Mtaje mshikaji wako ambae akipata Mil 1, una uhakika wa kupata laki moja,au hata Afutatu tu

Mtaje mshikaji wako ambae akipata Mil 1, una uhakika wa kupata laki moja,au hata Afutatu tu

Kuna mshikaji wangu yupo taasisi fulani, akipiga mshindo ananipigia simu anauliza uko wapi? Kwanza sauti tu ntajua ehee! Kimelipuka huko.

Basi utasikia anasema wewe mjinga upo chini ya ulinzi, hapohapo ulipo kama ulikuwa unafanya kazi acha, kama unakula acha. Fasta chukua bodaboda au tax nipo sehemu fulani nalipa hukuhuku.

Basi nikifika nakuta jamaa kakaa anapata safari lager za baridi zinatoa jasho aisee! Huku kaagiza nyama safi nyeupe ambayo haina madhara na kachumbali pilipili. Hapo tutakunywa kula na hela za supu naondoka nayo.
Kwanza kwenye meza yetu wahudumu wanakuwa hawakauki.
Na mimi nikipiga mshindo vilevile kama yeye.
Hii dunia ni tamu jamani ukiamua.
 
Nina uhakika hiyo Aftatu
Demi hawezi kukosa kunipa au atanipa hiyo 1M yote ili yeye aanze upya.
 
Mtaje mshikaji wako ambae akipata Mil 1, una uhakika wa kupata laki moja,au hata Afutatu tu

Tuonyeshe love,kwa rafiki zetu wanaotupenda na kutupigania!
Mshikaji wangu akipata milioni moja sitegemei kunipa hata laki moja ila itabidi mie ndio nikae chini kumkumbusha nani asimsahau kumgawia katika familia yake. Maana alivyo na familia kubwa na akiaamua kiigawa hiyo milioni moja kwa familia yake yote basi yeye mwenyewe atabaki na mia moja tu
 
Asee mimi Sina huyo mshikaji wengi tu nikiona simu zao najua huwa wanataka msaada tu.
 
Mshikaji wangu wa ukweli run CMD akipata huwa hajali ananipa yote kabisa..akipata chochote najua lazima nitachia meno yote nje kwa shangwe..namkubali
 
Back
Top Bottom