TANZIA Mtanzania auliwa kwa kupigwa risasi Marekani, anaitwa RODGERS KYARUZI, alipata maluweluwe

TANZIA Mtanzania auliwa kwa kupigwa risasi Marekani, anaitwa RODGERS KYARUZI, alipata maluweluwe

Discrimination ipo sana USA kwenye mighahawa ikiwa wewe sio mzungu Kuna sehemu ukienda unaweza ambiwa all table has been reserved yaani inauma sana kisa wewe ni black, coloured au Asian #Americawillfall

Mimi napenda sana watu wabaguzi, Wazungu ni lazima wajilinde dhidi ya inferior cultures kama zetu, wasipofanya hivyo watakuja kuongozwa na akina Nape au Makamba.

Nchi kama Japan wakiruhusu inferior cultures wamekwisha, Japan ni tajiri sababu no immigration from third World!
 
Dah, sijawahi kusikia nchi za Kiarabu wanawaua watu kwa kuomba omba, tena ndio wanapenda kweli kusaidia waombao.
🙆🏿‍♂️🙆🏿‍♂️ Husika malalamiko ya dada wa kiafrika Mateso wanafanyiwa huko kwa waarabu ?
 
Naona ajenda ya mleta mada ilikuwa haijaeleweka.
Mkaenda kule asipotarajia.

Nilitaka kushangaa 'huyu Mtu' leo kuonea huruma 'marehemu wa race' yetu tena asiye wa itikadi yake na mbaya zaidi tukio lifanywe kwa hao Wazungu kwenye hilo Taifa kubwa!
 
Kifo huwa ni cha kijinga kweli,iki kiweze kuchomoka na wewe lazima kikutafutie sababu tu.
 
Anaandika MC Baraka Galiatano From Face Book Nime Copy na Ku Paste Kama Ilivyo

[emoji1484][emoji1484][emoji1484][emoji1484]

TANZIA :Wandugu wanajumuiya wa Tanzanite Community of Georgia, TCG.

Kwa taarifa zinazoendelea kwenye mitandao ya jamii hasa pia kwenye vyombo vya habari na vyombo vya dola, tunasikitika kutoa taarifa hizi za Mtanzania mwenzetu Ndugu Rogers kututoka gafla!!

Uongozi wetu umepata fursa ya kuongea na Mama mzazi wa Rogers, Mama Rose Yorke.
Kama jumuiya, Tunasikitika kuwatangazia kifo cha mwenzetu Rogers Kyaruzi Mtanzania mwenzetu na maisha yake kwa ufupi aliyoyaishi hapa Georgia USA:

~ Rogers alikuwa mtoto pekee wa kiume akiwa na umri 30, kati ya watoto watano kwenye familia yao, ameacha dada, Myra na wadogo zake wakike watatu (Agness, Maya, na Miya).

~ Rogers na mama yake walikuja hapa USA mwaka 2001 akiwa na umri wa miaka 10, waliishi Warner Robins GA.

~ Baada ya masomo yake ya juu; (major in Computer Networking) alifanikiwa kuoa Bi. Niteecha, ambapo walipata mtoto mmoja wa kiume (Raja, 5 yrs). Huku wakiishi Ellenwood GA na familia yake.

~Rogers alikuwa mjasiliamali ambapo alikuwa mtu wa maendeleo, aliwekeza kwenye biashara mbalimbali ikiwa pamoja na kumiliki mtandao (website) binafsi na kupata mafanikio makubwa.

~ Rogers alikuwa na rafiki yake wa karibu tokea utotoni alipofika hapa USA, huyu rafiki nae mwezi uliopita alitangulia mbele za haki jambo ambalo lilimuacha na huzuni kubwa.

~ Jumatatu ya tarehe 2 May hadi asubuhi ya Jumatano 4 May mwaka huu, Rogers alikuwa kwa mama yake Warner Robins GA, ambapo alikwenda kumtembelea.

~ Siku ya tukio, Rogers alikuwa ana appointment Apple store, Lenox Mall, karibu na eneo la tukio. Muda mfupi kabla ya tukio Rogers aliongea na mama yake na kusema, “Mama kila nikiingia kwenye gari namuona rafiki yangu aliyefariki amekaa pembeni yangu Mama, Mama naogopa, pls njoo unifate
Mama kwa kuwa anakaa mbali na Buckhead akampigia mke wa Rogers ili awahi aende kumchukua.

