TANZIA Mtangazaji wa Clouds FM, Ephraim Kibonde afariki dunia. Azikwa makaburi ya Kinondoni,Dar es Salaam

TANZIA Mtangazaji wa Clouds FM, Ephraim Kibonde afariki dunia. Azikwa makaburi ya Kinondoni,Dar es Salaam

Kibonde alikuwa anaipa radha Jahazi kwa kuropoka kwake sijui nani ataifit style ile!!..
 
Aliwaponda sana kina Dr Ulimboka na walichokuwa wanakipigania enzi zile 2012, sasa yale yale waliyokuwa wanalalamika ndio hayo hayo yamemkuta. Nenda tu kaka panapokustahili
 
Pole sana familia kwa kumpoteza baba na mama. Nawaonea huruma sana watoto wa marehemu kwa kuwapoteza wazazi wao wote. Nina imani Mungu atawalea kwani yeye ndiye muweza wa kila jambo.

Pole aside, kifo cha kibonde kiwe fundisho kwa watangazaji wengine wanaotumia sauti zao kukandamiza haki za wengine au kupindisha ukweli. Tumejifunza kitu kufuatia kifo cha Ruge kutoka kwa watu mbalimbali kama Konki na Jide. Hili ni fundisho kuwa unapokuwa hai, jitahidi kuwatendea haki kila mtu bila kujali nafasi yake ktk jamii.

Habari za hivi punde ni kuwa mtangazaji maarufu wa Clouds FM, Ndugu Ephraim Kibonde amefariki dunia alfajiri ya leo tarehe 7 Machi 2019.

Kibonde alianza kusumbuliwa na presha akiwa katika msiba wa marehebu Ruge Mutahaba huko Bukoba mkoani Kagera na kuhamishiwa hospitali ya Bugando jijini Mwanza ambapo mauti yamemkuta.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza pamoja na Mkuu wa Vipindi wa Clouds FM, Sebastian Maganga wamethibitisha kutokea kwa kifo hicho.

Bwana ametoa, Bwana ametwaa

Mwaka jana Ephraim Kibonde alimpoteza mkewe mama Sara Kibonde. Zaidi soma >TANZIA: Ephraim Kibonde afiwa na Mke wake Sara Kibonde - JamiiForums

View attachment 1039958
Ephraim Kibonde akiwa na mkewe enzi za uhai wao​

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pole sana mkuu kwa uchungu unaopitia, ila kuhusu binadamu kufa hiyo ni nature tu, mzungu/mwarabu alijaribu kutuhadaa kuwa kuna maisha baada ya kifo, its just fiction...
Mkuu hata bila mzungu mbona imani zetu za jadi pia zimetufundisha hivyo. Hujasikia habari za mizimu,mahoka na matambiko mbali mbali kwa hiyo mizimu?

Sent from my itel S11 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom