Mtaani Serikali ya Rais Samia inapoteza uungwaji mkono kwa kasi ya kutisha

Mtaani Serikali ya Rais Samia inapoteza uungwaji mkono kwa kasi ya kutisha

Missile of the Nation

JF-Expert Member
Joined
May 24, 2018
Posts
15,101
Reaction score
56,054
Salamu zimfikie ndugu Samia
Huku mtaani ndugu rais kuna malalamiko, wananchi wanasema hawakusomi, hawakuelewi, na nitakueleza nilichosikia huku mtaani!

1. Suala la tozo za miamala
Wananchi wanakusikilizia tu waone utafanya nini, lakini wameanza kuona dalili za wewe kupiga konakona. Kuna kila dalili ya hasira ya wananchi kuwa kubwa zaidi maana wanaona unawafanya kama watoto wadogo wa kudanganyadanganya

2. Uonevu wa jeshi la polisi juu ya wapinzani
Ndugu rais, sasa badala ya kushawishi kwa hoja, serikali yako imegeuka ya mabavu. Raia kwenye vijiwe vya kahawa, magazeti ya asubuhi wanashangazwa na miguvu unayotumia, wanauliza unawapeleka wapi?, mbona kila siku polisi wanaokamatakamata wapinzani, wamefanya kosa gani?

3. Kwenye Chanjo watu wanakwenda na kauli ya Magufuli kuwa chanjo hazifai
Binafsi naamini umeleta chanjo kwa nia njema, umefuata ushauri wa kisayansi. Hata hivyo sayansi ni kitu kimoja na perception ya wananchi ni kitu kingine, wananchi mtaani wanaamini kuna hela ya mzungu umechukua na unatafuta justification. Na hoja ambazo raia wanasema ni kuwa mbona wataalamu waliotwambia chanjo hazifai miezi michache iliyopita ndo haohao leo wanatwambia zinafaa, huko kufaa kumeanza lini. Watu wanaukubali msimamo wa hayati kwenye suala hili na wewe wanakuona kama mabeberu wamekuzidi nguvu

4. Influencers na kundi lililokuwa likikuunga mkono hapo awali linakukimbia kwa kasi
Wapo wale waliosimama kukutetea kwa hatua zako nzuri kabisa mwanzoni mwa utawala wako, watu kama akina Askofu Bagonza, watu wenye ushawishi mkubwa katika jamii. Leo hii wameanza kujidistance na wewe, wanasema mabaya unayoanza kuyatenda kwa kufanya utawala wa kimabavu kupitia jeshi la polisi yanafuta mazuri uliyoyatenda kwenye siku zako za awali za utawala. Wakati kundi hili likikukimbia, lile kundi linalomkumbuka hayati bado halijakukubali sana, kwa hiyo usipokuwa makini unapoteza uungwaji mkono wa umma hivihivi, Labda uegemeze nguvu zako kwa vijana wa Simon Sirro, lakini hao ni wachache hawafiki hata 50000 nchi nzima, Sijui utawezaje.

5. Miradi ya Hayati hata uisimamie na kuifanikisha vipi, wananchi wanampa credit hayati.
Japo kwenye hili mimi binafsi naona wananchi hawana hoja ya msingi kwa sababu serikali ni taasisi endelevu lakini ukweli ni kuwa huku mtaani bado hawajakuidentify na kitu chako binafsi
Mwanzo raia walisema labda wewe utakuwa mwanademokrasia, mtenda haki lakini mtu wa maendeleo, leo hiyo credit wamekuondolea kwa sababu ya ukandamizaji na uonevu serikali yako inayoufanya kwa wapinzani, lakini wakati huohuo hata miradi unayoendelea kuifanya (Kitu ambacho ni kizuri) raia wanakuona unakamilisha kazi ya Magufuli. Ukipokea ndege, wanasema ni Magufuli huyo, Raia hawajakuelewa wewe ni Magufuli asiye Magufuli, Au ni Muungwana asiye Muungwana?

Mwisho:
Ndugu rais watanzania ni wapole sana lakini wakikuchukia watakuchukia kwelikweli. TENDA HAKI NA EPUKA UONEVU ili ukistaafu wakukumbuke kwa wema la sivyo watakunyanyapaa sana, Haya madaraka huwa yanaisha na yanapita usijisahau sana!
 
Huyu mama hakua tayari kushika nafasi hiyo nyeti. Mambo ya mipasho kwenye maisha ya watu ni sumu.

Amini nakuambia hakuna hata mmoja anayemuunga mkono. Sio ccm wenzake sio sisi tusio na chama sio kwa wapinzani.

Amegusa pabaya sana tena wakati mbaya ambao watu wanahangaika wapate japo mlo mmoja
 
Huyu mama hakua tayari kushika nafasi hiyo nyeti. Mambo ya mipasho kwenye maisha ya watu ni sumu.

Amini nakuambia hakuna hata mmoja anayemuunga mkono. Sio ccm wenzakez sio sisi tusio na chama sio kwa wapinzani.

