Mtazamo: Kuhusu MCC kusitisha msaada wa MCC 2 na shughuli zake Tanzania

Mtazamo: Kuhusu MCC kusitisha msaada wa MCC 2 na shughuli zake Tanzania

Naishauri serikali iwe strong na isonge mbele najua kisaikojia na kiuchumi vitatusumbua lakin hutuwez anguka,pia serikali iwatazame vizuri wapinzani huwa katika nchi nyingi za kiafrika zilizo ingia migogoro na wahisan chanzo ni hawa watu kwahiyo ubandidu ni muhimu mm nawaona hata humu mitandaoni serikali inatengeza mikakati mahususi wao wanahangaika na wazungu,wazungu hupitia kwa vibaraka ambao kwa sasa ni hawa watu muwaangalie.uroho wa madaraka utafikiriki wakiwa madarakan wanaweza fanya lolote kumbe ni ubinafs umewajaa.
 
Na hivi leo nimemsikia Polepole akiongea chanel ten asubuhi hii na kuniharibia siku.
Eti vyombo vya habari vimemnukuu katibu mkuu wa hazina na kupotosha umma. Na anasema alimpigia na kumuuliza. Pia mabalozi wa nchi 10 wanaodaiwa kuinyima misaada Tanzania yeye kazipigia balozi 2 na kumwambia hawajajitoa. Yeye kageuka kuwa msemaji wa mabalozi? Ni kwanini hao mabalozi wasiitishe press conference wajisemee au kukanusha? Polepole tambua, watanzania wa leo siyo wale wa 2015 uliowageuka na kuanza kuwapopoa mawe ya katiba mpya. Eti wewe mwananchi unayekerwa, utakuwa mwananchi zaidi ya rais wako? Usiutafute ukuu wa wilaya kwenye media na tupunguziane kupotoshana na kujifanya msemaji wa taasisi na balozi.
 
Nianze na nukuu hizi mbili kuntu za Baba wa Taifa Mwalimu Julius K. Nyerere- Mwenyezi Mungu amrehemu.

“Democracy is not a bottle of Coca-Cola which you can import. Democracy should develop according to that particular country”. June 1991 in Rio De Janeiro, Brazil

"Demokrasia sio chupa ya Coca-Cola ambayo unaweza kuagiza. Demokrasia lazima ikue na kuendelezwa kulingana na nchi husika". Juni 1991 Rio De Janeiro, Brazil (Tafsiri ni yangu)

“No nation has the right to make decisions for another nation; no people for another people”. From ‘A Peaceful New Year’ speech, Tanzania, January 1968

"Hakuna Taifa lina haki ya kufanya maamuzi juu ya Taifa lingine; wala watu juu ya watu wengine ". Hotuba ya Amani ya Mwaka Mpya, Tanzania, Januari 1968 (Tafsiri ni yangu)

Hili la Marekani na uamuzi wa MCC ni jambo la mpito na haliwezi kuua mahusiano yetu na Marekani. Tanzania na Marekani zinashirikiana kwa mambo mengi na MCC ni sehemu tu tena ni eneo jipya la ushirikiano. Uamuzi huu ni jaribio kwa uhuru wa Taifa letu. Hakuna namna nyingine ila kushinda hili kama tulivyoshinda mengine huko nyuma. Kwa wale ambao wameuona umri watakumbuka namna tulivunja uhusiano na Ujerumani Magharibi 1964 pale walipotaka kuwa na kauli hasi dhidi ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Tulivunja uhusiano na Ujerumani Magharibi baada ya kutaka kuingilia Uhuru wa Mataifa Mawili huru yaliyoamua kuungana na kuunda Nchi Mpya ambayo leo tunajivunia, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. 1965 Tulivunja uhusiano na Uingereza kufuatia na kitendo cha wazungu wachache kujitangazia Uhuru (Unilateral Declaration of Independence) kule Rhodesia na uingereza kukaa kimya na kushindwa kuchukua hatua stahiki.