~ Mke wa Rogers kufika kwenye tukio, alikuta Paramedic wanatoa huduma ya kwanza, ambapo Rogers aliweza kumuangalia mkewe machoni ingawa hawakumruhusu, baadae hospitalini aliripotiwa kaaga dunia!!!!

~ Kwa habari za vyombo vya dola na Mama mzazi, ni kuwa uchunguzi unafanyika na majibu yatatolewa ndani ya siku tano!!

~ Wakati familia ikisubiria taarifa rasmi ya kitengo cha upelekezi hapa Jimboni Georgia, GBI. Familia imepanga mazishi kufanyika hapa GA, Warner Robins.
Taarifa kamili juu ya Safari ya mwisho Kwa mpendwa wetu itatolewa baadae!

~ Kama watanzania, tunaomba tuendelee kuiweka kwenye maombi yetu ya kila siku familia hii hasa kwenye kipindi hiki kigumu wanayopitia.

Bwana ametoa na Bwana ametwaa Jina la Bwana lihimidiwe.[emoji1374][emoji1374][emoji1374][emoji1374][emoji1374]

Peter Okungu, TCG - President.
 
Kuna huyu jamaa DIBAJI alinitapeli kwa ulaghai wake kisa anaishi marekani akanamnia nimtafutie kiwanja Dodoma, na hakika nilizunguka mji mzima takribani kwa week mbili nikapata kiwanja,nilimwambia jamaa na kirahisi tu akanambia amehahirisha bila hata kusema asante,mzunguko huo nilipiteza pesa zangu na mda wangu na jamaa hakutimiza ahadi.yake kwangu ya kuninunulia bajaji ya ambayo ningeendesha kwa mkataba.

Popote ulipo ulaaniwe sana wewe jamaa DIBAJI
Mbona jamaa yupo active?
Oyaaa DIBAJI acha itikadi za Ugumu wangu
 
Sasa mambo gani ya kujidhalilisha hayo kwenda kuombaomba watu huko kwenye hoteli? Mtu unasikia fulani yupo marekani kumbe ndio maisha yao hayo.duuh poleni mnaopenda kwenda kuishi huko.

Kwani huku hawauliwi??

Poli-ccm wanaua raia kila siku
 
Hawa jamaa weusi wenzetu wa US hivi kwa nini polisi akiwasimamisha, wanakimbia? Wengine wanapigana mieleka na polisi! Wengine wananyang'anyana bunduki na polisi! Hivi kwa nini? Nashangaa kwa nini huwa wataki kwenda kituoni ama mahakamani na kujitetea huko?
 
Poleni sana wafiwa, Poleni sana Watanzania popote mlipo, Poleni sana Tanzania Diaspora wa USA. sote tunyayue sauti kulaani kitendo hiki.

USA wanajulikana kwa ubaguzi wao kwa watu weusi, huyu Mtanzania mwenzetu na yeye yamemkumba? Au kauliwa na mweusi mwenzake?

The Georgia Bureau of Investigation has identified a man who was shot and killed Wednesday afternoon after struggling for an Atlanta police officer's gun at a restaurant in Buckhead.

The shooting happened around 2:45 p.m. at the Lenox Village business complex, located in the 2700 block of Lenox Road.

Soma zaidi: https://www.fox5atlanta.com/news/gb...over-atlanta-officers-gun-buckhead-restaurant

Habari inajieleza yenyewe lakini haijakamilika kwa kina, sema mtangazaji anaongea Kiswahili kibovu, hana sauti yenye haiba ya utangazaji. Mwenye maelezo zaidi atie nyama.

Poleni tena wafiwa





===========================


MAMLAKA ZAELEZEA TUKIO LA RODGERS KYARUZI KUULIWA KWA RISASI

Ofisi ya Upelelezi ya Georgia (GBI) imemtaja mtu ambaye amepoteza maisha kwa kupigwa risasi na askari baada ya kutokea purukushani Mei 4, 2022 kuwa anaitwa Rogers Kyaruzi.

Rogers Kyaruzi amekuwa akitajwa mara nyingi mitandaoni kuwa ni Mtanzania, alikuwa ameshabadili uraia na kuwa raia wa Marekani.

GBI wanasema tukio hilo lilitoka nje ya Mgahawa wa Buckhead, saa 8:45 mchana, ambapo askari Lawrence Holland aliyekuwa akilinda usalama karibu na maeneo hayo alimkuta Kyaruzi akidaiwa alikuwa akifanya vurugu.

