaka 100. Tanzania Kupoteza Mteja namba 2 wa Dar Port

Nchi ya Mozambique imeamua kuteka biashara ya Usafirishaji Kwa njia ya Maji Kwa Nchi zote za Sadc na kuiachia Tanzania maumivu makubwa.

Katika kutekeleza Hilo, Mozambique wameamua kuikodisha Bandari Yao ya Nacala Kwa Nchi ya Malawi na Zambia ambapo wataitumia Kwa kipindi Cha miaka 100 ijayo.

Nchi hizo 3 zinapanga kujenga miundombinu ya reli kutoka Nakala Hadi Mji Mkuu wa Malawi Lilongwe na kisha Hadi Mji Mkuu wa Zambia Lusaka.

Njia hiyo Mpya ya reli itapunguza umbali wa Zambia kuifikia Bandari ya Dar hivyo zaidi ya asilimia 90% ya mzigo wa Zambia utapitia Bandari za Msumbiji za Nakala na Beira.

Kwa hatua hiyo itakuwa ni pigo kubwa sana kwa Tanzania ambayo Bandari ya Dar ilikuwa inategemea zaidi mzigo wa Nchi ya Congo DRC na Zambia kama wateja Wakuu huko Nchi zingine zikiongesea ongezea shehena.

Endapo Zambia itaondoka rasmi kuwa mteja wa Tanzania sio tuu itapunguza mzigo wa Bandari ya Dar Bali itaua kabisa biashara ya Malori ya mizigo Tanzania ambapo Kwa sehemu kubwa yatahamia Nchi hizo za Zambia,Malawi na Msumbiji na zingine za Afrika Ili kuendelea na Biashara ya Usafirishaji.
View attachment 3080432

Pia soma: Bandari za Dar na Mtwara Kuwa Mashakani Kutokana na Nchi za Zambia,Malawi na Mozambique Kuzindua Upanuzi Mkubwa wa Miundombinu ya Nacala Port.

Kwa maelezo zaidi soma hapa Ili Kuongeza Ufanisi wa reli ya TAZARA,Tanzania na Zambia Ziiombe China Wajenge reli Mpya ya Makambako-Mtwara & Kasama-Lubumbashi/Likasi

Ushauri,;

Serikali ihakikishe mipango yetu yote Kwa Sasa iwe inalenga kuikumbatia DRC kuanzia Kusini Hadi Kaskazini maana ndio mteja pekee ambae walau jiografia inatupa nafasi.

Serikali ifanye yafuatayo
1.Lazima tujihusishe na kutafuta amani directly ndani ya DRC Ikibidi Kwa gharama zetu.

2.Lazima Sgr na Barabara zivuke na kuifikia DRC(Bukavu,Goma,Kinshasa,Kindu)

3.Lazima tuwashawishi Zambia na DRC tujenge reli kutoka Tunduma-Kasama-Lubumbashi-Likasi na Kutoka Makambako-Mtwara Port.

4.Lazima Sgr itoke Mpanda-Karema na Kigoma

5.Lazima tutafute pesa za kujenga meli kubwa za mizigo na abiaria ndani ya Ziwa Viktoria na pia tujenge Bandari,Barabara na reli upande wa DRC hata Kwa kuwakomesha pesa

6.Lazima tuwape DRC,Rwanda na Burundi Ardhi za Bure za kumhudumia mizigo Yao Pwani.

My Take
Tusipofanya hayo tunaenda kupoteza hata hiyo DRC Kwa Kenya,Angola na Mozambique na ikizingatiwa DRC inajenga Bandari na reli kuunganisha na Zambia na Angola.

Washindani Wetu wa Kenya wao Wana uhakika na Uganda,South Sudan, Northern DRC na somehow Ethiopia na Rwanda.

