Mtangazaji wa redio hajui kazi ya Baraza la Mitihani la Taifa NECTA

Mtangazaji wa redio hajui kazi ya Baraza la Mitihani la Taifa NECTA

Ndio ujue kuna radio presenter na journalist! Hapa bongo hawa wawili hatuwatofautishi. mmoja anajua kusoma kilichoaandaliwa na mmoja ni chanzo cha yanayoandaliwa kusomwa na radio ama tv presenter! Sasa unapokuta presenter anaanza kufanya kazi ya journalist wakati hajabombea katika hilo ndo utasikia madudu mengi yafananayo na hayo.
 
Mkuu kufeli kwa wanafunzi wenye uwezo mzuri haisiani na necta hujui huyo mwanafunzi alikuwa katika state gani kipindi

cha mitihani hata ww najua utakuwa shahidi umeshasoma na watu wenye uwezo mkubwa darasani lakini wakaja

wakakimbizwa na mtihani wa mwisho.

Hili tatizo limepigiwa kelele sana lakini wakuu wa kaya wameziba masikio haya ndiyo matokeo yake.

Necta hawawezi kuepuka hili kwani haya matokeo yanawalakini sababu hata wanafunzi ambao walikuwa na uwezo mzuri wamepigwa chini
 
Gerald Hando nilisha muombea msamaha kwenye swala la Bunge lisirushwe live maana natambua uwezo wake wa ku reason ni mdogo mno.Tatizo la watangazaji wa redio hizi za udaku ndio wale walofeli sasa ulitegemea angemuuliza maswali gani mama Ndalichako?Hivi kama sio uwenda wazimu kweli mtangazaji hajui majukumu ya NECTA?Watangazaji makini hujiandaa kwa kusoma yale mambo anayotarajia kuhoji.Najisikia aibu baadhi ya watangazaji wanaaibishhwa na watangazaji feki kama hawa?Nafikiri watangazaji nguli kama Gabriel Zakaria,Baruan mwahuza n.k kaani na hawa vijana welekezeni mnafanyeje interview wanazidi kuwadhalilisha na tasnia yenu ina onekana ya mambumbumbu.
 
Back
Top Bottom