Tulivunja Uhusiano na Uingereza kuieleza Dunia kwamba Uhuru wa nchi za Afrika ni kipaumbele muhimu kwa Tanzania. Jambo tunalopaswa kufahamu ni kuwa MCC 2 toka mwanzo imekuwa ni mtihani dhidi ya uhuru wetu. Napenda ieleweke kwamba kipindi hiki kilichotokea sio kuvunjika kwa uhusiano wetu na Marekani bali taasisi ya MCC ndio imesitisha msaada wao kwetu, lakini mahusiano yetu na marekani bado yako pale pale, na si Marekani au Tanzania inayoweza kuugharimu uhusiano wetu.

MCC 1 ilikuwa ni chambo cha kutuvuta na tulipewa bila masharti tena hela nyingi dola milioni 698 na ni fedha tulizopewa moja kwa moja na kupewa uhuru wa kuamua tuzitumieje. Tanzania ilitakiwa kuainisha maeneo kisha wao wanatoa hela. Ndio maana miradi kama ile barabara ambazo hazikuwa zikipata ufadhili kwa kuwa hazikuonekana ni za kiuchumi na miradi ya maji ya Morogoro na kwingineko iliingizwa humu na kupata ufadhili. MCC 2 sio hivyo. Kwenye MCC 2 walengwa wakubwa ni sekta binafsi ya Marekani, hapa kuna mtego hapa, hapa ni biashara hapa.

Mchakato wa MCC 2 ulipoanzishwa, wafanyabiashara kwa kushirikiana na Maseneta wakaanzisha hoja kuwa kwanini Marekani inatoa fedha kwa ufadhili katika nchi ambazo China ndio wenye kufaidika na fedha hizo? Wakaleta hoja ya kuwa Serikali ya Marekani ifanye jitihada ya kuweka fedha kwa kusaidia Sekta Binafsi ya Marekani kupenya Afrika.

Ukaitishwa mkutano wa US-Africa Summit na agenda kubwa ikawa Power Africa. Katika Power Africa, Marekani ikalichagua eneo la Nishati (si uzalishaji viwanda) kwa kutambua kuwa ndio eneo pekee wanaloweza kushindana na wachina. Wakasema wataelekeza fedha huko kuisaidia Afrika kutatua tatizo la nishati ambalo ndio pembejeo ya viwanda. Wakaweka sharti kuwa fedha hizo na miradi hiyo itatekelezwa na Sekta Binafsi ya Marekani.

Ndio sababu wengi wenu mtakumbuka hata Rais Obama alitangazia dhamira ile pale Ubungo kwenye Mitambo ya Symbion Power na sio kwamba alipenda kwenda kutembea Ubungo. Kuanzia hapo kumekuwepo na shinikizo kubwa sana na masharti magumu na yenye kuhamahama (shifting goal post) kutaka kuibaka sekta ya nishati nchini ikiwemo mageuzi ya TANESCO. Zikaainishwa hatua kadhaa,ambazo utekelezaji wake baadhi ni kisheria na kisera na hivyo haziwezi kwenda kwa deadline walizotaka. Kila bodi ikikutana wanaibua hiki na kile lakini wakisema hela watatoa. Hela hizi zikawa zimeshikiliwa kama chambo ukisogelea zinasogea, ni sawa na ule mchoro wa Mpanda Punde aliyeshika fimbo yenye majani na akiielekeza mbele ya punda, kwamba punda ataendelea kuyafuata majani akidhani atayafikia kumbe ndio anaupiga mwendo. Hatimaye wakasema wanasubiri uchaguzi mkuu jambo ambalo halihusiani na madai ya mwanzoni. Baada ya uchaguzi wakaibuka na suala la Zanzibar.

Hivyo, uamuzi wao wa leo ni uamuzi uliotarajiwa. Pia ni uamuzi wenye madhara kwa sekta binafsi ya Marekani pia ambayo ndio ilikuwa itekeleze miradi hiyo. Kama Taifa ni muhimu kulinda utu na uhuru wetu. Ndio msingi wa sera yetu ya nje toka mwanzo na hata sasa. Tumetofautiana na Marekani katika hili tutapatana katika mengine. Ndio uhai wa maisha ya diplomasia.

Wao nao wanayo hadhira ya wapiga kura wao wanayojaribu kuituliza huko nchini kwao kwa uamuzi huu. Tunapaswa kuheshimu uamuzi wao kama ambavyo wanapaswa kuuheshimu wetu. Hatimaye baadae tutapatana. Marekani inaihitaji Tanzania zaidi na Tanzania inaihitaji Marekani. Marekani inahitaji MCC 2 zaidi hali kadhalika Tanzania inahitaji MCC 2.

