Mtanzania acha kuji-stress kuwalipia watoto wako mamilioni kwenye shule za English Medium. Kilichomtokea Mr. Ibu kinaweza kukutokea hata wewe

Kuna watoto walio na dependency mindset kama walio soma EMs. Huko EMs kila kitu wanatafuniwa . Kayumba mtoto anajifunza kuwa fighter kuanzia darasa la kwanza . Anaanza kujifunza uhalisia wa maisha kuanzia darasa la kwanza. Hakuna mtu anae mpetipeti tofauti na huko EMs walimu wana show fake love to your children
 
Hizi shule zetu za kingereza nikwajili ya kufanya vizuri tu mitihani ya hapa kwetu. Hakuna cha ziada.
Hujui unachoongoe Kila mahali mtu unakuwa inatakiwa ku perform vizuri sana bila kujali ni ndani ya nchi iwe kijijini au popote

Mzazi unapopeleka mtoto shule kayumba na matokeo unayo kuwa asilimia kubwa wanafanya vibaya akili unakuwa huna .Mtoto anatakiwa kujengwa ku. Perform vizuri Kila eneo anatakiwa asijenge kichwani mentality ya kuwa yeye failure kumbe umempeleka shule bovu kaangalie vitoto vinavyotandika A masomo yote na division one vina confidence Kali ya kusoma na ambition kubwa mno utasikia nataka kusoma niwe Engineer au Doctor au Professor nk failure inavunja sana confidence ya mtoto kwenye malengo ya maisha .Mzazi kumpeleka mtoto environment ya failures humtendei mtoto Haki heri hata utembee uchi Kwa kujinyima mtoto asome shule nzuri
Kilimanjaro Mfano hata ng'ombe wa maziwa mzazi hata awe maskini akiwa na ng'ombe wawili wa maziwa anasema huyo mwingine maziwa yote nauza ada ya Watoto shule nzuri huyu mwingine ndio wa nyumbani hata shamba la migomba anagawa kipande kile migomba yote ada ya Watoto shule nzuri kipande hicho kingine ndio tutakula

Future ya mtoto ni gia ya kubadilisha generation kama mlikuwa maskini future ya mtoto inatakiwa kuandaliwa vizuri kama gia ya kubadili generation kuwa kije kizazi kipya tofauti na chako kilichosoma Kayumba
 
Unamkuza mtoto kuliko uwezo wake

Kutafuniwa Hadi chuo kikuu kupo digrii ya kwanza eneo pekee analoachiwa ni eneo la research kumzoeza kidogo kidogo kufanya research

Masters degree inakuwa nusu Kwa nusu kutafuniwa asilimia hamsini research asilimia 50

PhD kutafuniwa yaweza kuwa zero au percent ndogo sana

Mtoto wa sekondari kayumba kumgeuza sawa na mtu anasoma PhD akomae ajitafutie mwenyewe bila kutafuniwa ni uonezi wa Hali ya juu hajafikia kiwango hicho Kwa umri wake.Akili ya mtoto inatakiwa kukua slowly gradually
 
Kwanini Kayumba watoto hawafundishwi? Mimi sizungumzii kutaguniwa huko mkuu
 
Mbona sijaona taarifa ya Shule walizo soma au wewe umejiongeza
 
Yan mtoa post tafsiri yako ni sawa na kutuambia "tusipande daladala kwasbb tunaeza kupata ajali"
 
Tunauziwa kingereza kwa mamilioni ya pesa alafu ujuzi kidogo sana.

Kama umekusudia kumpa mwanao elimu ya tofauti msomeshe international schools. Hizi nyingine unauziwa kingereza tu hakuna cha ziada.
Sasa si afadhali hata hicho kingereza awe nacho!! Ni pumba tupu mara mia umpeleke hata british council au kwa ras simba
 
Kizazi kikubwa kinachokuwa scammed na hawa wamiliki wa English medium schools ni kile ambacho ukichunguza kilifeli wakati kinasoma miaka ya 80-90-early 20's. Unakuta wengi hawakupata access ya education hivyo wanaamini mafanikio ya mtoto kimaisha ni elimu hii ya the so called english medium.

Unakuta mzazi anajistress anacheza vikoba,anatapeli na kunyang'anya huku na huko ili mtoto asome english medium za 3-5M.

Yaani hata ada ya chuo kikuuu pale UDSM haifiki huko. Hiki kizazi hakihoji pindi kinapopandishiwa ada za shule kila mwaka na hawa wamiliki wa hizi shule huku ukiangalia quality na hata huduma kama za chakula na accomodation ni za kawaida mno ila wanaambiwa walipe pesa ndefu sana.
 