Amegusa pabaya sana tena wakati mbaya ambao watu wanahangaika wapate japo mlo mmoja
Halafu it seems wanamshika Masikio abadili maamuzi ambayo instinct zake zinamwambia ni sahihi, lakini wahafidhina wanamwambia komaa hivyohivyo!
Naamini kwenye miamala akina Mpango, Mwigulu na Ndugai watakuwa wamemshawishi arudi nyuma
 
Huyu mama hakua tayari kushika nafasi hiyo nyeti. Mambo ya mipasho kwenye maisha ya watu ni sumu.

Amini nakuambia hakuna hata mmoja anayemuunga mkono. Sio ccm wenzakez sio sisi tusio na chama sio kwa wapinzani.

Amegusa pabaya sana tena wakati mbaya ambao watu wanahangaika wapate japo mlo mmoja
tatizo hakuna anaeweza kufanya chochote. unaweza ona sheria zetu zinampa mtu mwanya wa kufanya lolote na taasis zita support.. akija mwingine atafanya hivyo.hivyo.. hatuna scope
 
Halafu it seems wanamshika Masikio abadili maamuzi ambayo instinct zake zinamwambia ni sahihi, lakini wahafidhina wanamwambia komaa hivyohivyo!
Naamini kwenye miamala akina Mpango, Mwigulu na Ndugai watakuwa wamemshawishi arudi nyuma
Unakuaje rais na unashikiwa masikio? Ndio maana nikasema hakua tayari kuwa kwenye nafasi hiyo. Magufuli aliitumia ipasavyo hiyo nafasi japo hakua na maono. Laiti angekua na maono, angetufikisha mbali sana. Hakuyumbushwa kwa kile alichokiamini yeye
 
Mitaa ipi??Huku nnapokaa watu hawajadili siasa kabisa..hawana hata time na mijadala..

Ukiingia JF ndo unakuta malalamiko tele..

Huku mitaani no body cares that much
Umejaribu kuongea nao? Au ulitaka kila ukipita uwe unasikia habari za tozo....tozo....tozo...

Ukitaka kujua watu wanatembea nayo, jaribu hata kumuongelesha yeyote kuhusu mtazamo wake juu ya hizi tozo mpya za uzalendo.

Alafu uje uniambie ni wangapi wanasema imekaa vizuri na inatekelezeka.

Pia huenda unajitenda na watu ndio maana huwezi kusikia
 
Mitaa ipi??Huku nnapokaa watu hawajadili siasa kabisa..hawana hata time na mijadala..

Ukiingia JF ndo unakuta malalamiko tele..

Huku mitaani no body cares that much
Boss, watu wa mtaani kwako ndio sisi tuko huku JF.

Mtaani hakuna Uhuru, watu wanayasema nyuma ya keyboard.

Enewei, leo nmeyagusa machungu ya Makato sikua mlalamikaji before ila kwa hili la kutuma hela shamba leo nimejua kwa nini Watanzania wengi wanalalamika.
 
Kosa halianzii kwake bali linaanzia kwa Mwendazake alipomteua kuwa Mgombea mwenza.

Bazungu balonga; it is a vicious cycle.
Nadhani walimteua kwa mazoea tu maana waliamini rais ni lazima amalize mihura yake yote. Na sioni dalili za yeye kugombea nafasi ya urais 2025
 
Hiyo ya 3 ungeiacha kwa sababu na Mboe pia inatoa povu sana na hiyo biashara hatuelewi, yaani yeye na mama ni wamoja.
Ya 4 hilo kundi unalolisema ni wapinzani hasa wa Ufipa walimfurahia sana mama ila mara alipotia pini yote ndiyo tumeanza kusikia kelele za maumivu zinasikika kama vile siyo wao (ninyi) mnaosemaga CCM ni ile ile. Au mkisema mnaonea tu, eleweni ni kweli CCM ni ile ile.

No. 2 mi naona CCM na polisi vinatimiza wajibu wao kwani nchi kama Zambia, Malawi na nchi nyingine nyingi za kiAfrika zimebadirisha vyama sana katika nchi zao kwa maana ya democrasia lakini maisha yao na maendeleo yamezidi kuwa duni tofauti na tulivyoambiwa kuwa muharobaini wa matatizo ya Afrika ni democrasia. Kule Libya ndiyo usiseme, hivyo leo uwezi kumdanganya mtu kuwa CCM ikiondoka madarakani maisha yatakuwa mzuri huwezi. Au usema Chadema ikichukuwa nchi maisha yatakuwa mazuri uwezi.

We unachotakiwa ni kufanya ni kumtii na kumsikiliza Mungu tu katika biblia amesema tiini mamlaka sasa wewe umeanza uchochezi ukiamishiwa maisha yako Stakishari hata week moja tu utaaza kununa alafu unaandika unaonewa sasa uonevu gani ujui maana ya mamlaka. Sasa kama CCM hakina sifa ya umiliki wa mtu fulani je ukiwapa Chadema ambao chama kinajulikana kabisa mwenyewe si watanzania watauzwa kama enzi za utumwa.
 
Back
Top Bottom