Mtakuja primary school na english ya Shule ya Msingi

Mtakuja primary school na english ya Shule ya Msingi

Mshinga

JF-Expert Member
Joined
Feb 5, 2013
Posts
3,532
Reaction score
1,126
nimeikumbuka hii story ya Mtakuja primary school shule ya msingi. Hoja si hiyo.

Hivi nini msaada na ufanisi wa somo la kiingereza shule za msingi za serikali?

Kila mtu ana maoni yake ila mimi sioni kabisa msaada wa hili somo hata likifutwa, nilimaliza shule ya msingi sijui chochote kuhusu kiingereza
 
Ujinga wako usituletee jamvini. Unamaanisha nini? Kama hujui ni upuuzi wako. Kwani kama itakuwa ni hoja mbona watu wanamaliza form four na English bado haijakaa vizuri kichwani? Mimi nilisoma tanzania nikamaliza darasa la saba nikijua kuongea sentensi za kiingereza. Nilikuwa natilia juhudi binafsi nikijua mwalimu hawezi kukupatia asilimia zote. Ila namshukuru Mungu waalimu wangu hawakuwa wabaya. Walinitia moyo na kufanya yote yawezekane. Pole kwa uzembe wako. Kesho utuambie na Hesabu iondolewe. Maskini wa ubongo.
 
Ujinga wako usituletee jamvini. Unamaanisha nini? Kama hujui ni upuuzi wako. Kwani kama itakuwa ni hoja mbona watu wanamaliza form four na English bado haijakaa vizuri kichwani? Mimi nilisoma tanzania nikamaliza darasa la saba nikijua kuongea sentensi za kiingereza. Nilikuwa natilia juhudi binafsi nikijua mwalimu hawezi kukupatia asilimia zote. Ila namshukuru Mungu waalimu wangu hawakuwa wabaya. Walinitia moyo na kufanya yote yawezekane. Pole kwa uzembe wako. Kesho utuambie na Hesabu iondolewe. Maskini wa ubongo.
kujua visentensi viwili vitatu ndio fahari yako? lugha unapofundishwa unapaswa kujua kuiandika, kuisoma, na kuizungumza kwa mawasiliano, wewe uliambulia lipi kati ya hayo kama si utoto wa fikra unakusumbua?
 
mwalimu wako mbovu mim nilijua kiingereza nikiwa nasoma shule ya msingi... tena msondo ngoma
 
mwalimu wako mbovu mim nilijua kiingereza nikiwa nasoma shule ya msingi... tena msondo ngoma
ukawa na uwezo wa kuwasiliana kwa kiingereza kama kiswahili na ukawa na uwezo wa kusoma na kuelewa maandiko ya kiingereza rahisi kama kiswahili na ukawa na uwezo wa kuandika mawazo yako kwa kiingereza? nahisi unamheshimu Mungu. majibu tafadhali
 
ukawa na uwezo wa kuwasiliana kwa kiingereza kama kiswahili na ukawa na uwezo wa kusoma na kuelewa maandiko ya kiingereza rahisi kama kiswahili na ukawa na uwezo wa kuandika mawazo yako kwa kiingereza? nahisi unamheshimu Mungu. majibu tafadhali

Watu wanapata walau msingi wa hiyo lugha mkuu. Kwa swali lako kwa miss chagga ni sawa na kutaka mtoto wa darasa la saba aweze kufanya integration kisa kasoma hesabu.
 
Last edited by a moderator:
Watu wanapata walau msingi wa hiyo lugha mkuu. Kwa swali lako kwa miss chagga ni sawa na kutaka mtoto wa darasa la saba aweze kufanya integration kisa kasoma hesabu.
nataka ajibu yeye, kwa kuwa unamsaidia well, soma vizuri hoja maana hujaelewa pia, kiswali nilifundishwa kuanzia la kwanza nikapata uwezo wa kusoma kiswahili, kuandika na kuiongea kiswahili pamoja na kwamba lugha yangu toka utotoni ilikuwa kisukuma. kwa hiyo nilitegemea kiingereza nikielewe kama kiswahili
 
Last edited by a moderator:
Ujinga wako usituletee jamvini. Unamaanisha nini? Kama hujui ni upuuzi wako. Kwani kama itakuwa ni hoja mbona watu wanamaliza form four na English bado haijakaa vizuri kichwani? Mimi nilisoma tanzania nikamaliza darasa la saba nikijua kuongea sentensi za kiingereza. Nilikuwa natilia juhudi binafsi nikijua mwalimu hawezi kukupatia asilimia zote. Ila namshukuru Mungu waalimu wangu hawakuwa wabaya. Walinitia moyo na kufanya yote yawezekane. Pole kwa uzembe wako. Kesho utuambie na Hesabu iondolewe. Maskini wa ubongo.

mh mh hyo ngumu kumeza lazima atapike huyo mleta mada.
 
nataka ajibu yeye, kwa kuwa unamsaidia well, soma vizuri hoja maana hujaelewa pia, kiswali nilifundishwa kuanzia la kwanza nikapata uwezo wa kusoma kiswahili, kuandika na kuiongea kiswahili pamoja na kwamba lugha yangu toka utotoni ilikuwa kisukuma. kwa hiyo nilitegemea kiingereza nikielewe kama kiswahili

Sijiu nafasi yako lakini mimi binafsi nilisoma primary za serikali na kwa kiingereza hicho hicho cha primary niliweza kuomba maji na kufanya mitihani ya kujiunga na kidato cha kwanza iliyoandaliwa kwa kiingereza, hali kadhalika ndugu zangu pia.

