Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
MTAA WA JOHN RUPIA TANGA
Moja ya vibao vingi vya Mtaa wa John Rupia kipo pembeni ya Msikiti Ngazija, Tanga.
Nimefikia hoteli jirani na kwa hakika ni mkabala na msikiti huu na ndiyo nikabahatika kuona kibao hicho.
Nilipata kuwauliza wahusika miaka mingi nyuma wakati naishi Tanga walipotoa jina la ''Maua,'' kwa mtaa mmoja mkubwa Ngamiani.
Niliuliza ''Maua'' ina maana gani katika historia ya Tanga?
Nikasema kwa nini mtaa ule haukupewa jina la Hamisi Heri au Abdallah Rashid Sembe waasisi wa TANU na wapigania uhuru wa Tanganyika?
Sikupata jibu?
Nilipoona kibao cha John Rupia, Tanga nilijisemeza moyoni kwangu nikajiambia, ''John Rupia tayari ana mtaa Dar es Salaam,
Kwa nini mtaa huu haukupewa jina la mpigania uhuru mwingine kutoka Tanga aliyeacha alama kubwa katika harakati za uhuru, mathalan mtu kama Peter Mhando kijana aliyeitumikia TANU lakini akafa mapema mwaka wa 1958 kabla ya uhuru kupatikana?
Hapana sababu ya kurudia majina ya viongozi ambao tayari tumeshawaadhimisha.
Moja ya vibao vingi vya Mtaa wa John Rupia kipo pembeni ya Msikiti Ngazija, Tanga.
Nimefikia hoteli jirani na kwa hakika ni mkabala na msikiti huu na ndiyo nikabahatika kuona kibao hicho.
Nilipata kuwauliza wahusika miaka mingi nyuma wakati naishi Tanga walipotoa jina la ''Maua,'' kwa mtaa mmoja mkubwa Ngamiani.
Niliuliza ''Maua'' ina maana gani katika historia ya Tanga?
Nikasema kwa nini mtaa ule haukupewa jina la Hamisi Heri au Abdallah Rashid Sembe waasisi wa TANU na wapigania uhuru wa Tanganyika?
Sikupata jibu?
Nilipoona kibao cha John Rupia, Tanga nilijisemeza moyoni kwangu nikajiambia, ''John Rupia tayari ana mtaa Dar es Salaam,
Kwa nini mtaa huu haukupewa jina la mpigania uhuru mwingine kutoka Tanga aliyeacha alama kubwa katika harakati za uhuru, mathalan mtu kama Peter Mhando kijana aliyeitumikia TANU lakini akafa mapema mwaka wa 1958 kabla ya uhuru kupatikana?
Hapana sababu ya kurudia majina ya viongozi ambao tayari tumeshawaadhimisha.