Mtanda fuatilia kwa karibu mradi wa jengo la uwanja wa ndege la kimataifa Mwanza, limesimama tena

Hivi kumbe wewe ni chizi tu mmoja hapa! Sitapoteza muda zaidi ya niliokwisha poteza.
 
Ninakuja ku-invest Mwanza na ninashangaa kwanini mji huu wenye watu wengi lakini kuna mambo ya hovyo sana. Najua uwanja wa ndege sio kwa watalii tu ila hata wafanyabiashara na wasafiri wa ndani pia. Ila uwanja wa ndege wa kimataifa lazima pawepo na wasafiri wengi kati ya mji huo na miji mingine nje ya nchi. Sasa kwa Mwanza mbona hakuna hayo? Hata kama kuna watu wa Mwanza wanakwenda nje, si wanapitia K"Njaro, Dar, Zanzibar au hata Dodoma itakapokamilika? Au unafikiri kila jiji au mji mkubwa lazima uwe na kiwanja cha kimataifa. Kuna majiji makubwa duniani kama Yokohama, Kyoto (Japan), Denver Colorado, Oklahoma (USA), nk haina viwanja vya kimataifa. Viwanja vya kimataifa sio kwa kila mji mkubwa, ni kwa strategic places kama Zanzibar, Kilimanjaro/Arusha, Dar na Dodoma. Tunaweza kuwa na international airport Kasulu tusiwe nayo Mwanza.

Kumbuka hata Kenya pamoja na kuwa na Jomo Kenyatta, Mombasa na Kisumu lakini international flights zinafanyika Jomo Kenyatta. Africa Kusini vipo viwanja vya maana Durban, Cape Town, nk lakini internatinal flights zinafanyika kwa zaidi ya 90% Johannesburg. Uwe na akili ya kuona hivyo na uache kulilia mambo usiyoyajua vizuri kwanini yapo hivyo.
 
Wewe nimekwisha malizana nawe, kwa sababu ni chizi mmoja tu asiyejuwa kitu.
Yote uliyo andika hapa umekwisha fahamishwa juu yake, lakini huna akili za kuelewa kwa sababu ya uchizi unaokusumbua wewe.
Mwanza utaiona ikishamiri, na hakuna lolote utakaloweza kufanya kuizuia.
 
Bro haipendezi kuwasemea watu tulioko huku tunauona huo uhitaji na hata serikali inauona huo uhitaji sasa kivip wewe useme abilia hawapo unataka shughuli zipi zi determine uhitaji wa International Airport tumekwambia uwanja haujaanza lakini tayali international flight zaidi ya kumi zimeshaomba Route, sasa wewe na makampuni ya ndege ni nani kafanya research ya uwepo wa abilia, au wasiwasi wako ikianza huenda viwanja vingine vikakosa abilia maana ni kama unawasiwasi ila kila mahali kuna potential yake abilia watakuwepo Kote.
 
Mimi binafsi ninajamaa zangu wawili wanafanya kazi South na familia zao zipo huku, wapo walioko Saudi, Mauritius, USA nk na wanalalamika sana kuhusu kukoseka kwa International Airport wewe unapinga kivipi, Majuzi hapa Mh Rais Mama Samia alikili haipendezi minofu ya Samaki kutoka Mwanza kwenda kuondokea Nairobi hivyo International Airport ijengwe au haufatilii?
 
Mwanza nakuja kuwekeza na tayari wenzangu wengi wapo kazini hapo ni pazuri kwa sangara na vitu vingine vichache ila kwa sasa hapajawa na ulazima wa international airport, tafadhali elewa hilo. Muache kulazimisha mambo kama Magufuli alivyolazimisha Chato na sasa kila kitu kimekufa.
 
Hata viwanja vilivyopo ikiwa ni pamoja na Dar havina abiria kwa kiasi kinachotakiwa kwa international airport zetu, sasa mnalazimisha Mwanza ni hasara, Kuna Songwe international airport wamejenga huko porini hakuna ndege ya kimataifa imewahi kutua pale. Chato airport wanaanikia mpunga pale, hivi mnafikiri aiports ni kwa mambo ya mchezo mchezo? Mwanza airport sawa, lakini Mwanza International Airport hapana kwa sasa1
 
Basi acha ijengwe tuone ni wapi pamelazimishwa unachohofia wewe ni kuhisi utatoa upinzani mkali badala ya kukiona kama ni moja ya viwanja vitakavyongeza fursa na uwekezaji ukanda wa ziwa sanjali na kusogeza huduma huku tofauti na hali ilivyosasa tunaingia extra cost za kuunga ndege wakati inawezekana kuja na direct flight
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…