MTAZAMO: Mwanadamu hakuumbwa na Mungu.

MTAZAMO: Mwanadamu hakuumbwa na Mungu.

Ryan The King

JF-Expert Member
Joined
Oct 6, 2016
Posts
2,788
Reaction score
2,690
Habarini!

Moja ya mambo ambayo ni telezi basi bila Shaka ni asili ya binadamu. Zipo nadharia nyingi kama mchanga wa bahari zinazoelezea asili ya kiumbe huyu ambaye ni mtawala wa hii dunia.

Moja ya nadharia kuhusu asili ya binadamu ni pamoja na nadharia ya kidini/kiimani ambayo imegawanyika katika makundi mbalimbali.
Wapo wanaodai mwanadamu aliumbwa na Mungu. Wapo pia wanaosema mwanadamu hakuumbwa na Mungu Bali ni matokeo ya Mabadiliko ya kikemikali yaliyochukua miaka zaidi ya bilioni moja iliyopitia.

Hakuna mwenye ushahidi hilo ndilo linafanya kila kundi kujiamini katika upande wake.

MTAZAMO WANGU.

Bila Shaka mwanadamu hakutokea katika ombwe Bali ni matokeo ya akili Fulani iliyojuu yake maradufu.
Huenda mwanadamu hakuumbwa na Mungu kama watu wanavyodhani. Hii pia ni nadharia.

Wazo hili linaibuka katika akili yangu kutokana maandiko ya Bibilia na QUruan.

Katika kitabu cha Mwanza moja. Kinasema Natuumbe mtu Kwa mfano wetu wakatawale samaki wa baharini, wanyama na ndege wa angani.

Kauli hiyo inadhihirisha moja Kwa moja aliyekuwa akiongea alikuwa Mungu ambaye hakuwa peke Yale bali alikuwa na jopo la wahusika ambao hawakutajwa.

Kauli hii ni fikirishi mno. Hii ni kutokana na muandishi wa kitabu hicho kushindwa kudokeza wahusika waliokuwa na Mungu katika Uumbaji.

Kwa mtazamo wangu; naona mwanadamu aliumbwa na moja ya viumbe wakubwa wenye mamlaka za juu. Na kuumbwa kwake ni kutokana na amri ya mwenyezi Mungu. Na huyu/ hawa waliomuumba Mwanadamu walikuwa moja wa Malaika au mfano wa Malaika.

Sikatai Mwanadamu hafanani Kwa chochote na Mungu bali hufanana na wale viumbe waliomuumba Kwa mfano wao yaani moja wa Malaika wakubwa wenye uwezo.

Kwa nini Mwanadamu aliumbwa?

Kwa mtazamo wangu;
Kuumbwa Kwa mwanadamu ni matokeo ya muendelezo wa mamlaka ya Mungu katika jeshi lake lote la angani. Ikumbukwe dunia ni moja ya jeshi la angani.

Zipo nyota mabilioni Kwa mabilioni. Hivyo katika kila nyota na sayari zake yupo kiumbe na mamlaka inayoongoza nyota hiyo. Katika kurahisisha mamlaka huenda Malaika huyo mwenye uweza mkubwa aliopewa na Mungu ndipo alipomuumba mwanadamu Kwa ajili ya kutawala dunia.

Hivyo mwanadamu aliumbwa Kwa ajili ya kuitawala dunia yaani kuwa muwakilishi wa Mungu japokuwa hafanani na Mungu hata chembe.

Kama vile Wanadamu walivyo na akili na maarifa ya kutengeneza vyombo kama ndege, magari, simu n.k Kwa ajili ya kuwarahisishia mambo yao ndivyo na wao walivyotengenezwa/ kuumbwa kwaajili ya kuweza kurahisisha mambo katika mamlaka za rohoni ambazo ndio hao malaika wakubwa. Ikumbukwe pia kama ilivyo Kwa binadamu kuwa si wote wenye maarifa ya kuunda vitu vya kisayansi halikadhalika si Malaika wote wenye uwezo wa kumuumba mwanadamu.

Mwanadamu ni akili Fulani ambayo ilibuniwa na Malaika Fulani wakubwa ambao walipewa akili na mwenyezi Mungu. Na Mungu ndiye aliyetoa ruhusa ya Mwanadamu kuumbwa japo huenda hakuhusika moja Kwa moja.

Kama mwanadamu angeumbwa na Mungu moja Kwa moja basi angekuwa mkamilifu asilimia Mia moja. Asingekuwa na mapungufu kama aliyonayo sasa. Ndio maana kuna wazo huwa linakujaga akilini mwangu kuwa huenda mwanadamu si kazi ya mikono ya Mungu.

Karibuni
 
FB_IMG_14666933460283298.jpg
 
Binadamu ali evolve, miaka takriban milioni 4 iliyo pita baada ya Apes kuanza kutembea kwa miguu miwili
 
umejiuliza swali sahihi mkuu ni sawa
lakini cornerstone ya point yako umeeleza Mungu alisema natuumbe mtu kwa mfano wetu
kwa uelewa wa maandiko Mungu aliposema natuumbe haimaniishi kwamba hakuwa peke yake
neno tuumbe=sisi laweza kutumika kuonyesha nguvu na mamlaka ya mtu japokuwa ni mmoja
kwa hiyo hata raisi anaweza kusema tunamfuta kazi bashite sababu ana vyeti feki
yawezekana yeye ndo kamfuta kazi lakini anaposema sisi tunamfuta ana maana ya mamlaka yake alonayo katika serikali
kwa hiyo Mungu aliposema tunaumba haimaanishi kuwa waumbaji walikuwa wengi
 
Haya yote ni kujaribu kujustify makosa yetu wanadamu na kujipa moyo hakuna judgement day. Mimi japo si mchamungu ninaamini Mungu yupo na atatuhukumu...haiwezekani wengine wafanye mabaya juu ya wengine ikapita hivihivi. Mola aliye mkuu yupo na atahukumu hukmu yenye haki kwa viumbe wake wote. Hakuna ujanjaujanja katika hilo. Na haya ya kumzushia na kukana kazi na uwepo wa Mungu yamekuja baada ya mwanadamu kujiona ameweza kufanya mengi katika uso wa dunia.
 
Habarini!

Moja ya mambo ambayo ni telezi basi bila Shaka ni asili ya binadamu. Zipo nadharia nyingi kama mchanga wa bahari zinazoelezea asili ya kiumbe huyu ambaye ni mtawala wa hii dunia.

Moja ya nadharia kuhusu asili ya binadamu ni pamoja na nadharia ya kidini/kiimani ambayo imegawanyika katika makundi mbalimbali.
Wapo wanaodai mwanadamu aliumbwa na Mungu. Wapo pia wanaosema mwanadamu hakuumbwa na Mungu Bali ni matokeo ya Mabadiliko ya kikemikali yaliyochukua miaka zaidi ya bilioni moja iliyopitia.

Hakuna mwenye ushahidi hilo ndilo linafanya kila kundi kujiamini katika upande wake.

MTAZAMO WANGU.

Bila Shaka mwanadamu hakutokea katika ombwe Bali ni matokeo ya akili Fulani iliyojuu yake maradufu.
Huenda mwanadamu hakuumbwa na Mungu kama watu wanavyodhani. Hii pia ni nadharia.

Wazo hili linaibuka katika akili yangu kutokana maandiko ya Bibilia na QUruan.

Katika kitabu cha Mwanza moja. Kinasema Natuumbe mtu Kwa mfano wetu wakatawale samaki wa baharini, wanyama na ndege wa angani.

Kauli hiyo inadhihirisha moja Kwa moja aliyekuwa akiongea alikuwa Mungu ambaye hakuwa peke Yale bali alikuwa na jopo la wahusika ambao hawakutajwa.

Kauli hii ni fikirishi mno. Hii ni kutokana na muandishi wa kitabu hicho kushindwa kudokeza wahusika waliokuwa na Mungu katika Uumbaji.

Kwa mtazamo wangu; naona mwanadamu aliumbwa na moja ya viumbe wakubwa wenye mamlaka za juu. Na kuumbwa kwake ni kutokana na amri ya mwenyezi Mungu. Na huyu/ hawa waliomuumba Mwanadamu walikuwa moja wa Malaika au mfano wa Malaika.

Sikatai Mwanadamu hafanani Kwa chochote na Mungu bali hufanana na wale viumbe waliomuumba Kwa mfano wao yaani moja wa Malaika wakubwa wenye uwezo.

Kwa nini Mwanadamu aliumbwa?

Kwa mtazamo wangu;
Kuumbwa Kwa mwanadamu ni matokeo ya muendelezo wa mamlaka ya Mungu katika jeshi lake lote la angani. Ikumbukwe dunia ni moja ya jeshi la angani.

Zipo nyota mabilioni Kwa mabilioni. Hivyo katika kila nyota na sayari zake yupo kiumbe na mamlaka inayoongoza nyota hiyo. Katika kurahisisha mamlaka huenda Malaika huyo mwenye uweza mkubwa aliopewa na Mungu ndipo alipomuumba mwanadamu Kwa ajili ya kutawala dunia.

