Mtanda fuatilia kwa karibu mradi wa jengo la uwanja wa ndege la kimataifa Mwanza, limesimama tena

Mtanda fuatilia kwa karibu mradi wa jengo la uwanja wa ndege la kimataifa Mwanza, limesimama tena

Sawa ila lazima uangalie ukaribu na vivutio hivyo na vipo vingi sehemu gani. Huwezi kujenga tourist hub Kigoma ambapo vivutio vya utalii ni vichache ukaacha kujenga hub hiyo mahali kama Arusha ambapo vivitio hivyo vimelundikana. Mwanza ukiacha Ziwa Victoria kuna national parks ngapi ukilinganishwa na ukanda wa Kaskazini? Kilimanjaro national park, Mkomazi np, Arusha np, Tarangire np, Manyara np, Ngorongoro np, na nyingine nyingi. Kwanini kuanza kuvunja nguvu hii kwa kuanzisha circuits nyingine pengine zitazoongeza gharama tu kwa serikali na watalii?
Kumbe ni lijitu la kaskazini? Ndio maana.
 
International Airport hazijengwi kwa sababu ya Tourism peke yake. Kuna mambo mengi muhimu, pengine muhimu zaidi ya hilo swala moja tu la utalii.
Hili la utalii ndilo wewe limekupofusha akili kabisa?

Dar es Salaam ilivyo sasa, ungetamani isiwe na international airport kwa vile haipo kwenye eneo la vivutio vya utalii?
Huyo jamaa anaamini miundombinu ipo kwa ajili ya kurahisisha shughuli za kitalii tu basi.... akili zake ni duni sana, sijui kasomea wapi.

Mtu anashindwa kuelewa ukiongelea habari ya maziwa makuu na shughuli zinazofanyika pembezoni kwa percentage kubwa zinafanyika Mwanza... biashara ya samaki,mabondo,dagaa na hata mifugo kwa kiasi kikubwa logistics huwa inafanyikia mwanza... na wanaoifanya ni watu kutoka mataifa tofauti tofauti.

Ila yeye amekariri, international airport ni kwa ajili ya utalii tu ni akili hizo? Au ngoja tumuulize pale Entebbe Uganda kuna international airport je kuna shughuli gani za kitalii zinazoendelea pale?
 
Huyo jamaa anaamini miundombinu ipo kwa ajili ya kurahisisha shughuli za kitalii tu basi.... akili zake ni duni sana, sijui kasomea wapi.

Mtu anashindwa kuelewa ukiongelea habari ya maziwa makuu na shughuli zinazofanyika pembezoni kwa percentage kubwa zinafanyika Mwanza... biashara ya samaki,mabondo,dagaa na hata mifugo kwa kiasi kikubwa logistics huwa inafanyikia mwanza... na wanaoifanya ni watu kutoka mataifa tofauti tofauti.

Ila yeye amekariri, international airport ni kwa ajili ya utalii tu ni akili hizo? Au ngoja tumuulize pale Entebbe Uganda kuna international airport je kuna shughuli gani za kitalii zinazoendelea pale?
Ilipokaa Mwanza ni sehemu ya kimkakati sana katika eneo zima la Afrika Mashariki. Ni bahati nzuri tu, kwamba Arusha iliwahi kuwa Makao ya Jumuia ya Afrika Mashariki, lakini kiuhalisia, eneo sahihi lilipashwa kuwa Mwanza.

Hata hivyo, Mwanza haizuiwi na jambo lolote, umuhimu wake unajitokeza tu kwa sababu ya umuhimu wa eneo ilipo. Itaendelea kukua na kupanuka zaidi na zaidi.

Ni sawa na kama majiji ya sehemu zingine duniani. New York inaweza kuwa mashuhuri, lakini umashuhuri huo hauzuii majiji kama Los Angeles kuwa majiji muhimu ndani ya nchi hiyo.

Huo uwanja wa ndege wa Mwanza, itafikia mahala italazimu ujengwe mwingine kwa ufinyu wake ulivyo hautaweza kuhimiri shughuli za usafiri miaka ishirini tu toka sasa.
 
