Mtangazaji Clouds TV afukuzwa kwa kutangaza habari za Tundu Lisu

Duuuhh yamemkuta mambo, ila sijafurahia yeye asimamishwe kazi
 
Mkuu huyu Hassan alikuwa na kejeli sana dhidu ya Lissu na upinzani kwa ujumla, kama ni kweli mimi napongeza
kama ndio hivyo basi ni sawa, Muda mwingine inabidi siasa aweke pembeni abaki kwenye misingi ya utangazaji
 
Kufukuzwa kazi vs KUSIMAMISHWA KAZI...mkuu uongo sio jambo zuri
 
Ruge kafanya safi sana. Najua huyu dogo Hassan lazima atakua akioonda pasipo kuzingatia maadili. Hakuna jambo positive analoweza akaongea huyu juu ya Lissu. Huyo Mange muwe mnajaribu kuzifanyia processing taarifa zake badla ya kuzimeza kama zilivyo.
Huyo Hassan Ngoma ni kweli amesimamishwa lakini haiwezi ikawa eti ni sababu ya kuchambua afta ya Lissu bali ni sababu ya kukashifu mgonjwa. Ruge si mwehu kufikia hatua hiyo.
 
Sababu yenyewe ni hiyo NYETI.
 
Hii ni hatari aisee yaani kutangaza hali ya afya ya Tundu Lissu inamsimamisha mtu kazi?? Vipi Clouds wanatumika?

Ona anapokea tu habari hata huulizi uhalisia wake ushaaanza Clouds wanatumika. Mnajitekenya mnacheka. Mleteni Dereva tu. Lissu Ni mtanzania kwenye uzima wa Mtu hata wewe usiyetumia akili unapopokea jambo ukaangalia side B na mtoa hoja mwenyewe. Una haki ya kuishi ila acha upumbavu. We Sio Roboti.
 
Duuu kumbe Da Mange kasema basi ni marufuku kupinga .... sasa wote tuseme ni kweli kabisa Hassan kasimamishwa kazi....asitokee mtu wa kumpinga Da MANGE maana yeye ndio huongea ukweli kwa kila jambo.........
Mdogo wangu Le Mutuz,tuliza korodani hzo acha kupiga kelele mwlm (Mange) yupo darasani...,otherwise jina lako litaingia kwenye orodha ya wapiga kelele!
 
hahahaha, wanaanza kufarakana, chezea kipindi favourite cha mzee nini
 
Tusilaumu tunataka yeye mwenyewe athibitishe vi ginevyo utakuwa niuongo labda wanamambo yao mengine.
 
Ok sawa
 
Sipendeleagi sana uchambuzi wa hassan ngoma,

ila kama ni kweli sina haja ya kuendelea kusikiliza/kuangalia hiyo Tv
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…