Mahusiano ya Tanzania na Marekani hayakuanza na hayataisha na MCC. MCC imeyakuta na itayaacha.

Kama marudio ya uchaguzi wa Zanzibar ndio kigezo, basi Marekani isingekuwa inatoa zaidi ya Dola Bilioni 3 kila mwaka kwa Egypt iliyo chini ya utawala wa kijeshi kwa sababu ya kuununua ugomvi wa Egypt na Israel na isingetoa kiasi cha dola bilioni 6 kwa Israel kila mwaka kwa yale wanayoyafanya dhidi ya Wapalestina.

Huu ni wakati ambao Taifa linawaita Wazalendo wake. Wazalendo wasimame na kusema 'Nchi yangu KWANZA, iwe Sahihi au Imekosea" na Makuwadi watashangilia na kusema "si mnaona sasa kiko wapi?".

Huu ni wakati wa kujifunga mikanda na kulinda heshima yetu kama Taifa letu. Tuna vyanzo vya mapato vingi sana ambavyo hatujaanza kukusanya mapato, tuwe wabunifu na tusibweteke na kutegemea mapato yataongezeka maradufu kwa vyanzo vile vile.

Niseme kwa uchache, sababu walizotoa MCC, na ieleweke aliyetoa tamko ni MCC, heri lingetoka tamko hili Wizara ya Mambo ya Nje au Ikulu ya Marekani, moja ni Zanzibar na pili ni Sheria ya Makosa ya Mitandao (Cyber crimes Act).

Sasa hebu tujadili kidogo, hivi kule Zanzibar tulitaka kitokee nini pale ambapo wanasiasa walikuwa hawataki kujadiliana? Tume ile ile ya Uchaguzi ambayo bado ilikuwa na uhalali wa kikatiba na kisheria kuuitisha, kuufuta na kuuitisha tena uchaguzi ikachukua nafasi yake. Wanasiasa wasio makini wakaishia kuhamishia malumbano mitandaoni badala ya kuitafuta suluhu ya kisiasa na pale siasa iliposhindikana basi wangeitafuta suluhu katika mahakama za Zanzibar. Mezani wakashindwa, mahakamani hawakwenda. Tume ikachukua uongozi, uchaguzi ukaitishwa Wananchi wakapiga kura na sasa huko Zanzibar kuna serikali na baraza la wawakilishi. Hata mimi sifurahii sana njia waliyoichukua Zanzibar lakini ilibidi siasa za madaraka zisite ili tuanze kufanya siasa za maendeleo. Je wamarekani walitaka muujiza gani utokee huko.?

Kuhusu Sheria ya Mitandao, hata mimi siipendi, si twende mahakamani, bunge litaanza vikao muda si mrefu je wabunge si wapeleke hoja ya kuifanyia marekebisho sheria hii. Sasa Marekani (MCC) inapoweka shinikizo kwa suala la Sheria ambayo ni jambo la ndani na linaloweza kujadilika, sijaelewa. Mbona sie hatujapiga kelele Yule jamaa yao Trump alipotutusi waafrika na kusema sisi stahili yetu ni kuwekwa tena chini ya ukoloni (hapa nimechomekea tu).

INDHARI

Ni aibu kwa viongozi wa kisiasa kufurahia jambo hili, ni ishara ya ukuwadi wa kisiasa na ambao uko tayari kukumbatia mahusiano yanayotweza Uhuru wetu. It is now high time kufanya siasa safi za maendeleo (politics of development) na sio kujikita katika katika siasa za madaraka (Politics of Power).

Mwandishi, Ndg. Humphrey Polepole amenufaika na uelewa wa watu wenye uzoefu wa mahusiano ya Tanzania na nchi za Nje. Aidha, ni mnufaikaji (alumni) wa programu ya uongozi chini ya Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani.

Unajikanganya. Kama Tz ilipingana na UK kuhusu UDI kule Rhodesia (salsa Zimbabwe) ni sawa na Zanzibar kujitungia katiba yake 2010 halafu kufuta uchaguzi 2015 Wana demokrasia wengine wasiseme kuhusu unafiki wa TZ bara wa kukumbatia ubakaji huu wa demokrasia?
 