Tuachane na Mpango wa kujenga reli ya Mtwara Corridor hiyo Haina maana tena imeshakufa,Nguvu zote zielekezwe Kujenga kioande Cha kutoka Makambako -Mtwara.
View attachment 3080431
Una hoja za msingi....lakini pia umeweka hofu zaidi....
1.DRC atabaki kuwa mteja wetu for 50 years more
  • Miji Tajiri kwa madini(Katanga,Tangayika na Kasai) ipo karibu zaidi na Tanzania kuliko Kenya....
  • Corridor ya Kaskazini Mashariki ndiyo ina vita
  • Kutoka Kongo Kusini kwenda Kaskazini,Jiografia ni Korofi,,,Misitu mikubwa matawi ya Mto Kongo ni mengi mno
  • Kumbuka pia,hata DRC imegusa bahari
2.Zambia
  • Wanacho kifanya ni kuondoa utegemezi wa nchi moja, siyo kwamba kuachana na Tanzania moja kwa moja,,,hiyo ipo hata kwa Uganda,anatumia Bandari zote mbili,za Kenya na Tz.
  • Pia Kumbuka ,Akitolea Msumbiji, inabidi ajiandae na kodi za nchi mbili,Msumbiji na Malawi,,wakati huku mzigo wote unapitia nchi moja.
3.Angola
  • Hawezi kutupora mteja kwani ,Afrika tunategemea mizigo from Asia kuliko Amerika

Bandari zetu bado zitahitajika....tu
 
Ilifika
Ngonjera au siyo? Mda utasema.Tutafika mahala Bandari zetu zitakuwa zinategemea zaidi mzigo wa ndani ya Nchi zaidi kuliko wa Nje ya Nchi kama ilivyo Sasa hivi.
Ikifikia huko ina maana tutakuwa tumeendelea sana kiuzalishaji....and it's a good thing.
 
Ndio kwanza DP World wameanza Ujenzi wa Bandari nyingine DRC

Wao wanachojali ni kufanya biashara ya Bandari bila kujalisha volume ya mzigo Kwa sababu wanachowekeza ni Kufanya oparesheni tuu DP World Yazidi Kujichimbia Mizizi Afrika,Yajitosa DRC Congo Kuwajengea Bandari Kubwa Itakayounganisha Bahari ya Atlantic na Bahari ya Hindi.
Mkuu hao DP World kabla ya kuwekeza hapa Tanzania walifanya upembuzi yakinifu, hapo msumbiji Beira port wao wapo. Hiyo Bandari ya Banana wanajenga na wamelenga mizigo yote inayopita Atlantic ocean.

Nilibahatika kukutana Director mmoja wa DP World anasema Target yao kubwa kuwa operators wa bandari zote upande Africa pia Mombasa Port wameiweka kwenye target ya kuichukua. Hapo Somalia tayari DP World anafanya kazi
 
Tukubali kwamba hatuna guts na uwezo wa kuona fursa za kiuchumi mapema na intelligence ya kuzifikia.
Huyu mchechu ndio tumempa mambo ya planning na yeye ukufuatilia kariba yake ni uongozi wa mabenk na kujineemesha yeye mwenyewe.
 
Mwaka 2019 DP world waliingia Rwanda na kuanzisha Economic Processing Zone na Logistics Centre. Hawafanyi kwa kubahatisha kuipata Dar Port ni mafanikiko, hiyo mizigo ya Congo,Malawi,msumbiji,Zambia tayari wanahudumia kupitia Beira
 
Nchi ya Mozambique imeamua kuteka biashara ya Usafirishaji Kwa njia ya Maji Kwa Nchi zote za Sadc na kuiachia Tanzania maumivu makubwa.

Katika kutekeleza Hilo, Mozambique wameamua kuikodisha Bandari Yao ya Nacala Kwa Nchi ya Malawi na Zambia ambapo wataitumia Kwa kipindi Cha miaka 100 ijayo.

Nchi hizo 3 zinapanga kujenga miundombinu ya reli kutoka Nakala Hadi Mji Mkuu wa Malawi Lilongwe na kisha Hadi Mji Mkuu wa Zambia Lusaka.

Njia hiyo Mpya ya reli itapunguza umbali wa Zambia kuifikia Bandari ya Dar hivyo zaidi ya asilimia 90% ya mzigo wa Zambia utapitia Bandari za Msumbiji za Nakala na Beira.

Kwa hatua hiyo itakuwa ni pigo kubwa sana kwa Tanzania ambayo Bandari ya Dar ilikuwa inategemea zaidi mzigo wa Nchi ya Congo DRC na Zambia kama wateja Wakuu huko Nchi zingine zikiongesea ongezea shehena.

Endapo Zambia itaondoka rasmi kuwa mteja wa Tanzania sio tuu itapunguza mzigo wa Bandari ya Dar Bali itaua kabisa biashara ya Malori ya mizigo Tanzania ambapo Kwa sehemu kubwa yatahamia Nchi hizo za Zambia,Malawi na Msumbiji na zingine za Afrika Ili kuendelea na Biashara ya Usafirishaji.
View attachment 3080432

Pia soma: Bandari za Dar na Mtwara Kuwa Mashakani Kutokana na Nchi za Zambia,Malawi na Mozambique Kuzindua Upanuzi Mkubwa wa Miundombinu ya Nacala Port.

Kwa maelezo zaidi soma hapa Ili Kuongeza Ufanisi wa reli ya TAZARA,Tanzania na Zambia Ziiombe China Wajenge reli Mpya ya Makambako-Mtwara & Kasama-Lubumbashi/Likasi

Ushauri,;

Serikali ihakikishe mipango yetu yote Kwa Sasa iwe inalenga kuikumbatia DRC kuanzia Kusini Hadi Kaskazini maana ndio mteja pekee ambae walau jiografia inatupa nafasi.

Serikali ifanye yafuatayo
1.Lazima tujihusishe na kutafuta amani directly ndani ya DRC Ikibidi Kwa gharama zetu.

2.Lazima Sgr na Barabara zivuke na kuifikia DRC(Bukavu,Goma,Kinshasa,Kindu)

3.Lazima tuwashawishi Zambia na DRC tujenge reli kutoka Tunduma-Kasama-Lubumbashi-Likasi na Kutoka Makambako-Mtwara Port.

4.Lazima Sgr itoke Mpanda-Karema na Kigoma

5.Lazima tutafute pesa za kujenga meli kubwa za mizigo na abiaria ndani ya Ziwa Viktoria na pia tujenge Bandari,Barabara na reli upande wa DRC hata Kwa kuwakomesha pesa

6.Lazima tuwape DRC,Rwanda na Burundi Ardhi za Bure za kumhudumia mizigo Yao Pwani.

My Take
Tusipofanya hayo tunaenda kupoteza hata hiyo DRC Kwa Kenya,Angola na Mozambique na ikizingatiwa DRC inajenga Bandari na reli kuunganisha na Zambia na Angola.

Washindani Wetu wa Kenya wao Wana uhakika na Uganda,South Sudan, Northern DRC na somehow Ethiopia na Rwanda.

Tuachane na Mpango wa kujenga reli ya Mtwara Corridor hiyo Haina maana tena imeshakufa,Nguvu zote zielekezwe Kujenga kioande Cha kutoka Makambako -Mtwara.
View attachment 3080431
Bandari si ya Tanzania Bali ya AUE
 
Ngonjera au siyo? Mda utasema.Tutafika mahala Bandari zetu zitakuwa zinategemea zaidi mzigo wa ndani ya Nchi zaidi kuliko wa Nje ya Nchi kama ilivyo Sasa hivi.
Hii sio sahihi, tayari DP world yupo Rwanda na logistics centre. Mizigo ya Rwanda na Kongo mashariki kaweka mazingira ya kuja Dar.

