Mtandao wa Vodacom wajitafakari

Mtandao wa Vodacom wajitafakari

Ukiwa na Akili timamu huwezi kuutumia huu / huo Mtandao badala yake utautumia Mtandao mzuri, wenye uhakika 100% na ambao Watu wengi wenye Akili Kubwa na Ushawishi Uliotukuka tunautumia huko Tanzania na hata hapa nchini Uganda nilipo wa Airtel.

Nikiona Mtu yoyote hatumii Mtandao wa Airtel huwa namdharau mno na wala huwa sitaki pia kupoteza muda wangu Kuzungumza nae kwakuwa najua hata Vichwani mwao pia huwa ni Watupu. Na pia Mtandao wa Airtel ni Mtandao ambao ukiutumia tu haaka sana kama ulikuwa Masikini basi Maisha yanabadilika na unakuwa Tajiri.

Imeisha hiyo.....!!
😂😂😂😂.... Loh mkurugenzi... Tafadhali,... Siyo kwa promo hii uliyowapa Airtel.... Ingawa wao naonaga katika intaneti Kasi Yao Huwa hairidhishi kabisa
 
Kutwa kuomba radhi kwa tatizo linalojirudia rudia

Mpendwa Mteja, Tunaomba radhi kwa changamoto uliyoipata ya miamala ya M-Pesa kwenda mitandao mingine na benki. Kwa sasa huduma zimerejea kikamilifu. Miamala ambayo haijakamilika, itakamilishwa au kurudishwa haraka iwezekanavyo. Tunakushukuru kwa uvumilivu wako.
Kila wakati wanarejea kuomba radhi.... Baada ya wiki unashangaa tena wamenasa....

Alafu ni mtandao ambao ninauamini kwelikweli.... Nadhani kuliko mitandao yote....
 
Ukiwa na Akili timamu huwezi kuutumia huu / huo Mtandao badala yake utautumia Mtandao mzuri, wenye uhakika 100% na ambao Watu wengi wenye Akili Kubwa na Ushawishi Uliotukuka tunautumia huko Tanzania na hata hapa nchini Uganda nilipo wa Airtel.

Nikiona Mtu yoyote hatumii Mtandao wa Airtel huwa namdharau mno na wala huwa sitaki pia kupoteza muda wangu Kuzungumza nae kwakuwa najua hata Vichwani mwao pia huwa ni Watupu. Na pia Mtandao wa Airtel ni Mtandao ambao ukiutumia tu haaka sana kama ulikuwa Masikini basi Maisha yanabadilika na unakuwa Tajiri.

Imeisha hiyo.....!!
We jamaaa muongo sana nilishawahi kukuona kwenye group fulani la whatsapp la Simba SC una namba ya vodacom 0743 XXX XXX na unatumia jina lako hili hili la Gentamycine
 
CCM ni Moja ya shareholders wakubwa wa Vodacom
 
Pamoja na Changamoto hizi (Backdates to August), bado naamini Vodacom Tanzania ndio Mtandao Bora na Reliable zaidi hapa Tanzania, ukifuatiwa kwa mbali na Airtel.

Hizi Hard times huwa zipo tu regardless the Mtandao!
 
Kesho Nahamisha vitu vyangu nusu na kuweka Tigo,Bora nipate hasara ya kutuma kuliko fedhea niliyopata leo.
Una hela hazitoki.

Bila kuwa na mtu alieniamini ningeaibika sana.
Kuna siku nilikula msosi sehemu wakanipa lipa namba ya Mpesa nilipe, aisee kwenye Airtel yangu nimekatwa, kwenye Mpesa yao haijafika kuna tatizo.., aisee, kidogo niaibike, na sikuwa na cash kabisa.., pesa imekuja kurudi kwangu baada ya wiki…, ikabidi niende kwenye ule mgahawa kuirudisha..
 
Kwa siku za hivi karibuni mtandao wa Vodacom umekuwa ukisumbua sana Hali ambayo imepelekea usumbufu mkubwa sana kwa watumiaji wa mtandao huu.

Kumekuwa na Hali ya kukatika kwa network au kushindwa kufanya miamala ya kifedha jambo ambalo limekuwa likijirudia rudia na kuzua sintofahamu Kubwa kwa watumiaji.

Ikumbukwe kuwa mtandao huu umekuwepo nchini kwa miongo miwili Sasa na hivyo kujizolea watumiaji lukuki...

Lakini changamoto hii iliyoanza kujitokeza itasababisha watumiaji kuanza kuwakimbia...

Nitoe Rai kwa Menejimenti ya Vodacom na timu Yao ya Ufundi wajitafakari sana.

Wachukue hatua muhimu ili kuondoa changamoto hii kwa mtandao huu pendwa ambao umetumika kwa muda mrefu nchini Sasa.
SiyoVoda com pekee, hata Halo tel wameshiba pesa wanaanza kubweteka.

Huduma kwa wateja hawapokei simu, ukiuliza salio hakuna majibu yapata wiki sasa!

Ndomaana nikiamuaga kuchomoa line, ninachomoa mazima, sipendi upumbaf mie.
 
Pamoja na Changamoto hizi (Backdates to August), bado naamini Vodacom Tanzania ndio Mtandao Bora na Reliable zaidi hapa Tanzania, ukifuatiwa kwa mbali na Airtel.

Hizi Hard times huwa zipo tu regardless the Mtandao!
Unatetea uzembe wa uwajibikaji si ndiyo?

Hizi zinazoitwa 'Huduma biashara', wanatakiwa ku update mapingamizi yao yanapojitokeza kila siku, hakuna mteja atalalamika.

Hii ya kupiga kimya ni dharau, kwamba tutawafanya nini.
 
Walisema wanamaboresho mpaka November, Baada ya Nov mambo yatakuwa zaidi ya bora
 
We jamaaa muongo sana nilishawahi kukuona kwenye group fulani la whatsapp la Simba SC una namba ya vodacom 0743 XXX XXX na unatumia jina lako hili hili la Gentamycine
Kila Mtu hapa Duniani (hasa huko Mitandaoni) anapenda sana kutumia hii ID yangu ya GENTAMYCINE ila labda nikusaidie tu kuwa kuna ID moja tu ya GENTAMYCINE ambaye ni Mimi huyu hapa JamiiForums na hao sijui akina Gentamycine wengine huko Kwingineko si Mimi na wanataka tu Kusafiria Nyota yangu Kali ya Mvuto na Ushawishi.
 
Kila Mtu hapa Duniani (hasa huko Mitandaoni) anapenda sana kutumia hii ID yangu ya GENTAMYCINE ila labda nikusaidie tu kuwa kuna ID moja tu ya GENTAMYCINE ambaye ni Mimi huyu hapa JamiiForums na hao sijui akina Gentamycine wengine huko Kwingineko si Mimi na wanataka tu Kusafiria Nyota yangu Kali ya Mvuto na Ushawishi.
#NguvuMoja
#UbayaUbwela
🦁
 
Back
Top Bottom