Wakipitia Arusha ndio kila kitu kwanza wanaanza na:
My Kilimanjaro, then
Arusha national park
Tarangire
Manyara
Ngorongoro halafu ndio
Serengeti
Arusha pamekaa kistratejia zaidi
Una mawazo mazuri, lakini mawazo yake ni mgando!
Tuko kwenye zama za ku-diversify, zama za kuweka mayai yote kwenye kapu moja zimeshapita
 
AHaa. Kumbe unasukumwa na maslahi na siyo sababu za sifa za kuwa na uwanja wa kimataifa wa ndege?
Ni mtalii gani anakuja Tanzania na lengo la kutembelea maeneo hayo pekee uliyoyataja wewe? Unataka vivutio viwe sehemu moja tu ya nchi; kwa nini?
Inajulikana toka zamani, maslahi ya watu wenye mawazo kama yako ndio miaka yote wamekuwa wakiukwamisha huu uwanja wa Mwanza usipewe hadhi inayoistahili. Huu ni ubinafsi usiohitajika ndani ya nchi hii. Maendeleo ya nchi ni kwa watu wote, siyo eneo fulani pekee.
Tunahitaji ku diversified tourist products kusini,magharibi,kanda ya ziwa,na mashariki kanda ya kaskazini imekuwa saturated mno. Mwanza international airport is a solution,Said Mtanda kwa hili usifanye siasa au longolongo as a strong RC. NI issue kwa mza
 
Huyo jamaa anaamini miundombinu ipo kwa ajili ya kurahisisha shughuli za kitalii tu basi.... akili zake ni duni sana, sijui kasomea wapi.

Mtu anashindwa kuelewa ukiongelea habari ya maziwa makuu na shughuli zinazofanyika pembezoni kwa percentage kubwa zinafanyika Mwanza... biashara ya samaki,mabondo,dagaa na hata mifugo kwa kiasi kikubwa logistics huwa inafanyikia mwanza... na wanaoifanya ni watu kutoka mataifa tofauti tofauti.

Ila yeye amekariri, international airport ni kwa ajili ya utalii tu ni akili hizo? Au ngoja tumuulize pale Entebbe Uganda kuna international airport je kuna shughuli gani za kitalii zinazoendelea pale?
Sasa hapo Mwanza international international airport ya nini? Walikimbilia kujenga Songwe international airport zaidi ya miaka 10 iliyopita lakini umewahi kusikia ikifanya international flights? Hakuna sababu ya maana ya kuwa na international airport Mwanza.
 
International Airport hazijengwi kwa sababu ya Tourism peke yake. Kuna mambo mengi muhimu, pengine muhimu zaidi ya hilo swala moja tu la utalii.
Hili la utalii ndilo wewe limekupofusha akili kabisa?

Dar es Salaam ilivyo sasa, ungetamani isiwe na international airport kwa vile haipo kwenye eneo la vivutio vya utalii?
Mwanza haina abiria wengi wanaoweza kusababisha kujengwa international airport. Hakuna shughuli za kimataifa kama Arusha, Dar, Dodoma. Mnataka international airport ya nini?
 
Utalii sio kuangalia wanyama pekee lazima tubadilike tuendane na wakati leo hii Dubai wanatengeneza mbuga zao zenye wanyama kama ambao wapo kwetu na ukweli ni kwamba wametoka kwetu kwahiyo itafika muda watalii wengi wataishia Dubai badała ya kują nchini kwetu kutolana na mikakati wenzetu waliyojiwekea huko mbeleni. Utalii upo wa aina nyingi ingawa sisi tumekomaa na wanyama tu miaka nenda rudi wakati mila na tamaduni za baadhi ya jamii zetu ni utalii tosha pia fukwe na majengo ya kale, miamba na mapango, vyakula nk. Mpaka hapo hujaona umuhimu wa kuwa na uwanja wa ndege Wenye hadhi ya kimataifa kwa ukanda ule?
Mwanza bado kabisa hata huo uwanja mdogo tu abiria ni wachache international airport ya nini?
 