Dp world sio nchi zenye bandari tu ndio anawekeza, anawekeza mpaka Land Locked countries kwa kuweka vituo vya Logistics
 
Mwaka 2019 DP world waliingia Rwanda na kuanzisha Economic Processing Zone na Logistics Centre. Hawafanyi kwa kubahatisha kuipata Dar Port ni mafanikiko, hiyo mizigo ya Congo,Malawi,msumbiji,Zambia tayari wanahudumia kupitia Beira
Kagame aliifungua hiyo economic zone mwaka jana, walishajipanga kwa muda mrefu kwamba mzigo huo wote ni lazima upitie bandari ya Dar kwenda huko nje.

Hiyo ni logistic chain nzima kaishikilia DPW, hivyo anayehoji kwanini tenda haijatangazwa huyo hafahamu kuhusu DPW kuwa tayati anayo economic zone huko Rwanda tangu mwaka 2019.

Tenda aliyopewa DPW ya kuendesha magati ya TPA iliangalia mchakato mzima wa kuutoa huo mzigo Rwanda na kuupitisha kwenye bandari ya Dar kisha ukaenda huko kwa mteja wa mwisho.
 
Umeandika points nyingi. Safi sana. Mimi nadhani pia DP World waanze na jambo dogo sana la kutoa mizigo bandarini kwa haraka. Kwa sasa mzigo kutoka inachukua hadi wiki 3 tangu meli kufika Tanzania. Inashangaza kwasababu tuliambiwa ingechukua muda mfupi zaidi. Bandari ya Nacala ni tishio ila maboresho yakifanyika bado TZ haitayumba kibiashara. Bandari ya Mtwara ikifanyiwa kazi itasambaratisha hilo suala la Nacala.
 
angola nao wamejenga reli kutoka lubumbashi hadi Lobito tayari shehena ya kwanza ya shaba kwenda us imeshawasili bandarini salama, halafu sisi tuko busy na wamasai wa ngorongoro
Ile itaisha 2029, wanaiboresha...maumivu ni makali
 
Umeandika points nyingi. Safi sana. Mimi nadhani pia DP World waanze na jambo dogo sana la kutoa mizigo bandarini kwa haraka. Kwa sasa mzigo kutoka inachukua hadi wiki 3 tangu meli kufika Tanzania. Inashangaza kwasababu tuliambiwa ingechukua muda mfupi zaidi. Bandari ya Nacala ni tishio ila maboresho yakifanyika bado TZ haitayumba kibiashara. Bandari ya Mtwara ikifanyiwa kazi itasambaratisha hilo suala la Nacala.
Mkuu suala la mzigo kuchukua wiki 3 nadhani sio upande wa DP World. Anayekuchelewesha ni agent wako
 
Tatizo ni viongozi ...nchi kama Rwanda iko vizuri kiuchumi na ni ka nchi kadogo tu.Lakini Tz bonge la nchi na lasimali kibao ila viongozi hatuna ...so sad 🥺Maana taifa kama halina viongozi wenye maono na wakimbilia fulsa sio mikopo nchi hii ingekua mbali sana.
Issue sio viongozi, ila jamii ya watanzania ni wajinga sana. Tumeona wasomi hata wa kiwango cha PhD wameongopeana sana kuhusu mkataba wa Bandari hapa hadi unajiuliza kama usomi wetu una maana gani. Unadhani ingetokea Tanzania ndio imekodisha bandari ya Mtwara kwa Malawi au Zambia au Congo hizo kelele pangetosha kweli?

Kiukweli tuna kundi kubwa tu la wasomi halafu wajinga nchi hii. Wanachojua ni kuiba hela halafu kunywa pombe na kuiba wake za watu au wanachuo. Angalia kelele za Ngorongoro, ni ujinga wa kundi hilohilo la wasomi. Ni ngumu sana kufanya radical reforms katika nchi yetu tofauti na tunavyodhani.
 
Nchi ya Mozambique imeamua kuteka biashara ya Usafirishaji Kwa njia ya Maji Kwa Nchi zote za Sadc na kuiachia Tanzania maumivu makubwa.

