Mtaji wa milioni 3 unatosha kufungua duka la dawa?

Lyugi sana

Member
Joined
Dec 11, 2020
Posts
31
Reaction score
19
Nina pesa kama nilivyoiainisha hapo juu,

Na ninahitaji kufanya biashara ya duka la dawa na sina kitu hata kimoja zaidi ya pesa yangu mfukoni. Je, nikianza harakati sitoishia njiani?

Zaidi soma:

 
Ninapesa kama nilivyoiainisha hapo juu, na ninahtaji kufanya biashara ya duka la dawa na sina kitu hata kimoja zaidi ya pesa yangu mfukoni je, nikianza harakati sitoishia njian?
Dawa za binadamu au nini?
 
Ungejaribu pia na fursa nyingine kuangalia kwa mtaji huo kama:-

1. Uchuuzi wa mazao
2. Mobile money Mpesa, tigopesa airtel money ikiichanganya biashara na vitu vingine hasa Gas na vinywaji jumla na rejareja.
3. Nguo na viatu vya mtumba.

Kwa duka la dawa naona kama ndogo ukizingatia vibali vya duka hilo na kuiwezesha office iwe ya duka la dawa kweli kwa kuwa aircondition yatakiwa hapo, waweza jikuta lisifanikiwe ila endelea kupima uzito.
 
Hiyo namba moja, unaweza ambiwa onesha shamba lako
 
Mkuu pamoja na wengine wanaopinga kua m3 haianzishi duka la muhimu mnachanganya mambo kua pharmacy na duka la dawa muhimu(DLDM) ni vitu viwili tofauti.

Sent from my M2004J19C using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…