Alipojaribu kumtuliza ilishindikana na Kyaruzi akawa anataka kuchukua silaha ya askari huyo, ambapo katika kujilinda akafyatua risasi iliyompata Kyaruzi.

Kyaruzi aliyekuwa na umri wa miaka 30 alikuwa Mkazi wa Lithonia, alipelekwa Atlanta Medical Center ambapo ndipo mauti yalipomkuta akiwa hospitalini hapo.

GBI wamesema kuwa uchunguzi unaendelea kiwemo kupitia video iliyorekodiwa na kamera ya askari huyo kupitia vifaa maalum wanavyovaa askari.

Takwimu zinaonesha askari huyo anakuwa wa 45 kuhusika katika tukio la kurusha risasi ambalo linalofanyiwa uchunguzi na GBI tangu kuanza kwa mwaka 2022.

DADA WA KYARUZI AZUNGUMZA
Myra Yorke ambaye ni dada wa Kyaruzi anasema: “Nilishtushwa sana na taarifa hiyo, sijui nini kimetokea, tunasubiri uchunguzi.

“Kaka yangu alihamia hapakutoka Tanzania akiwa mdogo, alikuja Marekani kuishi katika ndoto yake, alikuwa mcheshi na mtu ambaye anapenda utani.”


KIONGOZI WA WATANZANIA AELEZEA HISTORIA YA KYARUZI
Mtu mmoja ambaye amejitambulisha kuwa ni Kiongozi wa Watanzania waliopo Georgia, Marekani amesimulia kuhusu anavyomfahamu marehemu na kufafanua kilichotokea:

“Rogers Kyaruzi ni mzaliwa wa Tanzania, alikuja hapa akiwa na umri wa miaka 12, baadaye mama yake aliolewa na Mghana ambaye ni Profesa.

“Kyaruzi alihitimu masomo yake hadi ngazi ya chuo, maisha yao hayakuwa mabaya katika familia.

“Kyaruzi ni mmoja wa Watanzania ambao wamekuja muda mrefu na hawapo karibu sana na Watanzania wengine kama kina sisi ambao tumekuja hivi karibuni, hiyo ni kwa kuwa maisha yao yamebadilika na kuwa kama Wamarekani, hata uzungumzaji wao unabadilika.

“Mimi sikuwa namjua kwa ukaribu, lakini ni Mtanzania kabisa hata kama alikuwa ameshachukua uraia wa Marekani, mama yake yuko hapa na ni mwanajumuiya mwenzetu (Watanzania).


CHANZO CHA KIFO
“Kyaruzi alikuwa na rafiki yake wa karibu sana ambaye alifariki mwaka jana (2021).

“Siku ya tukio (Mei 4, 2022), Kyaruzi alipofika eneo la tukio akaingia kwenye mgahawa baada ya kutoka wakati anaingia kwenye gari inadaiwa akawa anamuona rafiki yake huyo ambaye alishafariki, akitoka ndani ya gari hamuoni.

“Akampigia simu mama yake kuomba msaada kumwambia anahisi anaona kama kuna maluweluwe yanamtokea, mama mtu akamwambia kuwa yuko mbali muda huo na akampigia simu mke wa Kyaruzi ili aende eneo la tukio.

“Baada ya hapo Kyaruzi akawa anapiga kelele akiomba msaada kwa watu wanaopita, ikaonekana kama anafanya vurugu, alipotokea askari akajaribu kumtuliza lakini ikawa ngumu na inaonekana kuna vitu ambavyo walitofautiana.

“Kumbuka kuwa Kyazuri alikuwa ni mpiganaji wa mieleka, hapo ikatokea mshikemshike, akamkamata askari chini na kumuweka chini kwa dakika kadhaa, lakini ghafla askari akampindua na kumuweka chini kisha katika kujilinda akafyatua risasi ambayo ndiyo iliyomuua mwenzetu.

“Hata nilipozungumza na mama yake baadaye akakiri kupigiwa simu na mwanaye na kusema mwanaye hakuwa sawa kichwani, hata video za tukio lenyewe nilizoona zinaonesha alikuwa akipiga magoti kama anayeomba msaada, yaani ni kama alikuwa amechanganyikiwa hivi.”

Source: Ajc & Fox5atlanta

Vijana wa kihaya huwa bia haiwakubali, wakinywa huchanganyikiwa, ndivyo walivyo.
 
Back
Top Bottom