KERO Mtaa wa Kisonge na Mtaa wa Bin Abeid (Zanzibar) maji taka yanasambaa mitaani na barabara ni mbovu

KERO Mtaa wa Kisonge na Mtaa wa Bin Abeid (Zanzibar) maji taka yanasambaa mitaani na barabara ni mbovu

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Sisi Wakazi wa Mtaa wa Kisonge na Mtaa wa Bin Abeid hapa Mkoa wa Mjini Magharibi tuna changamoto ya mifumo ya Maji taka kutowekwa katika mazingira mazuri na kwa ufupi ni kuwa Miundombinu imeharibika lakini Viongozi wetu hawachukui hatua.
IMG_1659.jpeg
Kuna mabomba na chemba za majitaka zinavujisha maji machafu ambayo yanasamba hapa mtaani kwetu.
IMG_1658.jpeg
Wakati huohuo hali ya Barabara zenu nazo sio nzuri, kutokana na ubovu maji yametuama na kusababisha kero zaidi kwetu wakati wa kupita.
IMG_1655.jpeg


Watoto wetu wanapita katika maeneo yenye maji machafu na wengine wanayachezea, tunaomba viongozi wanaohusika wafanye jambo kurekebisha hali hii kwa kuwa ni hatari kwa afya zetu wote.​

IMG_1661.jpeg
IMG_1656.jpeg
 

Attachments

  • IMG_1657.jpeg
    IMG_1657.jpeg
    433.5 KB · Views: 5
Back
Top Bottom