Serikali ya ccm itawajuwa watu wa marekani ni kina Nani.

Ujumbe huu umeletwa kwa hisani ya watu wa Tanzania.
 
Ahsante kwa andiko hili kuntu bwana polepole. Mimi nakukubaligi wewe polepole ingawa wengine hawakukubali.
Wewe ni mfano wa mzalendo kamili.
viva polepole
Sikushangai, ni kawaida yetu kushabikia tune ya mwimbo ulioimbwa kwa lugha usioielewa.
Humphrey Polepole ana tumbo kama alivyo mwanadamu yeyote. Hili za sizitaki mbichi hizi ndio la kumfanya aandike maandishi meeengi namna hii jukwaani?
Mbona haya hayakusemwa awali wakati tukipokea fedha? Leo hii Wachina wanasema uchaguzi wa Zanzibar safi, hutasikia kauli yao ikijadiliwa na Polepole sbb imeenda alongside na ahadi ya kuendelea kuisaidia Tanzania.

My friend, siasa ni siasa, hakuna Marekani wala China, tusichopaswa kufanya ni kuwa wanafiki.

Critics wa kweli hawamchagui wa kumkosoa.
 
Sikushangai, ni kawaida yetu kushabikia tune ya mwimbo ulioimbwa kwa lugha usioielewa.
Humphrey Polepole ana tumbo kama alivyo mwanadamu yeyote. Hili za sizitaki mbichi hizi ndio la kumfanya aandike maandishi meeengi namna hii jukwaani?
Mbona haya hayakusemwa awali wakati tukipokea fedha? Leo hii Wachina wanasema uchaguzi wa Zanzibar safi, hutasikia kauli yao ikijadiliwa na Polepole sbb imeenda alongside na ahadi ya kuendelea kuisaidia Tanzania.

My friend, siasa ni siasa, hakuna Marekani wala China, tusichopaswa kufanya ni kuwa wanafiki.

Critics wa kweli hawamchagui wa kumkosoa.
Sikushangai, ni kawaida yetu kushabikia tune ya mwimbo ulioimbwa kwa lugha usioielewa.
Humphrey Polepole ana tumbo kama alivyo mwanadamu yeyote. Hili za sizitaki mbichi hizi ndio la kumfanya aandike maandishi meeengi namna hii jukwaani?
Mbona haya hayakusemwa awali wakati tukipokea fedha? Leo hii Wachina wanasema uchaguzi wa Zanzibar safi, hutasikia kauli yao ikijadiliwa na Polepole sbb imeenda alongside na ahadi ya kuendelea kuisaidia Tanzania.

My friend, siasa ni siasa, hakuna Marekani wala China, tusichopaswa kufanya ni kuwa wanafiki.

Critics wa kweli hawamchagui wa kumkosoa.
Hivi China ilishawahi kufanya uchaguzi? Maana ukisifiwa na kichaa umependeza inabidi ujitafakari, leo hii North Korea waisifie Tanzania kwa demokrasia inahitaji akili ya maiti au ya Jecha kuwaelewa.
 
Bravo Bw. polepole kwa ufafanuzi wako murua! MCC kazi yao ni kuhamisha goli. Wakati Mh. Kafulila anashupalia suala la MCC katika Bunge lililopita sababu ya kuzuia kutopewa fedha zile zilikuwa tofauti kabisa na hizi za sasa. Kipindi kile suala la uchaguzi wa Zanzibar lilikuwa halipo na sheria ya mtandao nafikiri ilikuwa bado haijapitishwa! Hawa jamaa ni wasanii wa kutupwa! Walisita kutoa pesa za mradi wa umeme wa Malagarasi eti utafiti umeonyesha kuwa kuna samaki adimu katika mto huo (Kambare) ambao hawatakiwi kubugudhiwa!
Polepole kila kitu ni expert. Makala yako hai-reflect kilichotukosesha package ile.
 
Kama huhitaji msaada wa wamarekani, na kama unaona haina tija kwa nchi kwa nini useme mcc haitaondoa uhusiano wetu uliopo kati yetu na marekani? kama wanatuingilia na hatuwahitaji sema moja kwa moja hata wamarekani wakivunja uhusiano wetu haina tatizo, sio kupiga miguu wakati unataka kutembea.
 
what the hell..Kwani ninyi na mmarekani nani anamuhitaji mwingine zaidi?

CCM itaendelea kuigharimu nchi hii...tena sana

Huu ni mwanzo tu....

Ila namshukuru Mungu kwa sababu mwisho wa siku utawala huu ndio utakaowaonyesha watanzania kuwa CCM haifai......ni kiini cha matatizo ya nchi hii......

Muda ni judge mzuri sana
 
Naelewa spirit ya watu wanaotamani nchi yetu ijitegemee lakini nachelea kusema ni uwandawazimu kudhani spirit pekee inaweza kuondoa ukweli kwamba pamoja na juhudi zote za serikali ya awamu ya tano kuminya mianya ya ukwepaji wa kodi bado ni tegemezi iwe ni kwa nchi za magharibi au japan na uchina there is no lesser evil wote wapo kwenye kulinda maslahi yao lakini swala la kua na demokrasia ya kweli nadhani ni la maslahi makubwa ya watanzania kuliko ilivyo kwao hivyo hatuwezi kusema kilio cha wazanzibar kuhusu uchaguzi wa mwezi October kilichagizwa na nchi wahisani kila mtanzania asiyesukumwa na unazi wa uchama " he was smelling something fishy" kuhusu uamuzi wa jecha. Nadhani bwana polepole hizo nukuu za mwl. nyerere hazisadii kujenga hoja yako bali zinazidi kuidhoofisha naamini tasfiri sahihi ya nchi kuamua mambo yake si watawala bali wananchi hivyo naamini kama ilivyo batili marekani au nchi nyingine kuingilia mambo yetu ya ndani (yaliyoamuliwa na wananchi) ni kwa kiasi hichohicho (labda zaidi) sio sahihi kwa kikundi kidogo cha watu wanajiita watawala au chama cha siasa kudhani wanaweza kuamua jambo zito kinyume na matakwa ya wananchi na pale zinapokuja athari kubwa kwa nchi nzima kudhani they will win public sympathy kwa kujificha kwenye kichaka cha uzalendo!
 
Ahsante kwa andiko hili kuntu bwana polepole. Mimi nakukubaligi wewe polepole ingawa wengine hawakukubali.
Wewe ni mfano wa mzalendo kamili.
viva polepole
Kama unamkubali huyo Polepole ucpate tabu katoe Posa umpeleke kwako chama chao kishazoea mombasa hana shida kijana

Sent from my TECNO M6 using JamiiForums mobile app
 
Tuweni tu wakweli, wana ccm mlio wengi kwenu nyie chama chenu ni muhimu zaidi kuliko Tanzania. Mpo tayari kuona Tanzania inaangamia lakini sio ccm; tukubali tukatae, iwe ndio sababu ya kukosa pesa au isiwe sababu, Zanzibar ccm imecheza faulo. Tukumbuke maneno ya Nape Nnauye aliposema hata kwa GOLI la MKONO ccm itashinda. Leo eti Polepole unasema watu waende mahakamani au bungeni kubadiri sharia? Kweli? Tanzania hi hi au nyingine? Kwani wewe umaarufu wako ulianzia wapi kama sio kwenye tume ya KATIBA? Bunge la katiba kwa kupitia jingo hilo hilo ndio walikufanya wewe na kina mzee Warioba either kua maarufu au kukutweza, halafu wewe huyo unashauri eti BUNGE lijadiri sharia lililotunga lenyewe; wonders shall never end! Hivi nani asiyejua kua sharia inasema kilicho tangazwa na tume hakuna mahakama yoyote yenye uwezo wa kutangua?
Napendekeza hivi; kama mnavyo tutaka tuanze kua wazalendo kwenye nchi yetu, na nyie ccm ondoeni mawazo haya, "ccm ndio Tanzania na Tanzania ndio ccm" oneni kwamba Tanzania inao uwezo wa kuendelea hata zaidi sana bila uwepo wa ccm, ccm inaihitaji sana Tanzania lakini Tanzania haina uhitaji wa kitu kinacho itwa ccm. Tukifika hapo wala hivi viji mawazo vya kutwambia tuwe wazalendo havitakua na sababu yoyote.
 
Kwanza naomba nitangulie kwa kusema kwamba ni ujinga uliotopea kuamini kwamba kila anayelaumu au kwenda tofauti na dhana hii ya MCC basi ni mwanaccm.

Hoja yangu ni kwamba nani anaeweza kuleta ushahidi wa moja kwa moja kwamba CCM imevuruga matokeo au CCM imejitwalia madaraka kwa nguvu?

Kati ya CCM ya Shein na CUF ya Seif nani aliyekiuka kanuni za uchaguzi wakati wa uchaguzi October 25 mwaka jana?

CCM ya Shein na CUF ya Seif ni ipi iliokimbia meza ya mazungumzo?
CCM chini ya M/kiti Dr. Jakaya imesikitishwa na kufutwa uchaguzi Zanzibar, maneno haya ameyatamka siku ya maadhimisho ya chama pale singida.

Kwa nini akina Msigwa hawajadili zile sababu 8 zilizopelekea kufutwa uchaguzi Zanzibar na badala yake wanaimbisha kasuku wimbo wa CCM?

Na kama Cyber crime hilo suala limepitia bungeni pamoja na sheria ya Takwimu, sasa yeye na wenzie walitakiwa waifanye hiyo kazi wakiwa bungeni lawama haisaidii.
 
Naishauri serikali iwe strong na isonge mbele najua kisaikojia na kiuchumi vitatusumbua lakin hutuwez anguka,pia serikali iwatazame vizuri wapinzani huwa katika nchi nyingi za kiafrika zilizo ingia migogoro na wahisan chanzo ni hawa watu kwahiyo ubandidu ni muhimu mm nawaona hata humu mitandaoni serikali inatengeza mikakati mahususi wao wanahangaika na wazungu,wazungu hupitia kwa vibaraka ambao kwa sasa ni hawa watu muwaangalie.uroho wa madaraka utafikiriki wakiwa madarakan wanaweza fanya lolote kumbe ni ubinafs umewajaa.
Tanzania tuliona mbali, heri Trump kaja.
 
Nianze na nukuu hizi mbili kuntu za Baba wa Taifa Mwalimu Julius K. Nyerere- Mwenyezi Mungu amrehemu.

“Democracy is not a bottle of Coca-Cola which you can import. Democracy should develop according to that particular country”. June 1991 in Rio De Janeiro, Brazil

"Demokrasia sio chupa ya Coca-Cola ambayo unaweza kuagiza. Demokrasia lazima ikue na kuendelezwa kulingana na nchi husika". Juni 1991 Rio De Janeiro, Brazil (Tafsiri ni yangu)

“No nation has the right to make decisions for another nation; no people for another people”. From ‘A Peaceful New Year’ speech, Tanzania, January 1968

"Hakuna Taifa lina haki ya kufanya maamuzi juu ya Taifa lingine; wala watu juu ya watu wengine ". Hotuba ya Amani ya Mwaka Mpya, Tanzania, Januari 1968 (Tafsiri ni yangu)

Hili la Marekani na uamuzi wa MCC ni jambo la mpito na haliwezi kuua mahusiano yetu na Marekani. Tanzania na Marekani zinashirikiana kwa mambo mengi na MCC ni sehemu tu tena ni eneo jipya la ushirikiano. Uamuzi huu ni jaribio kwa uhuru wa Taifa letu. Hakuna namna nyingine ila kushinda hili kama tulivyoshinda mengine huko nyuma. Kwa wale ambao wameuona umri watakumbuka namna tulivunja uhusiano na Ujerumani Magharibi 1964 pale walipotaka kuwa na kauli hasi dhidi ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Tulivunja uhusiano na Ujerumani Magharibi baada ya kutaka kuingilia Uhuru wa Mataifa Mawili huru yaliyoamua kuungana na kuunda Nchi Mpya ambayo leo tunajivunia, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. 1965 Tulivunja uhusiano na Uingereza kufuatia na kitendo cha wazungu wachache kujitangazia Uhuru (Unilateral Declaration of Independence) kule Rhodesia na uingereza kukaa kimya na kushindwa kuchukua hatua stahiki.

Tulivunja Uhusiano na Uingereza kuieleza Dunia kwamba Uhuru wa nchi za Afrika ni kipaumbele muhimu kwa Tanzania. Jambo tunalopaswa kufahamu ni kuwa MCC 2 toka mwanzo imekuwa ni mtihani dhidi ya uhuru wetu. Napenda ieleweke kwamba kipindi hiki kilichotokea sio kuvunjika kwa uhusiano wetu na Marekani bali taasisi ya MCC ndio imesitisha msaada wao kwetu, lakini mahusiano yetu na marekani bado yako pale pale, na si Marekani au Tanzania inayoweza kuugharimu uhusiano wetu.

MCC 1 ilikuwa ni chambo cha kutuvuta na tulipewa bila masharti tena hela nyingi dola milioni 698 na ni fedha tulizopewa moja kwa moja na kupewa uhuru wa kuamua tuzitumieje. Tanzania ilitakiwa kuainisha maeneo kisha wao wanatoa hela. Ndio maana miradi kama ile barabara ambazo hazikuwa zikipata ufadhili kwa kuwa hazikuonekana ni za kiuchumi na miradi ya maji ya Morogoro na kwingineko iliingizwa humu na kupata ufadhili. MCC 2 sio hivyo. Kwenye MCC 2 walengwa wakubwa ni sekta binafsi ya Marekani, hapa kuna mtego hapa, hapa ni biashara hapa.

Mchakato wa MCC 2 ulipoanzishwa, wafanyabiashara kwa kushirikiana na Maseneta wakaanzisha hoja kuwa kwanini Marekani inatoa fedha kwa ufadhili katika nchi ambazo China ndio wenye kufaidika na fedha hizo? Wakaleta hoja ya kuwa Serikali ya Marekani ifanye jitihada ya kuweka fedha kwa kusaidia Sekta Binafsi ya Marekani kupenya Afrika.

Ukaitishwa mkutano wa US-Africa Summit na agenda kubwa ikawa Power Africa. Katika Power Africa, Marekani ikalichagua eneo la Nishati (si uzalishaji viwanda) kwa kutambua kuwa ndio eneo pekee wanaloweza kushindana na wachina. Wakasema wataelekeza fedha huko kuisaidia Afrika kutatua tatizo la nishati ambalo ndio pembejeo ya viwanda. Wakaweka sharti kuwa fedha hizo na miradi hiyo itatekelezwa na Sekta Binafsi ya Marekani.

Ndio sababu wengi wenu mtakumbuka hata Rais Obama alitangazia dhamira ile pale Ubungo kwenye Mitambo ya Symbion Power na sio kwamba alipenda kwenda kutembea Ubungo. Kuanzia hapo kumekuwepo na shinikizo kubwa sana na masharti magumu na yenye kuhamahama (shifting goal post) kutaka kuibaka sekta ya nishati nchini ikiwemo mageuzi ya TANESCO. Zikaainishwa hatua kadhaa,ambazo utekelezaji wake baadhi ni kisheria na kisera na hivyo haziwezi kwenda kwa deadline walizotaka. Kila bodi ikikutana wanaibua hiki na kile lakini wakisema hela watatoa. Hela hizi zikawa zimeshikiliwa kama chambo ukisogelea zinasogea, ni sawa na ule mchoro wa Mpanda Punde aliyeshika fimbo yenye majani na akiielekeza mbele ya punda, kwamba punda ataendelea kuyafuata majani akidhani atayafikia kumbe ndio anaupiga mwendo. Hatimaye wakasema wanasubiri uchaguzi mkuu jambo ambalo halihusiani na madai ya mwanzoni. Baada ya uchaguzi wakaibuka na suala la Zanzibar.

Hivyo, uamuzi wao wa leo ni uamuzi uliotarajiwa. Pia ni uamuzi wenye madhara kwa sekta binafsi ya Marekani pia ambayo ndio ilikuwa itekeleze miradi hiyo. Kama Taifa ni muhimu kulinda utu na uhuru wetu. Ndio msingi wa sera yetu ya nje toka mwanzo na hata sasa. Tumetofautiana na Marekani katika hili tutapatana katika mengine. Ndio uhai wa maisha ya diplomasia.

Wao nao wanayo hadhira ya wapiga kura wao wanayojaribu kuituliza huko nchini kwao kwa uamuzi huu. Tunapaswa kuheshimu uamuzi wao kama ambavyo wanapaswa kuuheshimu wetu. Hatimaye baadae tutapatana. Marekani inaihitaji Tanzania zaidi na Tanzania inaihitaji Marekani. Marekani inahitaji MCC 2 zaidi hali kadhalika Tanzania inahitaji MCC 2.

Mahusiano ya Tanzania na Marekani hayakuanza na hayataisha na MCC. MCC imeyakuta na itayaacha.

Kama marudio ya uchaguzi wa Zanzibar ndio kigezo, basi Marekani isingekuwa inatoa zaidi ya Dola Bilioni 3 kila mwaka kwa Egypt iliyo chini ya utawala wa kijeshi kwa sababu ya kuununua ugomvi wa Egypt na Israel na isingetoa kiasi cha dola bilioni 6 kwa Israel kila mwaka kwa yale wanayoyafanya dhidi ya Wapalestina.

Huu ni wakati ambao Taifa linawaita Wazalendo wake. Wazalendo wasimame na kusema 'Nchi yangu KWANZA, iwe Sahihi au Imekosea" na Makuwadi watashangilia na kusema "si mnaona sasa kiko wapi?".

Huu ni wakati wa kujifunga mikanda na kulinda heshima yetu kama Taifa letu. Tuna vyanzo vya mapato vingi sana ambavyo hatujaanza kukusanya mapato, tuwe wabunifu na tusibweteke na kutegemea mapato yataongezeka maradufu kwa vyanzo vile vile.

Niseme kwa uchache, sababu walizotoa MCC, na ieleweke aliyetoa tamko ni MCC, heri lingetoka tamko hili Wizara ya Mambo ya Nje au Ikulu ya Marekani, moja ni Zanzibar na pili ni Sheria ya Makosa ya Mitandao (Cyber crimes Act).

Sasa hebu tujadili kidogo, hivi kule Zanzibar tulitaka kitokee nini pale ambapo wanasiasa walikuwa hawataki kujadiliana? Tume ile ile ya Uchaguzi ambayo bado ilikuwa na uhalali wa kikatiba na kisheria kuuitisha, kuufuta na kuuitisha tena uchaguzi ikachukua nafasi yake. Wanasiasa wasio makini wakaishia kuhamishia malumbano mitandaoni badala ya kuitafuta suluhu ya kisiasa na pale siasa iliposhindikana basi wangeitafuta suluhu katika mahakama za Zanzibar. Mezani wakashindwa, mahakamani hawakwenda. Tume ikachukua uongozi, uchaguzi ukaitishwa Wananchi wakapiga kura na sasa huko Zanzibar kuna serikali na baraza la wawakilishi. Hata mimi sifurahii sana njia waliyoichukua Zanzibar lakini ilibidi siasa za madaraka zisite ili tuanze kufanya siasa za maendeleo. Je wamarekani walitaka muujiza gani utokee huko.?

Kuhusu Sheria ya Mitandao, hata mimi siipendi, si twende mahakamani, bunge litaanza vikao muda si mrefu je wabunge si wapeleke hoja ya kuifanyia marekebisho sheria hii. Sasa Marekani (MCC) inapoweka shinikizo kwa suala la Sheria ambayo ni jambo la ndani na linaloweza kujadilika, sijaelewa. Mbona sie hatujapiga kelele Yule jamaa yao Trump alipotutusi waafrika na kusema sisi stahili yetu ni kuwekwa tena chini ya ukoloni (hapa nimechomekea tu).

INDHARI

Ni aibu kwa viongozi wa kisiasa kufurahia jambo hili, ni ishara ya ukuwadi wa kisiasa na ambao uko tayari kukumbatia mahusiano yanayotweza Uhuru wetu. It is now high time kufanya siasa safi za maendeleo (politics of development) na sio kujikita katika katika siasa za madaraka (Politics of Power).

Mwandishi, Ndg. Humphrey Polepole amenufaika na uelewa wa watu wenye uzoefu wa mahusiano ya Tanzania na nchi za Nje. Aidha, ni mnufaikaji (alumni) wa programu ya uongozi chini ya Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani.
Pole Pole mbona huandiki tena maandiko kama haya??
 
Back
Top Bottom