Mtanzania apata ajali Michigan, Mahututi..

Mtanzania apata ajali Michigan, Mahututi..

Status
Not open for further replies.
Ningeshauri mtu mwenye picture ya late Ndalima Nzaro aiweke hapa ili na wasio mfahamu kwa sura wapate nafasi.

R.I.P Ndalima
 
Ab-Titchaz,

Wakati tunaendelea kuombeleza ni vizuri pia mkashauriana na familia ya Marehemu kungalia uwezekano wa kuwachukulia hatua za kisheria Polisi waliohusika na hiyo high speed chase.

Katika hali ya kawaida na kulingana na kosa la huyo 15 years ( tunaambiwa aliwaonyesha ishara ya kidole cha kati polisi) halikuhitaji mafukazano yale hususan ktk dunia ya leo ya teknolojia wangeweza ku mtrack na kumpata kirahisi bila ya kusababisha madhara kwa public.

Hapa UK trafick offense ndogo kama hizo polisi huwa wana abandon chase na hasa mtuhumiwa akiwa anaelekea maeneo ya watu wengi, unless awe jambazi ambalo halitakiwi kuwa on the loose hata dakika moja.

Naamini polisi hapo wame act irresponsible na wana big share of blame. Something should be taken against them.

Naomba kutoa hoja


Yegho Masatu,

Kwanza poleni wafiwa. Najua ni ngumu kwa wafiwa wakati huu, lakini suala la msingi ni kuakikisha kwamba a next of kin anatunza paperworks zote associated na hii kesi and then he/she needs to consult a lawyer ambaye amespecialize kwenye trafic & motor accident.

Mdau
 
May all beings attain enlightenment.

A life senselessly and cruelly robbed.

kweli kabisa.

namuomba Mwenyezi Mungu awape faraja ndugu jamaa na marafiki wa marehemu, hususan mtoto na mchumba wa marehemu, na ampe pumziko jema la milele marehemu.
 
Tunawaombea kwa Mungu kwa kipindi hiki kigumu familiya yote ya Nzaro. Mpewe moyo wa uvumilivu kaw kipindi hiki.
Bwana ametoa na Bwana ametwaa - Jina la bwana lihimidiwe- AMEN
 
277221852_476e8916f0.jpg

Absolve, we beseech Thee, O Lord,
the soul of Thy servant Ndalima,
from every bond of sin,
that being raised in the glory of the resurrection,
he may be refreshed among the Saints and Elect.
Through Christ our Lord.

Amen
 
Titchaz

Pole, majonzi na simanzi si kwako pekee. Anapofariki jamaa hukumbusha misiba mingi sana, ndio maana tunalia tunaposikia mtu katutoka hata kama hatumjui. Inaumiza sana kuondokewa na jamaa ghafla namna hii, few days back alikuwa na mzima mkicheka na kuongea, na imegeuka kuwa impossible...never again. Its so painful. Pole sana na wakati unaomboleleza jua huko peke yako.
 
Titchaz

Pole, majonzi na simanzi si kwako pekee. Anapofariki jamaa hukumbusha misiba mingi sana, ndio maana tunalia tunaposikia mtu katutoka hata kama hatumjui. Inaumiza sana kuondokewa na jamaa ghafla namna hii, few days back alikuwa na mzima mkicheka na kuongea, na imegeuka kuwa impossible...never again. Its so painful. Pole sana na wakati unaomboleleza jua huko peke yako.

Thank you so much for your kind words.
 
Natanguliza rambirambi kwa familia,ndugu na marafiki wa Ndalima, Mungu ailaze roho ya marehemu peponi. Ameen. Watanzania sote tulio nje tunakuwa wamoja hasa linapotokea jambo la kushikamana kama hili la msiba, kwani kifo hakitabiriki. Ombi kwa mkuu Ab-Titchaz na Mkjj ningeshauri kama inawezekana mkatupatia kiungo kwa mtu aliyeko hapa UK ili sisi tulio hapa tuwasilishe michango yetu? it is more convenient and quicker for those of us who are on this side. Ahsante.

Nasubiri tupate SWIFT CODE ili watu walioko nje ya US waweze kutumia benki zao kutuma michango yao. Tunashukuru kwa support kubwa ambayo tumeipata kutoka kwa watu mbalimbali. Kwa wana JF, Ndali alikuwa ni mmoja wetu hapa na mara nyingi tukikutana tunaendelea mazungumzo yetu ya JF nje ya hapa. So, siyo tu kwamba familia imempoteza bali pia familia ya JF imempoteza.

