TANZIA Mtangazaji wa Clouds FM, Ephraim Kibonde afariki dunia. Azikwa makaburi ya Kinondoni,Dar es Salaam

TANZIA Mtangazaji wa Clouds FM, Ephraim Kibonde afariki dunia. Azikwa makaburi ya Kinondoni,Dar es Salaam

Wana watoto watatu,mkubwa wa kiume yupo chuo kama si mwaka wa kwanza basi wa pili,wa pili sekondar, na wa tatu primary wakike hawa
Dah...sijui alijiwekea bima..dah... Kusaga inabidi alipe fadhila tu...hakuna namna...

Sent using Beretta ARX 160
 
Bob Marley alikufa na miaka 36, akiwa bado kijana mbichi kabisa.

Malcom X alikufa na miaka 39 akiwa na mipango mingi tu ya kuleta mabadiliko ya kisiasa kwa wamarekani weusi.

Martin Luther King alikufa na miaka 39 akiamini kwamba yupo tayari kuelekea mbinguni.

John Lennon alikufa na miaka 40, mmoja wa mashabiki wake alimpiga risasi.

Mwanamuziki Gerard Levert mzee wa Cassanova alikufa na miaka 40 baada ya kunywa dawa aina mbili tofauti zilizotengeneza sumu mwilini mwake.

Rajiv Gandhi alikufa na miaka 46, akiwa bado kijana mng'avu na mwenye matumaini mengi tu.

John F Kennedy alikufa na miaka 46, akiamini kuwa uchaguzi wa mwaka 1964 angeweza kushinda na kuiongoza Marekani kwa mihula miwili.

Edward Moringe Sokoine alikufa na miaka 46, akiwa katikati ya vita dhidi ya wahujumu uchumi.

Mjasiriamali Ruge Mutahaba kaondoka duniani na miaka 48 akiwa na mipango mingi mikubwa.

Nahisi Marehemu Ephraim Kibonde ni wa umri huo huo wa Ruge, nae kaondoka na uchangamfu wake maskini!.

Maishani unaweza usifikishe hata miaka 50 kwa mipango ya Mungu, unaweza ukawa na miaka 45 au chini ya hapo lakini kumbe wewe ni "mzee" tayari.

Ujumbe wa hao wote niliowataja na ambao waliaga dunia wakiwa hata hawajaishi nusu karne ni kwamba muda wetu ni mfupi.

Uhairishaji wa mambo (procrastination) wakati hujui kama wewe tayari ni "mzee" kwa mipango ya muumba wetu sio jambo jema.

Kesho hatuijui, kwanini tunapoteza muda kwenye kuendekeza siasa za makundi na upambe na uhasama wakati muda wetu hatujui utaisha lini?.

Vipaji vyetu na tuvitumie kwa ajili ya kuinua maisha yetu binafsi na kuuinua mustakabali mwema wa Tanzania.

Tunajua tumekuja lini duniani lakini hatujui hii sinema yenye mengi iitwayo maisha, itamalizika lini na sehemu gani.

RIP Kaka Kibonde, RIP Kaka Ruge. Siku zetu chini ya jua sio nyingi kama tunavyozipanga katika mipango yetu, dakika ya kufanya masuala ya muhimu ndio hii ya sasa.
Dah...Cha msingi ni kujipanga....yaani kutoacha pengo lisilozibika kwenye maisha yako binafsi...hasa kwenye majukumu...[emoji41]

Sent using Beretta ARX 160
 
Mwili wa aliyekuwa Mtangazaji wa Clouds FM, Ephraim Kibonde, umewasili wakati huu hapa nyumbani kwa wazazi wake, maeneo ya Mbezi Africana jijini Dar es Salaam.

Kibonde alifariki Machi 6, 2019 alipokuwa akiwahishwa Hospitali ya Bugando Mwanza baada ya hali yake kubadilika ghafla alipokuwa akitibiwa katika hospitali ya Uhuru jijini Mwanza.

Baada ya taratibu zote za kuaga na ibada, msafara utaondoka hapa nyumbani milango ya saa 9 kwenda kumlaza kwenye nyumba yake ya milele, katika makaburi ya Kinondoni, Dar es Salaam.

Kibonde alikuwa muongozaji wa shughuli (MC) kwenye msiba wa Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji wa Clouds Media, Ruge Mutahaba aliyezikwa Machi 4, 2019, alianza kujihisi vibaya mara baada ya maziko hayo yaliyofanyika Bukoba mkoani Kagera.
Hawawezi kuwa na Misa. Hao si mashahidi was yehova?
 
mwilipic.jpg
 
Mtoto wa pili wa mpendwa wetu Ephraim Kibonde akiwa kwenye hali ya huzuni kwani leo ndiyo siku ambayo anaenda kumpumzisha Baba yake kwenye makazi ya milele na kutomuona tena, Huzuni imetawala, mioyo inayovuja jasho la uchungu huku machozi yasiyokatika yakidondoka
51951573_2183937435254738_4928346515966822188_n.jpg
 
Rafiki yangu Ephrahim, Tulicheza Basketball, Football, Keram, Table Tenis pamoja wote Don Bosco Upanga, Tulikuwa hatukosi kila siku Don Bosco baada ya shule, baada ya ukubwa vijana wote kila mtu aliaanza maisha yake, Tulikuwa tunakoona enzi hizo CTN TV yaani we acha tu
Ulikuwa MC kwenye Harusi yangu mpaka leo nina kumbukumbu hiyo saa hiyo mwenzangu ulishaanza maisha ya majukumu long time Brother
Mungu akulaze mahala pema peponi Amin
Pole kwa Familia, Mungu awatunze watoto wako Inshaalah Amin

Nami pia nakumbuka kile kijiwe chenye mabomba pale nyumba ya ile kona inayotazamana na Don Bosco!

Ephraim Kibonde ni mmoja watu ambao hawakati tamaa kutumia vipaji vyao na kuchakarika na alianza mapema sana.

Ni jambo la kusikitisha na kuhuzunisha kuondoka duniani tukiwa bado tunafaidi maisha yetu na kuacha familia changa lakini yote hayo ni mipango ya Mungu na kifo hakina appointment ni wakati wowote ule na mahali popote.

Namkumbuka Ephraim wakati kuna kipindi fulani tulipiga boksi pale UK (Royal Mail) na alikuwa so entertainer yaani ni mtu ambae utapenda kuwa nae karibu kwa vichekesho na mazumgumzo yake.

Hakika, kipindi cha Jahazi kitakosa mmoja wa wachangiaji mahiri sana.

Halikadhalika CMG imepoteza vipaji maalum vya Ruge Mutahaba na Ephraim Kibonde.

Pia wadau mbalimbali waloshiriki na Ephraim nao watamkosa mtu muhimu sana.

RIP Ephraim.
 
Back
Top Bottom