TANZIA Mtangazaji wa Clouds FM, Ephraim Kibonde afariki dunia. Azikwa makaburi ya Kinondoni,Dar es Salaam

Sijui walikuwa na watoto? Balaa gani hili kwao!
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Du!,jamani[emoji26]
RIP Brother.

Sent from Nokia 7 Plus
 

Nimeanza kuamini.
 
Kila Nafsi Itaonja Mauti Na Hakuna Atakayebakia Isipokuwa Allaah ุณุจุญุงู†ู‡ ูˆุชุนุงู„ู‰
Kila Nafsi Itaonja Mauti Na Hakuna Atakayebakia Isipokuwa Allaah ุณุจุญุงู†ู‡ ูˆุชุนุงู„ู‰
Iymaan-Taqwa
Anasema Allaah ุณุจุญุงู†ู‡ ูˆุชุนุงู„ู‰:

ูƒูู„ู‘ู ู†ูŽูู’ุณู ุฐูŽุขุฆูู‚ูŽุฉู ุงู„ู’ู…ูŽูˆู’ุชู ูˆูŽุฅูู†ู‘ูŽู…ูŽุง ุชููˆูŽูู‘ูŽูˆู’ู†ูŽ ุฃูุฌููˆุฑูŽูƒูู…ู’ ูŠูŽูˆู’ู…ูŽ ุงู„ู’ู‚ููŠูŽุงู…ูŽุฉู ููŽู…ูŽู† ุฒูุญู’ุฒูุญูŽ ุนูŽู†ู ุงู„ู†ู‘ูŽุงุฑู ูˆูŽุฃูุฏู’ุฎูู„ูŽ ุงู„ู’ุฌูŽู†ู‘ูŽุฉูŽ ููŽู‚ูŽุฏู’ ููŽุงุฒูŽ ูˆูŽู…ุง ุงู„ู’ุญูŽูŠูŽุงุฉู ุงู„ุฏู‘ูู†ู’ูŠูŽุง ุฅูู„ุงู‘ูŽ ู…ูŽุชูŽุงุนู ุงู„ู’ุบูุฑููˆุฑ
((Kila nafsi itaonja mauti. Na bila ya shaka mtapewa ujira wenu kamili Siku ya Qiyaamah. Na atakayeepushwa na Moto na akatiwa Peponi basi huyo amefuzu. Na maisha ya dunia si kitu ila ni starehe ya udanganyifu)) [Al-'Imraan: 185]

Tokea kuumbwa kwa Nabii Aadam ุนู„ูŠู‡ ุงู„ุณู„ุงู… hadi leo na mpaka siku ya Qiyaamah hakuna kiumbe kitakachobakia isipokuwa Mwenyewe Mola Mtukufu kama Anavyosema:
ูƒูู„ู‘ู ุดูŽูŠู’ุกู ู‡ูŽุงู„ููƒูŒ ุฅูู„ู‘ูŽุง ูˆูŽุฌู’ู‡ูŽู‡ู
((Kila kitu kitaangamia isipokuwa Yeye)) [Al-Qaswas: 88]

Vile vile Anasema Allaah ุณุจุญุงู†ู‡ ูˆุชุนุงู„ู‰ :

((ูƒูู„ู‘ู ู…ูŽู†ู’ ุนูŽู„ูŽูŠู’ู‡ูŽุง ููŽุงู†ู))
((ูˆูŽูŠูŽุจู’ู‚ูŽู‰ ูˆูŽุฌู’ู‡ู ุฑูŽุจู‘ููƒูŽ ุฐููˆ ุงู„ู’ุฌูŽู„ูŽุงู„ู ูˆูŽุงู„ู’ุฅููƒู’ุฑูŽุงู…))

((Kila kilioko juu Yake kitatoweka))
((Na Atabakia Mwenyewe Mola wako Mwenye utukufu na ukarimu)) [Ar-Rahmaan: 26-27]

Baada ya kupulizwa Swuur (baragumu) siku ya Qiyaamah viumbe vyote vitakufa kwa mpangilio Anaoutaka Mwenyewe Allaah ุณุจุญุงู†ู‡ ูˆุชุนุงู„ู‰. Kisha mwisho atabakia Malakul Mawt (Malaika mtoaji roho) na Allaah ุณุจุญุงู†ู‡ ูˆุชุนุงู„ู‰. Kisha Allaah ุณุจุญุงู†ู‡ ูˆุชุนุงู„ู‰ Atamuamrisha Malakul Mawt ajitoe roho yake mwenyewe. Atakapokufa Malakul Mawt Atabakia Allaah ุณุจุญุงู†ู‡ ูˆุชุนุงู„ู‰ Pekee wa Mwanzo na wa Mwisho, Al-Hayyul-Qayyuum (Mwenye uhai wa maisha, Msimamia kila jambo). Allaah ุณุจุญุงู†ู‡ ูˆุชุนุงู„ู‰ Siku hiyo Atazikusanya ardhi na mbingu katika Mikono Yake,

((ูˆูŽุงู„ู’ุฃูŽุฑู’ุถู ุฌูŽู…ููŠุนู‹ุง ู‚ูŽุจู’ุถูŽุชูู‡ู ูŠูŽูˆู’ู…ูŽ ุงู„ู’ู‚ููŠูŽุงู…ูŽุฉู ูˆูŽุงู„ุณู‘ูŽู…ุงูˆูŽุงุชู ู…ูŽุทู’ูˆููŠู‘ูŽุงุชูŒ ุจููŠูŽู…ููŠู†ูู‡ู))

((Na Siku ya Qiyaamah ardhi yote itakuwa mkononi Mwake, na mbingu zitakunjwa katika mkono wake wa kuume)) [Az-Zumar: 67]