Katika kutekeleza Hilo, Mozambique wameamua kuikodisha Bandari Yao ya Nacala Kwa Nchi ya Malawi na Zambia ambapo wataitumia Kwa kipindi Cha miaka 100 ijayo.

Nchi hizo 3 zinapanga kujenga miundombinu ya reli kutoka Nakala Hadi Mji Mkuu wa Malawi Lilongwe na kisha Hadi Mji Mkuu wa Zambia Lusaka.

Njia hiyo Mpya ya reli itapunguza umbali wa Zambia kuifikia Bandari ya Dar hivyo zaidi ya asilimia 90% ya mzigo wa Zambia utapitia Bandari za Msumbiji za Nakala na Beira.

Kwa hatua hiyo itakuwa ni pigo kubwa sana kwa Tanzania ambayo Bandari ya Dar ilikuwa inategemea zaidi mzigo wa Nchi ya Congo DRC na Zambia kama wateja Wakuu huko Nchi zingine zikiongesea ongezea shehena.

Endapo Zambia itaondoka rasmi kuwa mteja wa Tanzania sio tuu itapunguza mzigo wa Bandari ya Dar Bali itaua kabisa biashara ya Malori ya mizigo Tanzania ambapo Kwa sehemu kubwa yatahamia Nchi hizo za Zambia,Malawi na Msumbiji na zingine za Afrika Ili kuendelea na Biashara ya Usafirishaji.
View attachment 3080432

Pia soma: Bandari za Dar na Mtwara Kuwa Mashakani Kutokana na Nchi za Zambia,Malawi na Mozambique Kuzindua Upanuzi Mkubwa wa Miundombinu ya Nacala Port.

Kwa maelezo zaidi soma hapa Ili Kuongeza Ufanisi wa reli ya TAZARA,Tanzania na Zambia Ziiombe China Wajenge reli Mpya ya Makambako-Mtwara & Kasama-Lubumbashi/Likasi

Ushauri,;

Serikali ihakikishe mipango yetu yote Kwa Sasa iwe inalenga kuikumbatia DRC kuanzia Kusini Hadi Kaskazini maana ndio mteja pekee ambae walau jiografia inatupa nafasi.

Serikali ifanye yafuatayo
1.Lazima tujihusishe na kutafuta amani directly ndani ya DRC Ikibidi Kwa gharama zetu.

2.Lazima Sgr na Barabara zivuke na kuifikia DRC(Bukavu,Goma,Kinshasa,Kindu)

3.Lazima tuwashawishi Zambia na DRC tujenge reli kutoka Tunduma-Kasama-Lubumbashi-Likasi na Kutoka Makambako-Mtwara Port.

4.Lazima Sgr itoke Mpanda-Karema na Kigoma

5.Lazima tutafute pesa za kujenga meli kubwa za mizigo na abiaria ndani ya Ziwa Viktoria na pia tujenge Bandari,Barabara na reli upande wa DRC hata Kwa kuwakomesha pesa

6.Lazima tuwape DRC,Rwanda na Burundi Ardhi za Bure za kumhudumia mizigo Yao Pwani.

My Take
Tusipofanya hayo tunaenda kupoteza hata hiyo DRC Kwa Kenya,Angola na Mozambique na ikizingatiwa DRC inajenga Bandari na reli kuunganisha na Zambia na Angola.

Washindani Wetu wa Kenya wao Wana uhakika na Uganda,South Sudan, Northern DRC na somehow Ethiopia na Rwanda.

Tuachane na Mpango wa kujenga reli ya Mtwara Corridor hiyo Haina maana tena imeshakufa,Nguvu zote zielekezwe Kujenga kioande Cha kutoka Makambako -Mtwara.
View attachment 3080431
Imagine Tanzania ndio ingekuwa imekodisha bandari ya Mtwara kwa nchi hizo, hali ingekuwaje? Wanaharakati fake wangekuwa wamepata hoja ya kupayuka mwezi mzima.
 
