Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #21
19.
Muda mfupi baadaye.
“Ni kweli hujui… Hujui kama unabaka. Na unambaka afisa
wa ngazi ya juu wa Jeshi la Polisi…” Kicheko.
“Sikujua… nilidhani mimi pia nimebakwa.” Kicheko.
“Ni wazi kuwa hujaipitia vizuri sheria ya ubakaji. Mwanaume habakwi, anabaka. Unaijua adhabu yake?”
“Sijui.”
“Miaka ishirini na minane jela. Lakini kwako wewe adhabu hiyo haitoshi. Utafungwa kifungo cha maisha, pingu mkononi.”
Kicheko.
“Naanza lini kuitumikia adhabu hiyo?”
“Toka sasa uko chini ya ulinzi. Huruhusiwi kukutana na mwanamke mwingine. Huruhusiwi kuoa wala kuolewa…”
Kicheko. Usingizi…
Kwa mujibu wa kumbukumbu iliyomjia Joram hayo yalikuwa maongezi yake ya mwisho na Mona Lisa kabla hajaamka na kujikuta akiwa amekumbatia maiti yake, tundu kubwa la risasi kifuani pake likiendelea kuvuja damu.
Huo ulikuwa usiku wa Jumamosi au alfajiri ya Jumapili. Kilichomshangaza ni hii hadithi mpya ya kuwa leo ni Jumatatu. Ukweli ni upi, Jumapili au Jumatatu?
Joram hakuona kama alikuwa na haja ya kuupoteza muda wake kufikiria kama leo ilikuwa Jumapili au Jumatatu. Kama daktari ameandika tarehe ya Jumatatu na kama hata gazeti lilikuwa la Jumatatu, kwa vyovyote siku ya leo ni Jumatatu. Alichohitaji kufanya ilikuwa ni kukusanya akili yake ili imwambie kitu gani kilimtokea hata akalala kwa saa ishirini na nne bila kujua kinachoendelea.
Ilikuwaje? Alijiuliza.
Taratibu, ule utandu uliokuwa ukiudumaza ubongo wake ukaanza kumtoka na picha mpya kuingia akilini. Ilikuwa kama mkanda wa video ambao unarudishwa nyuma na kuchezeshwa upya.
Sasa alikumbuka vizuri kabisa kuwa mara baada ya Mona kumwambia, “Huruhusiwi kuoa wala kuolewa…” na usingizi kuwachukua, Mona Lisa alitoweka.
Joram alibaini kutoweka huko pale alipoamka na kushituka mida fulani baina ya saa tatu au nne na kujikuta peke yake. Ubavuni mwake, pale alipolala Mona Lisa, sasa palikuwa na mto ambao yeye, Joram, aliukumbatia. Hakujali, akijua kuwa msichana huyo alikuwa ameondoka kimyakimya kwa kuchelea kumsumbua. Akaurudia usingizi wake ambao aliuchapa hadi saa saba za mchana huo. Baada ya kuoga, kunywa supu na chupa mbili za club soda alirejea chumbani kwake ambako alijilaza chali na kuendelea na mswada wa Mona, UBONGO WA MWALIMU NYERERE.
Ilikuwa riwaya tamu. Ilimvutia na kumsisimua kiasi kwamba alijikuta amezama moja kwa moja katika msitu huo wa maneno yaliyopangiliwa kisanii. Ilimwia vigumu zaidi kuamini kuwa mbunifu mwenyewe alikuwa msichana mpole na mrembo kama yule. Ufundi wa matumizi ya lugha, hila katika mpangilio wa matukio na zaidi ya yote uhalisia wa matukio ya mambo katika hadithi hiyo ni miongoni mwa mambo yaliyomfanya Joram amezwe moja kwa moja, bila kujua kuwa muda umekwenda, hadi aliposikia mlango wake ukigongwa.
Muda mfupi baadaye.
“Ni kweli hujui… Hujui kama unabaka. Na unambaka afisa
wa ngazi ya juu wa Jeshi la Polisi…” Kicheko.
“Sikujua… nilidhani mimi pia nimebakwa.” Kicheko.
“Ni wazi kuwa hujaipitia vizuri sheria ya ubakaji. Mwanaume habakwi, anabaka. Unaijua adhabu yake?”
“Sijui.”
“Miaka ishirini na minane jela. Lakini kwako wewe adhabu hiyo haitoshi. Utafungwa kifungo cha maisha, pingu mkononi.”
Kicheko.
“Naanza lini kuitumikia adhabu hiyo?”
“Toka sasa uko chini ya ulinzi. Huruhusiwi kukutana na mwanamke mwingine. Huruhusiwi kuoa wala kuolewa…”
Kicheko. Usingizi…
Kwa mujibu wa kumbukumbu iliyomjia Joram hayo yalikuwa maongezi yake ya mwisho na Mona Lisa kabla hajaamka na kujikuta akiwa amekumbatia maiti yake, tundu kubwa la risasi kifuani pake likiendelea kuvuja damu.
Huo ulikuwa usiku wa Jumamosi au alfajiri ya Jumapili. Kilichomshangaza ni hii hadithi mpya ya kuwa leo ni Jumatatu. Ukweli ni upi, Jumapili au Jumatatu?
Joram hakuona kama alikuwa na haja ya kuupoteza muda wake kufikiria kama leo ilikuwa Jumapili au Jumatatu. Kama daktari ameandika tarehe ya Jumatatu na kama hata gazeti lilikuwa la Jumatatu, kwa vyovyote siku ya leo ni Jumatatu. Alichohitaji kufanya ilikuwa ni kukusanya akili yake ili imwambie kitu gani kilimtokea hata akalala kwa saa ishirini na nne bila kujua kinachoendelea.
Ilikuwaje? Alijiuliza.
Taratibu, ule utandu uliokuwa ukiudumaza ubongo wake ukaanza kumtoka na picha mpya kuingia akilini. Ilikuwa kama mkanda wa video ambao unarudishwa nyuma na kuchezeshwa upya.
Sasa alikumbuka vizuri kabisa kuwa mara baada ya Mona kumwambia, “Huruhusiwi kuoa wala kuolewa…” na usingizi kuwachukua, Mona Lisa alitoweka.
Joram alibaini kutoweka huko pale alipoamka na kushituka mida fulani baina ya saa tatu au nne na kujikuta peke yake. Ubavuni mwake, pale alipolala Mona Lisa, sasa palikuwa na mto ambao yeye, Joram, aliukumbatia. Hakujali, akijua kuwa msichana huyo alikuwa ameondoka kimyakimya kwa kuchelea kumsumbua. Akaurudia usingizi wake ambao aliuchapa hadi saa saba za mchana huo. Baada ya kuoga, kunywa supu na chupa mbili za club soda alirejea chumbani kwake ambako alijilaza chali na kuendelea na mswada wa Mona, UBONGO WA MWALIMU NYERERE.
Ilikuwa riwaya tamu. Ilimvutia na kumsisimua kiasi kwamba alijikuta amezama moja kwa moja katika msitu huo wa maneno yaliyopangiliwa kisanii. Ilimwia vigumu zaidi kuamini kuwa mbunifu mwenyewe alikuwa msichana mpole na mrembo kama yule. Ufundi wa matumizi ya lugha, hila katika mpangilio wa matukio na zaidi ya yote uhalisia wa matukio ya mambo katika hadithi hiyo ni miongoni mwa mambo yaliyomfanya Joram amezwe moja kwa moja, bila kujua kuwa muda umekwenda, hadi aliposikia mlango wake ukigongwa.