Na ndio maana nimesema inakupa msingi kama ilivyo kwa hisabati na masomo mengine.
Jambo la zaidi ya kujadili nafikiri ni ufanisi wa walimu wa kiingereza kwa shule za msingi huenda hapo ndipo shida inapnzia.
N.B nimepitia elimu ya msingi miaka ya 90 mwanzoni.
 
nadhani kiswahili ndio kifutwe... uswahili umezidi maofisini..

lugha ya kiofisi iwe english tu... kiswahili kiwe kama lugha nyingine angalau tutasonga mbele.
 
mimi sioni kabisa msaada wa hili somo hata likifutwa, nilimaliza shule ya msingi sijui chochote kuhusu kiingereza

Mkuu kuna msemo mmoja ambao ni mithali ya Wachina wanasema:

"Asiyejua asimshauri yule anayejua au anayejaribu kufanya".
 
kujua visentensi viwili vitatu ndio fahari yako? lugha unapofundishwa unapaswa kujua kuiandika, kuisoma, na kuizungumza kwa mawasiliano, wewe uliambulia lipi kati ya hayo kama si utoto wa fikra unakusumbua?

Kama niliweza hata hivyo visentensi vichache, shida iko wapi? Kwani kiswahli ulikuwa unapata mia? Mimi ni mkatoliki, sala zote ya kikatoliki niliweza kwa kiswahili nikiwa primary. Nilikuwa nahudhuria ibada za kiingereza hapa Nairobi na Arusha. Ni juhudi binafsi zitakusaidia. Halafu wewe huwezi kuwa mwalimu, kama utamdharau mwanafunzi wako na kumwambia vijisentensi. Kuomba maji kwa kiingereza ukiwa primary ni mtihani tosha. Hebu pitia mada yako na uweze kuitathmini kama mchangiaji alivyotaka iwe kwa mfumo mwingine.
 
When giving a post to be discussed you must be ready to accept whatever the challenge encoutered. Some would be harsh when others polite.
 
Mtoa mada english ya primary acha iendelee kuwepo,.tena ikibidi masomo yote yafundishwe kwa english...liwepo na somo la kiswahili...huo ndo ukombozi wa mtakuja primary school.
Nasema hivyo kwa sababu kwa nchi kama yetu ambayo haijakua kiuchumi tunahitaji sana english ili iwe rahisi kujifunza mambo mengi kutoka kwa wenzetu walioendelea.
 
Mimi nimesoma shule za kayumba lakini darasa la 4 niliweza kusoma na kuandika kiingereza vizuri kwa level ya std 4. Kufikia std 5 nilikuwa nimemaliza brighter grammar book 1 up to 8. By the way hivi vitabu uliwahi kuviona? Kama hujawahi kavitafute.
 
Mkumbuke hata Diamond,Arusha school na Olympio ni za Serikali a.k.a Kayumba ila ni english medium wengine msijishaue mmejulia english darasa la tatu kumbe mlisoma hizo shule, maana wengine pamoja na juhudi zetu ila kumbukumbu zangu zinaonyesha kwanza english kwa kayumba ilikuwa inaanza kufundishwa ukifika std 3 hadi la 7, darasa la 1&2 ilikuwa mwendo wa Hesabu na Hati tu kuanzia mwaka 1998 mtaala ukabadilishwa english ikaanza kufundishwa kuanzia std 1 na kuongeza masomo mengine kama standadi za kazi n.k
 
Watu wanapata walau msingi wa hiyo lugha mkuu. Kwa swali lako kwa miss chagga ni sawa na kutaka mtoto wa darasa la saba aweze kufanya integration kisa kasoma hesabu.
mantiki ya mfano wa INTERGRATION ni ishara kuwa hukusoma vizuri, niliandika KIINGEREZA RAHISI nikimaanisha kwa level ya primary. INTERGRATION ni ngumu kuliko hata proffesional english na wewe umeona KIINGEREZA RAHISI=INTERGRATION
 
Last edited by a moderator:
Sijiu nafasi yako lakini mimi binafsi nilisoma primary za serikali na kwa kiingereza hicho hicho cha primary niliweza kuomba maji na kufanya mitihani ya kujiunga na kidato cha kwanza iliyoandaliwa kwa kiingereza, hali kadhalika ndugu zangu pia. Na ndio maana nimesema inakupa msingi kama ilivyo kwa hisabati na masomo mengine. Jambo la zaidi ya kujadili nafikiri ni ufanisi wa walimu wa kiingereza kwa shule za msingi huenda hapo ndipo shida inapnzia. N.B nimepitia elimu ya msingi miaka ya 90 mwanzoni.
tindikali, swali what is acid? hesabu AB ni sambamba na CD,tafuta thamani ya X? Ukaletewa if AB is parallel to CD find X. Eti ukaelewa na kujibu kwa kimombo, uongo mwingine.
 
Back
Top Bottom