Tutawaletea update kwa kadiri mipango inavyoendelea.
 
Ni masikitiko makubwa kupoteza kijana kama kama huyu.

Mungu na awajaze nguvu wafiwa

Tangulia kwa amani ndugu yetu,sisi sote njia yetu ni moja.
 
Tutayasomaje mawazo yake alookuwa akichangia humu bila kuathiri utambulisho wake?
 
Kwa wana JF, Ndali alikuwa ni mmoja wetu hapa na mara nyingi tukikutana tunaendelea mazungumzo yetu ya JF nje ya hapa. So, siyo tu kwamba familia imempoteza bali pia familia ya JF imempoteza.

Alikuwa akitumia jina gani hapa JF, au itaendelea kuwa siri.?
 
Wana-JF,

maila.jpg

Kwa masikitiko makubwa Familia ya Mohamed Nzaro na Balozi Eva Nzaro inatangaza kifo cha mtoto wao Ndalima Yusuph Nzaro kilichotokea siku ya Alhamisi Katika Hospitali ya Chuo Kikuu cha Michigan mjini Ann Arbor ambapo alikuwa amekimbizwa kutibiwa baada ya ajali ya gari iliyotokea usiku wa kuamkia Jumanne ya Oktoba 14, 2008.

Gari alilokuwa akiendesha marehemu liligongwa na gari nyingine wakati likisubiri taa za kuongozea magari.

Mipango ya kuusafirisha mwili wa marehemu nyumbani Tanzania kwa mazishi inaendelea. Vile vile, utoaji wa heshima za mwisho mjini Detroit unatarajiwa kufanyika siku ya Jumamosi tarehe 18 Oktoba, 2008. Muda rasmi utatangazwa baada ya maandalizi kukamilika.

Familia inapenda kutumia nafasi hii kuwashukuru na kuwaomba msaada wenu wa hali na mali katika kufanikisha safari hii ya mwisho ya kijana wao mpendwa Ndalima.

Michango kwa ajili ya msiba huu inaweza kupelekwa moja kwa moja kwenya akaunti maalum ifuatayo:

Bank Of America:

A/C Name: Mboja Nzaro (Dada wa Marehemu)
Routing No. 072000805
A/C No. 5407722411


Mawasiliano zaidi Kuhusu habari za msiba huu wasiliana na wafuatao:

Anna Royal Mfinanga 248-778- 6395
Abdul Kufakunoga 248-515- 5509
Salum Ndolanga 248-796-1267
Philemon Mnzava 248-417-5015
Leo The Saint 614-426-3422


Msiba huu kwa Detroit unafanyika nyumbani kwa binamu yake Ayubu Mfinanga.
Anuani ya Kwa Ayub:

22255 Hessel
Detroit, MI 48219


Tutaendelea kuwahabarisha kwa kadiri mipango inavyoendelea.

Asanteni kwa sala zenu, ushirikiano wenu na misaada yenu.

Rose1.gif

FAMILIA YA NZARO

Inna lillahi Wa ina Ilayhi Rajioon, Mungu amlaze mahala pema, Amina.
 
Kamwe hatusemi wanachama waliotutoka ambao hawakutoa idhini ya majina yao. Alipenda kuwa anonymous (hata mimi in real life sikuwahi kumuuliza yeye ni nani hapa). Najua alikuwa anaingia mara nyingi tu kwani he was always updated.

Wiki ile iliyopita tulipokutana kwenye msiba wa baba yake Ayubu yeye alikuja right behind me na mwanawe; baada ya kusalimiana akawa anazungumzia mambo ya JF na hata tulipokaa ndani baadaye na watu wengine tulikuwa na mjadala kuhusu mambo ya mabaki ya Utumwa, tofauti ya Utumwa wa Pembetatu na ile ya utumwa uliopeleka watu wetu mashariki ya kati. He was so fascinated with the whole concept.

Nakumbuka zaidi changamoto alizokuwa ananipa kwenye suala la vijana wa Ukraine, tulikuwa na mjadala mzito sana kuhusu jukumu la serikali na wazazi katika aidha kuwarudisha watoto nyumbani au kuwaendeleza na masomo.

He was very engaging.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom