Mtanzania kwafukuta, Absalom Kibanda kupewa likizo ya lazima kupisha uchaguzi Mkuu

Mtanzania kwafukuta, Absalom Kibanda kupewa likizo ya lazima kupisha uchaguzi Mkuu

Anonymous

Senior Member
Joined
Apr 6, 2006
Posts
118
Reaction score
339
Wakuu,

Mhariri Mtendaji wa gazeti la Mtanzania, Absalom Kibanda, ametakiwa kuenda likizo kwa lazima kwa ajili ya kupisha uchaguzi Mkuu unaotegemewa kufanya Oktoba 25, 2015.

Imebainika kuwa sababu kubwa itakayotolewa na ndugu Kibanda ni kuwa anaenda kwenye matibabu nje ya nchi.

Aidha Mhariri Mwandamizi, Kulwa Karedia, ataenda likizo ya lazima kwa kipindi hicho na nafasi za wawili hao zitachukuliwa na ndugu, Michael Mande amabaye ni kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) aliyegombea kura za maoni za ubunge kwa tiketi ya CCM na kuanguka huko Masasi.

Kwa hali ilivyo sasa, haijulikani ninani yuko nyuma ya hili jambo, ninaendelea kufuatilia sakata hili kwa karibu zaidi, pindi nitakapopata taarifa kamili nitawajulisha.

Itakumbukwa kuwa Kibanda kwa muda mrefu sasa amekuwa mtu wa karibu na Mgombea Urais kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Edward Lowassa, tangu alipotangaza kujiunga na chama hicho.

Asante..

=========
UPDATE:

JamiiForums imeongea na Absalom Kibanda (ambaye pia ni mwanachama wa JamiiForums), amekiri kuna jambo kama hili lakini akasisitiza lipo tofauti na lilivyoandikwa hapo juu. Ataingia JF kufafanua akipata muda lakini kasisitiza kuwa yeye hajalazimishwa kwenda likizo bali kaamua kukaa kando kwa muda.
 
Nadhani hata yeye mwenyewe anaweza kutueleza wazi juu ya uhalisia wa likizo hiyo.
 
wanahangaika sanaaa ila kifo cha CCM Kimewadia na tayari kishatangazwa rasmi mazishi yatakua oktoba 25
 
namkumbuka mh lissu aliwahi sema kila mabadiliko yana wahanga wake,mabadiliko 2015 tanzania wahanga ndio hawa absalom kibanda ila hayaepukiki hata mafisiem wafanye nini
 
Wakuu,

Mhariri Mtendaji wa gazeti la Mtanzania, Absalom Kibanda, ametakiwa kuenda likozo kwa lazima kwa ajili ya kupisha uchaguzi Mkuu unaotegemewa kufanya Oktoba 25, 2015.

Imebainika kuwa sababu kubwa itakayotolewa na ndugu Kibanda ni kuwa anaenda kwenye matibabu nje ya nchi.

Aidha Mhariri Mwandamizi, Kulwa Karedia, ataenda likizo ya lazima kwa kipindi hicho na nafasi za wawili hao zitachukuliwa na ndugu, Michael Mande amabaye ni kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) aliyegombea kura za maoni za ubunge kwa tiketi ya CCM na kuanguka huko Masasi.

Kwa hali ilivyo sasa, haijulikani ninani yuko nyuma ya hili jambo, ninaendelea kufuatilia sakata hili kw akaribu zaidi, pindi nitakapopata taarifa kamili nitawajulisha.

Itakumbukwa kuwa Kibanda kwa muda mrefu sasa amekuwa mtu wa karibu na Mgombea Urais kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Edward Lowassa, tangu alipotangaza kujiunga na chama hicho.


Asante

Tanzania amani asili yetu wenye dhamana ya kulinda sio ya ccm pekee bali sisi wote lakini kwa haya mambo ya kichini chini ni mabaya sana kwa Taifa Letu ila ni mbinu za kizamani wananchi wameamka tayari huwezi kulazimishwa kupendwa CCM imepoteza imani na wananchi na hata tukisema ni utaratibu haiwezi ikawa kwa nyakati kama hizi
 
Bora mngesema yuko neutral mngekuwa na hoja...
Kumbe ni Team Lowasa afu awachwe????
Hata mimi ningemtimua kabisa...nini kumsimamisha.....
 
Bora mngesema yuko neutral mngekuwa na hoja...
Kumbe ni Team Lowasa afu awachwe????
Hata mimi ningemtimua kabisa...nini kumsimamisha.....

Yeye team Lowassa huku owner ni team CCM
kwa hiyo kulikuwepo na struggle waripoti vipi kampeni
both side zilikuwa zinapewa promo ingawa Lowassa zaidi
so now owner wameamua moja kwa moja wawe team CCM
kwa hiyo lazima apewe likizo..hawezi kutimuliwa sababu
hao owner walikuwa team lowassa zamani akiwa ccm...
so wanarudi CCM kwa maslahi tu lakini hawapo CCM kimoyo...
 
Kwahiyo ndio kusema wamepigwa "Sabbatical leave"
kutokana na misimamo yao katika kazi.?
Poor u uliyewasimamisha.
 
Back
Top Bottom