Mwanza haina abiria wengi wanaoweza kusababisha kujengwa international airport. Hakuna shughuli za kimataifa kama Arusha, Dar, Dodoma. Mnataka international airport ya nini?
Kwa maoni yako haya ni kwamba Mwanza hata kama haina vitu hivyo leo, itakuwa hainavyo miaka yote?

Angalia uwingi wa watu. Hao unaowaona leo hawawezi kupanda ndege, ni hao hao miaka kumi ijayo watakuwa wanapigana vibega kutumia usafiri huo.
Palipo na uwingi wa watu, shughuli zote hizo ulizotaja wewe ni lazima ziwepo

Kwanza kimandhari tu, huwezi kulinganisha Arusha kwa njia yoyote na Mwanza.

Pengine kwa vile huna 'exposure' na miji mingi duniani, ndiyo maana unashindwa kujuwa maana ya uwanja wa kimataifa ni nini.
Chukulia uwanja wa Kimataifa wa Hartfield-Jackson, kwa mfano uliopo Atlanta Georgia; uwanja ambao ni wa pili (nadhani) duniani kwa wingi wa wasafiri kwa ndege duniani. Hapo Atlanta hakuna vivutio vya utalii unavyodai wewe; lakini mahali ulipo uwanja huo ni sehemu muhimu inayounganisha wasafiri toka maeneo mbalimbali duniani.

Kwa mahali ilipo Mwanza katika bara la Afrika, hata hiyo Hartfield-Jackson haiwezi kuwa na 'potential' iliyonayo Mwanza.
Kwani shughuli za Kimataifa ni nini? Si ni kuwa na kumbi tu za kutosha na hotel nzuri? Unategemea hayo yote yawepo hata bila kuwepo kwa uwanja kwanza?
Kigali kuna nini, mbona mikutano ya kimataifa mingi tu inafanyika huko?
Ni hivi, unayo hofu kubwa sana juu ya 'potential' iliyo nayo Mwanza, kiasi kwamba hofu yako inakupofusha na kudhani kukua kwa Mwanza kutaiua Arusha. Na bila shaka, hata huko kwenye wafanya maamuzi serikalini hofu hii ndiyo inayofanya pawepo na mizengwe mingi juu ya mji huu wa Mwanza. Mizengwe hii haiwezi kuizuia Mwanza kuchukua hadhi yake katika majiji bora kabisa duniani.
 
Mwanza haina abiria wengi wanaoweza kusababisha kujengwa international airport. Hakuna shughuli za kimataifa kama Arusha, Dar, Dodoma. Mnataka international airport ya nini?
Wanahitsjika wangapi?
 
Wananchi wa Mwanza tumekuwa tukifuatilia kwa karibu ujenzi wa jengo la abiria la uwanja wa ndege la Mwanza linalotarajiwa kuufanya uwanja huu kuwa wa kimataifa.

Aliyekuwa RC wa Mwanza Makalla alijitahidi sana kuurejesha kwenye uhai lakini kampuni ya Mzawa haionekani kufanya chochote hadi sasa site kulikoni? kimya kabisa.

Aidha, kuna ahadi ya kujenga njia 4 barabara za Kenyata na Nyerere kuingia/kutoka jijini ahadi ya muda mrefu tunataka kuona vitendo na matokeo, wizara ya uchukuzi na pia ujenzi si jui wanatuonaje kanda hii.

Tunaangalia utakavyoisaidia Mwanza na Kanda ya Ziwa kukamilisha miradi. Tunakutakia kazi njema na uongozi uliotukuka kwenye mkoa huu ili uache alama
Arudishwe jeshini kashindwa kazi, watuletee wamkaya makonda
 
Wananchi wa Mwanza tumekuwa tukifuatilia kwa karibu ujenzi wa jengo la abiria la uwanja wa ndege la Mwanza linalotarajiwa kuufanya uwanja huu kuwa wa kimataifa.

