Mtanzania, Alphonce Simbu ashika nafasi ya tatu Marathon IAAF LONDON

Kama nchi itahamishia fungu kubwa kwenye riadha tutafika mbali hongera sana Simbu kwa juhudi binafsi
 
Kumbe mnajielewa ninyi ni vichwa vya wendawazimu kila mtu anajifunza kunyolea tukiongea ukweli mnaona tunadharau. Kumbe kiuhalisia unajua hali zetu zilivyo wtz bana
Nafasi ya tatu sio mbaya...ina medali pia.
 

Huyu Kirui ni kama anatumia diesel,mapafu gani ya binadamu muda unavyozidi kwenda ndio anaongeza mwendo?

Ila Simbu kamkosa kosa sana yule Muethiopia nafasi ya pili,ni kama point 49 kwa 51.Si haba...Hela atakayopata inatosha sana sana kwa kuanzia maisha,maana jamaa alikuwa anakaa chumba kimoja tu na sebule kule Arusha.

Wakati ule majirani pale Arusha hawakujua kama ameenda Rio de Jeneiro kwenye Olympic,walishangaa kumuona na kumfananisha kwenye TV wakati anakaimbia.Mkewe akiwa nyumbani hana hata Tv kujua nini mume wake anafanya huko Brazil.

Mungu amtie nguvu,amzidishie na siku moja ampe medali ya ushindi ya dhahabu kwa moyo wake wa kujituma.Anatoka Singida vijijini sana,katikati ya jamii masikini.Kwa kipaji chake,Mungu atamjalia.

Kama namuona jamaa yangu Gidabudayi,mzee wa Shirikisho la Riadha Tanzania
 
Hayo maisha alishaachana nayo zamani, Sasa hivi anakula vinono ndani ya udhamini wa Dstv.
 
Na pesa ya kutosha tu.Kama ile ya Brazil ilimpa wadhamini kama DSTV,hii itampa wengine zaidi na zaidi na itamuingizia pesa.

Apate tu mtu wa kumuongoza vyema awekeze kwa ajili ya baadae
Sasa hivi amejifungulia milango. World Championship Bronze Medallist sio mtu mdogo, ameingia kwenye historia ya riadha duniani.

Hata Usain Bolt mwaka huu kaishia bronze medal!
 
Hayo maisha alishaachana nayo zamani, Sasa hivi anakula vinono ndani ya udhamini wa Dstv.
Asante sana
Mimi nakumbushia tu kabla ya kwenda Rio jinsi alivyokuwa akiishi.
Mtindo wa maisha ulibadilika baada ya kutoka Rio,ila kabla ya Rio huo ndio ulikuwa mtindo wake wa maisha.
 
Huyu dogo yuko vzr, akiweka bidii zaidi atafika mbali
 

Yeah, soon we are going to take over the marathon race from dominance of Ethiopians and Kenyans, today the story of Tanzania forcing itself in the marathon ''elites'' is being splashed all over the world through TV screens !.
 
Hayo maisha alishaachana nayo zamani, Sasa hivi anakula vinono ndani ya udhamini wa Dstv.
Sasa hiivi anaanza ku,deal na IAAF direct...atakuwa anaalikwa kabisa, marathonskama japan,usa,uk lazima wamualike...kwenye michezo mingine tungesema among top seeds.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…