Na Hadiyth kutoka kwa Ibn 'Umar ุฑุถูŠ ุงู„ู„ู‡ ุนู†ู‡ kwamba:

((ูŠุทูˆูŠ ุงู„ุณู…ูˆุงุช ูˆุงู„ุฃุฑุถ ุจูŠุฏู‡ุŒ ุซู… ูŠู‚ูˆู„: ุฃู†ุง ุงู„ู…ู„ูƒุŒ ุฃู†ุง ุงู„ุฌุจุงุฑุŒ ุฃู†ุง ุงู„ู…ุชูƒุจุฑุŒ ุฃูŠู† ู…ู„ูˆูƒ ุงู„ุฃุฑุถุŸ ุฃูŠู† ุงู„ุฌุจุงุฑูˆู†ุŸ ุฃูŠู† ุงู„ู…ุชูƒุจุฑูˆู†ุŸ)) ู…ุณู„ู…

((Allaah Atazikunja mbingu kwa Mikono Yake, kisha Atasema, Mimi ni Mfalme, Mimi ni Al-Jabbaar (Mwenye Kushurutisha), wako wapi wafalme wa dunia? Wako wapi majabbaar (wanaolazimisha), wako wapi wanaotakabari?))[Muslim]

Hapo tena Atauliza mara tatu:
((ู„ู‘ูู…ูŽู†ู ุงู„ู’ู…ูู„ู’ูƒู ุงู„ู’ูŠูŽูˆู’ู…ูŽ))
((Ufalme ni wa nani leo?)) [Ghaafir:16]

Hakutakuwa na mtu wa kujibu, basi Atajibu Mwenyewe,
((ู„ูู„ู‘ูŽู‡ู ุงู„ู’ูˆูŽุงุญูุฏู ุงู„ู’ู‚ูŽู‡ู‘ูŽุงุฑ))

((Ni wa Allaah Mmoja Mtenda Nguvu)) [Ghaafir 16]

Na hapo tena ndipo kila mtu atakuta hesabu yake ya matendo aliyoyatenda duniani ikiwa ni mema au mabaya, hakuna atakayedhulumiwa hata chembe, kwani Allaah ุณุจุญุงู†ู‡ ูˆุชุนุงู„ู‰ Atahukumu kwa uadilifu baina ya viumbe Vyake. Kila jema Atalilipa kwa mara kumi na kila ovu atahesabiwa mja kwa ovu moja.

((ุงู„ู’ูŠูŽูˆู’ู…ูŽ ุชูุฌู’ุฒูŽู‰ ูƒูู„ู‘ู ู†ูŽูู’ุณู ุจูู…ูŽุง ูƒูŽุณูŽุจูŽุชู’ ู„ูŽุง ุธูู„ู’ู…ูŽ ุงู„ู’ูŠูŽูˆู’ู…ูŽ ุฅูู†ู‘ูŽ ุงู„ู„ู‘ูŽู‡ูŽ ุณูŽุฑููŠุนู ุงู„ู’ุญูุณูŽุงุจู))

((Leo kila nafsi italipwa kwa iliyochuma. Hapana dhulma leo. Allaah ni Mwepesi wa kuhisabu)) [Ghaafir: 17]
 
Bob Marley alikufa na miaka 36, akiwa bado kijana mbichi kabisa.

Malcom X alikufa na miaka 39 akiwa na mipango mingi tu ya kuleta mabadiliko ya kisiasa kwa wamarekani weusi.

Martin Luther King alikufa na miaka 39 akiamini kwamba yupo tayari kuelekea mbinguni.

John Lennon alikufa na miaka 40, mmoja wa mashabiki wake alimpiga risasi.

Mwanamuziki Gerard Levert mzee wa Cassanova alikufa na miaka 40 baada ya kunywa dawa aina mbili tofauti zilizotengeneza sumu mwilini mwake.

Rajiv Gandhi alikufa na miaka 46, akiwa bado kijana mng'avu na mwenye matumaini mengi tu.

John F Kennedy alikufa na miaka 46, akiamini kuwa uchaguzi wa mwaka 1964 angeweza kushinda na kuiongoza Marekani kwa mihula miwili.

Edward Moringe Sokoine alikufa na miaka 46, akiwa katikati ya vita dhidi ya wahujumu uchumi.

Mjasiriamali Ruge Mutahaba kaondoka duniani na miaka 48 akiwa na mipango mingi mikubwa.

Nahisi Marehemu Ephraim Kibonde ni wa umri huo huo wa Ruge, nae kaondoka na uchangamfu wake maskini!.

Maishani unaweza usifikishe hata miaka 50 kwa mipango ya Mungu, unaweza ukawa na miaka 45 au chini ya hapo lakini kumbe wewe ni "mzee" tayari.

Ujumbe wa hao wote niliowataja na ambao waliaga dunia wakiwa hata hawajaishi nusu karne ni kwamba muda wetu ni mfupi.

Uhairishaji wa mambo (procrastination) wakati hujui kama wewe tayari ni "mzee" kwa mipango ya muumba wetu sio jambo jema.

Kesho hatuijui, kwanini tunapoteza muda kwenye kuendekeza siasa za makundi na upambe na uhasama wakati muda wetu hatujui utaisha lini?.

Vipaji vyetu na tuvitumie kwa ajili ya kuinua maisha yetu binafsi na kuuinua mustakabali mwema wa Tanzania.

Tunajua tumekuja lini duniani lakini hatujui hii sinema yenye mengi iitwayo maisha, itamalizika lini na sehemu gani.

RIP Kaka Kibonde, RIP Kaka Ruge. Siku zetu chini ya jua sio nyingi kama tunavyozipanga katika mipango yetu, dakika ya kufanya masuala ya muhimu ndio hii ya sasa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