Aliyekuwa RC wa Mwanza Makalla alijitahidi sana kuurejesha kwenye uhai lakini kampuni ya Mzawa haionekani kufanya chochote hadi sasa site kulikoni? kimya kabisa.

Aidha, kuna ahadi ya kujenga njia 4 barabara za Kenyata na Nyerere kuingia/kutoka jijini ahadi ya muda mrefu tunataka kuona vitendo na matokeo, wizara ya uchukuzi na pia ujenzi si jui wanatuonaje kanda hii.

Tunaangalia utakavyoisaidia Mwanza na Kanda ya Ziwa kukamilisha miradi. Tunakutakia kazi njema na uongozi uliotukuka kwenye mkoa huu ili uache alama
Hizo ni dili za Mbarawa na Abdul
 
Lile wazo la Magu Kutengeneza mbuga nyingine tofauti na tulizozizoea lilikuwa sahihi sana sema wabongo tunachukua muda mrefu kuelewa vitu tunaishia kwenye kuponda bila kuwaza kwa usahihi na kufikiria kwa mapana zaidi. Fikiria Waarabu wameona wachukue wanyama huku kwetu wakatengeneze mbuga sisi tupo tu na zile zile za kale hata hatuwazi vizuri kuongeza vivutio zaidi vya utalii.
Sisi tunaongozwa na watu wapuuzi ndiyo maana hatuwazi nje ya box
 
International Airport hazijengwi kwa sababu ya Tourism peke yake. Kuna mambo mengi muhimu, pengine muhimu zaidi ya hilo swala moja tu la utalii.
Hili la utalii ndilo wewe limekupofusha akili kabisa?

Dar es Salaam ilivyo sasa, ungetamani isiwe na international airport kwa vile haipo kwenye eneo la vivutio vya utalii?
Dar, Mwanza, Mbeya, Arusha na Dom zinatakiwa kuwa na International Airport maana kuna wageni wengi wanaingia na kutoka, tena ikiwezekana hata Kahama nayo sababu za kiuchumi
 
Mwanza bado kabisa hata huo uwanja mdogo tu abiria ni wachache international airport ya nini?
Tatizo unaonekana umejichimbia hapo kwenu tu ungalimited ukishinda unavuta bangi, na huna exposure yoyote wala hiyo mwanza yenyewe huijui zaidi ya kuisoma tu mitandaoni kutoka kwa haters wenzio wanaoichukia mwanza...!!

Umewahi kwenda pale Ilemela Airport ukaona jinsi abiria walivyojazana wakisubiri ndege? Je unatambua kwanza baada ya JNIA the busiest airport inayifuata kwa hapa bongo ni mwanza airport, na pia ni rahisi sana leo hii ukienda pale JNIA kupata flight ticket ya kwenda Arusha/kilimanjaro leo kuliko kupta ya kwenda Mwanza kwa safari ya leo leo.

Majitu yenye fikra za kibaguzi na chuki kama wewe ndio mmekwa ni kikwazo kikubwa sana cha maendeleo ya sehemu zingine, huwa mnataka mambo yote ya maana yafanyike kaskazini tu... ovyo sana wewe
 
Acha bangi basi, nenda Air Tanzania au TAA uwaulize. Mwanza ni ya 2 kwa domestic flights baada ya JNIA! Air Tanzania pekee wana route 5 per day kutoka na kwenda viwanja tofauti nchi hii.
Huyo jamaa inaonekana wazi anasumbuliwa na chuki za kikanda,ujinga, kutokujiamini na na bangi zilzomuathiri mshipa ya ubongo... ndio maana ana bwabwaja tu bila kujua anachokiandika ni nini.

Mtu anakwambia mkoa ambao ndio ni wa pili kwa income generation haustahili kuwa na international airport kisa tu hakuna mnyumbu wala swala kama wale waliopo ngoro ngoro, sasa huyo ni mtu mwenye akii kweli?
 