Kama una uwezo wa kumlipia mtoto 5M kila mwaka kwanini zile oesa usimuhifadhie kwa kipindi cha miaka 13 ya elimu yake uje kumpatia huko mbeleni....mtoto afike chuo kikuu akute mzazi wake alimuwekea akiba ya zaidi ya milioni 65 akimaliza aanzie maisha au kama mdau aliyesema kuwa anawanunulia wanawe viwanja kila mwaka wa masomo kwa ada ile ile ambayo angeilipa EM School.
 
Cha msingi, somesha kwa uwezo wako,
Kuacha kufanya kitu kzr, kwa sababu tu, kuna watu walifanya wakaumia, ni ujinga,tusipande ndege kwa sababu kuna waliopanda ndege ikaanguka ikawaua!
Au, tusipande meli kwa vile Mv bukoba ilizama, au tusijenge nyumba kwa vile, kuna watu waliangukiwa na Kuta za nyumba, au tusisome wala kupeleka watoto shule,kwa vile tu, mbona Diamond hakusoma na Ana pesa ndeeefu.
Angalia na upande wa pili, watoto wa kikwete ni marubani Qatar! Ukafikiri waliishia LA saba!
Watoto wa Aden lage,wamesoma Melbourne austalia universities, ukiwalinganisha na waliosoma UD, unafikri yupi ana chance kubwa ya kuapata ajira kwenye mashirika ya kidunia, world Bank, UN, ICJ,
Acha ujinga, wa sizitaki mbichi hizi, kwa vile umeshindwa kuzifikia,
Kuna uhusiano, wa, karibu Sana Kati yq kuwa na pesa na akili,
Mtoto wa Mo anasoma IST, Ada milioni 60! Kwa mwaka,kwa logic yako, huyu anapoteza muda!sasa na ni mwenye akili tumsikilize, wewe apeche alolo au Mo!
Mtoto wako anasoma kayumba, class mate wake, ni watoto wa, katibu kata,jirani mchoma mkaa, police, mwenzio watoto wake wapo International, class mate wao ni watoto wa mabalozi, mawaziri, foreigne diplomats,
Yupi anakuwa na network Bora!
Angalizo, unaweza soma kayumba, na ukafika mbali Sana, kama dangote, lakini,safari ni ndeeefu na ngumu, lakini, ukimwezesha mtoto pa kuanzia, na base nzuri ya elimu,connection, atafika kirshisi,
Hakuna ufahari, we ulisoma kayumba, na mtoto asome kayumba!
Kaangalie matokeo ya kidato cha nne, utajua kwanini tuna somesha hizo shule,
By the way, shule zetu tunazoita English medium, kwa nchi zilizoendelea ni shule za kawaida kabisa, ndivyo shule zinatskiwa kuwa,
Hizi kayumba, ni mabanda ya kuku tu!
 
Sidhani kama hata umeelewa nilicho kiandika mkuu
 
Mo hategemei kuja kuona mwanawe anahangaika na bahasha akitafuta ajira kutoka ofisi moja mpk nyingine. Mo anasomesha wanawe ili waje kurithi ,kusimamia na kuendeleza ukwasi wa familia ya DEWJI.

Watoto wa kikwete na wako wana ufanano gani? Familia ya kikwete ina ukwasi mkubwa hivyo inahitaji warithi watakaoendeleza mali za familia.

Ila ww pangu pakavu tia mchuzi kujistress kulipa mamilioni kwenye EM schools uchwara ili wanao waje kugombania shuttle pale mabibo hostel ni upumbavu wa kiwango cha SGR
 
Naunga mkono hoja halafu huwaga wana hangaika kweli kwenye mikopo chuo kwa sababu wengi huwa hawapati mkopo na mzazi anakuwa nguvu zimeisha au hakujua kama atatakiwa kuendelea kuonyesha umwamba wake wa kulipa ada hadi chuo kikuu. Wanaishia kuwatesa tu vijana wao bila sababu ya msingi
 
English Medium ni Muhimu kwa wanangu, naplay part yangu na wao wakikua wataplay part yao, wasipo play it's all fine
Mmmh!! Wabongo bwana vitu vingine acheni mkumbo.Nafuatilia hizi shule walimu hawajui grammar kabisa yani wanawafundisha utumbo tena ni hizi shule zenu kubwa kabisa[emoji2357]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…