Hao ni wapiga kura wa zamani, wale vichwa vya kuku (wajinga), ambao hawajui wamchague nani mpaka wanaingia kituoni.
Siku hizi wananchi walio wengi wanayo elimu ya uraia, wameshafanya maamuzi mapema kabisa, ukiingia kituoni hata mgombea anayemtaka awe ukurasa wa tatu atatafutwa tu.
Kwahiyo NEC kama walidhani kumweka joni awe wa kwanza kutasaidia wamaulamba wa chuya.
Kampeni ya kuufahamisha umma Lissu huko wapi katika hiyo karatasi inaweza ikaeleweka nchi nzima ndani ya nusu SAA tuu. Mchawi technology.
Tatizo wanaweza kubadili alafu akala mweleka. Yaani Hii kitu ni hataree
Ninyi wawili wa kwanza kwa taarifa yako, bila kujali nafasi ya mgombea kwenye kura ya karatasi, kwa wagombea wa Urais Lissu amekwisha kupoteza kura za wafuatao, kutokana na kauli zake kwenye kampeni, nitarudi hapa ni kuwakumbusha:
√ waliopata vitambulisho vya Magufuli vya biashara ndogo na familia zao;
√ wanachama hai na waliojiandikisha kupiga kura wa CCM;
√ wananchi ambao si wanachama wa CCM ambao wanatambua mchango wa Magufuli kwa maendeleo ya nchi na wapenda amani (viongozi wa dini wanalisisitiza hili na wamepanga maombi ya siku 3 tena);
√ wafanyakazi wa serikali, na taasisi zake, waliokuwa wakicheleweshewa mishahara yao na waliopandishwa madaraja; na
√ mwisho lakini siyo mwisho kabisa, wafanyakazi wote wa kima cha chini ya laki 3 (300,000/-) waliofutiwa PAYEE, ambao kwa sasa pato la mshahara limeongezeka maradufu.
Utafiti wangu kwa makundi hayo (kila watu 10 niliongea nao kuhusu kura watampa nani na kwa sababu ipi ya msingi) wote (10) walitoa ahadi isiyo na mashaka watampa kura Magufuli kwa kuwa maamuzi yake yamegusa maisha yao moja kwa moja.
Na haya makundi (9/10) pia yameahidi kumpa kura Magufuli kwa sababu ya misimamo yake:
√ wazazi wenye watoto shuleni ambao hawakuwa na uwezo kulipa ada;
√ wazazi na wanachuo ambao walikuwa wanakosa ada;
√ wananchi ambao huduma za jamii (maji na afya) hazikuwepo;
√ wanavijiji waliopata huduma ya umeme;
√ wachimbaji wadogo wa madini kwa ujenzi wa msoko ya kuuzia madini yao;
√ wafanyakazi wa sekta ya utalii kwa kuendelea na biashara wakati nchi nyingi na hasa za jirani kuendelea kufunga mipaka yao;
√ mwisho lakini siyo mwisho kabisa, wafanya biashara, hasa ndogo ndogo, kuendelea na biashara wakati wa korona.