Hivyo mwanadamu aliumbwa Kwa ajili ya kuitawala dunia yaani kuwa muwakilishi wa Mungu japokuwa hafanani na Mungu hata chembe.

Kama vile Wanadamu walivyo na akili na maarifa ya kutengeneza vyombo kama ndege, magari, simu n.k Kwa ajili ya kuwarahisishia mambo yao ndivyo na wao walivyotengenezwa/ kuumbwa kwaajili ya kuweza kurahisisha mambo katika mamlaka za rohoni ambazo ndio hao malaika wakubwa. Ikumbukwe pia kama ilivyo Kwa binadamu kuwa si wote wenye maarifa ya kuunda vitu vya kisayansi halikadhalika si Malaika wote wenye uwezo wa kumuumba mwanadamu.

Mwanadamu ni akili Fulani ambayo ilibuniwa na Malaika Fulani wakubwa ambao walipewa akili na mwenyezi Mungu. Na Mungu ndiye aliyetoa ruhusa ya Mwanadamu kuumbwa japo huenda hakuhusika moja Kwa moja.

Kama mwanadamu angeumbwa na Mungu moja Kwa moja basi angekuwa mkamilifu asilimia Mia moja. Asingekuwa na mapungufu kama aliyonayo sasa. Ndio maana kuna wazo huwa linakujaga akilini mwangu kuwa huenda mwanadamu si kazi ya mikono ya Mungu.

Karibuni
017eb7dbf0e238cceb866b53a5177804.jpg

43e2ef7adf127958031e26f6bc726241.jpg

ca2bea79c4424c6cf157894912414148.jpg
 
umejiuliza swali sahihi mkuu ni sawa
lakini cornerstone ya point yako umeeleza Mungu alisema natuumbe mtu kwa mfano wetu
kwa uelewa wa maandiko Mungu aliposema natuumbe haimaniishi kwamba hakuwa peke yake
neno tuumbe=sisi laweza kutumika kuonyesha nguvu na mamlaka ya mtu japokuwa ni mmoja
kwa hiyo hata raisi anaweza kusema tunamfuta kazi bashite sababu ana vyeti feki
yawezekana yeye ndo kamfuta kazi lakini anaposema sisi tunamfuta ana maana ya mamlaka yake alonayo katika serikali
kwa hiyo Mungu aliposema tunaumba haimaanishi kuwa waumbaji walikuwa wengi
Umeongea vyema mkuu.
Lakini hoja yangu inasimama kutokana na istilahi "Kwa mfano wetu" kumaanisha kufanana baina ya mtu na huyo anayemuumba japo sio Kwa 100%.

Wakati huo huo Mungu angasema hafananishwi na chochote na ni kweli.

Huoni kuna utata katika kauli hizo.

Mi naona kuwa kama mwanadamu angeumbwa na Mungu huenda angekuwa Mkamilifu Kwa 100%.

Mwanadamu yeye Kwa utashi wake naye akatengeneza vitu kama Marobot, magari n.k. ambayo nayo yanamapungufu.
 
Haya yote ni kujaribu kujustify makosa yetu wanadamu na kujipa moyo hakuna judgement day. Mimi japo si mchamungu ninaamini Mungu yupo na atatuhukumu...haiwezekani wengine wafanye mabaya juu ya wengine ikapita hivihivi. Mola aliye mkuu yupo na atahukumu hukmu yenye haki kwa viumbe wake wote. Hakuna ujanjaujanja katika hilo. Na haya ya kumzushia na kukana kazi na uwepo wa Mungu yamekuja baada ya mwanadamu kujiona ameweza kufanya mengi katika uso wa dunia.

Hutakuja kumuona Mungu Mkuu hata ufufuke. Mungu haonekani mkuu.
Hivyo hata atakayepewa Mamlaka ya kuhukumu ni mwingine lakini hutokuja kumuona Mungu. Ndio maana dai la Yesu ni Mungu huweza kupata Mashiko zaidi. Japo na yeye sio Mungu bali amepewa Mamlaka na Mungu
 
Ahsante Kwa Kutupa Aya.

Hata Mimi naamini kila kitu kiliumbwa Kwa amri ya mwenyezi Mungu. Lakini kuna vilivyoumbwa na viumbe wenye akili na utashi mkubwa walioumbwa na Mungu. Ni kama vile binadamu anavyounda gari na Marobot lakini anatumia akili aliyoikuta.

Huenda binadamu naye aliumbwa hivyo hivyo
 
Unapokuwa hai ndipo unapoandaa maisha utakayoishi baada ya kifo.
Sasa subiria Ukifa ndipo utayajua haya uyasemayo na nadharia zote utazikuta huko.
 
Back
Top Bottom