Tatizo unaonekana umejichimbia hapo kwenu tu ungalimited ukishinda unavuta bangi, na huna exposure yoyote wala hiyo mwanza yenyewe huijui zaidi ya kuisoma tu mitandaoni kutoka kwa haters wenzio wanaoichukia mwanza...!!

Umewahi kwenda pale Ilemela Airport ukaona jinsi abiria walivyojazana wakisubiri ndege? Je unatambua kwanza baada ya JNIA the busiest airport inayifuata kwa hapa bongo ni mwanza airport, na pia ni rahisi sana leo hii ukienda pale JNIA kupata flight ticket ya kwenda Arusha/kilimanjaro leo kuliko kupta ya kwenda Mwanza kwa safari ya leo leo.

Majitu yenye fikra za kibaguzi na chuki kama wewe ndio mmekwa ni kikwazo kikubwa sana cha maendeleo ya sehemu zingine, huwa mnataka mambo yote ya maana yafanyike kaskazini tu... ovyo sana wewe
Mimi naipenda Mwanza sana na nashangaa kwanini serikali haiendelezi mji mzuri na mkubwa kama Mwanza. Mwanza ilipaswa kuwa jiji kubwa na zuri kweli kweli. Ilipaswa barabara ya njia nane kilometer 30 kabla ya kufika katikati ya mji, treni nzuri, kiwanja kikubwa cha mpira kama cha Dar, n.k.

Ila Mwanza kwa international airport bado.

Unakosea kuhusu viwanja bize vya ndege nchini, ipo hivi:
1. Dar (JNIA)
2. Zanzibar (ZNZ)
3. Kilimanjaro (JRO)
4. Arusha (ARK)
5. Dodoma (DOD)
6. Mwanza (MWZ)

Sote tunajua jinsi uwanja wa ndege Chato (HTGE) unavyotumika na wenyeji kuanikia mpunga. Sasa hapo Mwanza mnataka uwanja wa kimataifa wa ndege kwa kuanikia sangara? Kazi za viwanja vya kimataifa sio hiyo!
 
Acha bangi basi, nenda Air Tanzania au TAA uwaulize. Mwanza ni ya 2 kwa domestic flights baada ya JNIA! Air Tanzania pekee wana route 5 per day kutoka na kwenda viwanja tofauti nchi hii.
Mimi naipenda Mwanza sana na nashangaa kwanini serikali haiendelezi mji mzuri na mkubwa kama Mwanza. Mwanza ilipaswa kuwa jiji kubwa na zuri kweli kweli. Ilipaswa barabara ya njia nane kilometer 30 kabla ya kufika katikati ya mji, treni nzuri, kiwanja kikubwa cha mpira kama cha Dar, n.k.

Ila Mwanza kwa international airport bado.

Unakosea kuhusu viwanja bize vya ndege nchini, ipo hivi:
1. Dar (JNIA)
2. Zanzibar (ZNZ)
3. Kilimanjaro (JRO)
4. Arusha (ARK)
5. Dodoma (DOD)
6. Mwanza (MWZ)

Sote tunajua jinsi uwanja wa ndege Chato (HTGE) unavyotumika na wenyeji kuanikia mpunga. Sasa hapo Mwanza mnataka uwanja wa kimataifa wa ndege kwa kuanikia sangara? Kazi za viwanja vya kimataifa sio hiyo!
 
Dar, Mwanza, Mbeya, Arusha na Dom zinatakiwa kuwa na International Airport maana kuna wageni wengi wanaingia na kutoka, tena ikiwezekana hata Kahama nayo sababu za kiuchumi
Hata Kenya ambapo wapo wazungu wengi sana wanaishi na kumiliki mashamba na biashara kubwa na wakenya wengi sana husafiri kwenda kokote duniani, kiwanja cha kimaifa kwa maana halisi ni Jomo Kenyatta International Aiport, hata Mombasa International Airport in feed JKIA tu hairushi ndege moja kwa moja Dubai au Amsterdam. Sasa international airport Mwanza si itakuwa hasara tupu?
 
Back
Top Bottom