Issue sio viongozi, ila jamii ya watanzania ni wajinga sana. Tumeona wasomi hata wa kiwango cha PhD wameongopeana sana kuhusu mkataba wa Bandari hapa hadi unajiuliza kama usomi wetu una maana gani. Unadhani ingetokea Tanzania ndio imekodisha bandari ya Mtwara kwa Malawi au Zambia au Congo hizo kelele pangetosha kweli?

Kiukweli tuna kundi kubwa tu la wasomi halafu wajinga nchi hii. Wanachojua ni kuiba hela halafu kunywa pombe na kuiba wake za watu au wanachuo. Angalia kelele za Ngorongoro, ni ujinga wa kundi hilohilo la wasomi. Ni ngumu sana kufanya radical reforms katika nchi yetu tofauti na tunavyodhani.
Mtanzania anataka afanye kazi ya milioni mbili apokee mshahara wa milioni kumi. Ufahari mwingi wa kijinga na ujuaji kwenye maongezi ya kawaida tu.

Suala la bandari limewaaibisha sio wasomi wa fani nyingine pekee yao mpaka wanasheria tena waalimu wa pale Mlimani wa muda mrefu. Wakajikuta wakiwadanganya watanzania wengi wenye elimu ndogo na kuwapotosha juu ya ukweli wenyewe wa suala husika.
 
Una hoja za msingi....lakini pia umeweka hofu zaidi....
1.DRC atabaki kuwa mteja wetu for 50 years more
  • Miji Tajiri kwa madini(Katanga,Tangayika na Kasai) ipo karibu zaidi na Tanzania kuliko Kenya....
  • Corridor ya Kaskazini Mashariki ndiyo ina vita
  • Kutoka Kongo Kusini kwenda Kaskazini,Jiografia ni Korofi,,,Misitu mikubwa matawi ya Mto Kongo ni mengi mno
  • Kumbuka pia,hata DRC imegusa bahari
2.Zambia
  • Wanacho kifanya ni kuondoa utegemezi wa nchi moja, siyo kwamba kuachana na Tanzania moja kwa moja,,,hiyo ipo hata kwa Uganda,anatumia Bandari zote mbili,za Kenya na Tz.
  • Pia Kumbuka ,Akitolea Msumbiji, inabidi ajiandae na kodi za nchi mbili,Msumbiji na Malawi,,wakati huku mzigo wote unapitia nchi moja.
3.Angola
  • Hawezi kutupora mteja kwani ,Afrika tunategemea mizigo from Asia kuliko Amerika

Bandari zetu bado zitahitajika....tu
Nacala port,Beira no zipo upande wa Atlantic?
 
Ujinga tuu umewajaa watu wasioelewa
Kuna wakati tunalaumu viongozi ila kuna watu hata hawako Serikalini lakini wana nguvu ya kujaza ujinga kwa watanzania hadi unashangaa. Tuna akili za muda mfupi sana. Kila kitu chenye long term impact kinapingwa.

Angalia program ya BBT imavyopingwa kwa ujinga. Tutawezaji kufikia kilimo cha maana kama hujaanzisha programs za kuwa na mashamba makubwa yenye miundombinu yote. To be honest, tuna ujinga mwingi sana kama nchi.
 
Mwaka 2019 DP world waliingia Rwanda na kuanzisha Economic Processing Zone na Logistics Centre. Hawafanyi kwa kubahatisha kuipata Dar Port ni mafanikiko, hiyo mizigo ya Congo,Malawi,msumbiji,Zambia tayari wanahudumia kupitia Beira
Mimi Sina tatizo na Rwanda na Burundi,hizo ni lazima watumie Dar Port Kwa sababu ndio njia fupi kwao,swala ni DRC na Zambia.

Kwa Zambia Bandari za jirani kwake ni Nacala,Beira na Lobito the same applies to DRC.

Wanatumia Dar Kwa sababu ya kukosa ufanisi kwenye Bandari hizo za Mozambique na kama ujiavyo so far wateja wakubwa wa Tanzania ni Zina na DRC
 
Back
Top Bottom