Mtazamo: Polisi Tanzania hawana weledi wa kufanya Uchunguzi wa eneo la tukio la uhalifu (Crime Scene)

Mtazamo: Polisi Tanzania hawana weledi wa kufanya Uchunguzi wa eneo la tukio la uhalifu (Crime Scene)

DidYouKnow

JF-Expert Member
Joined
Jul 28, 2019
Posts
1,229
Reaction score
1,950
Nikiri kwamba andiko hili limepata nguvu kutokana na mauaji yaliyofanyika katika Bar ya Lemax, Sinza, kama yalivyoletwa na Tusker Bariiiidi. Kupitia taarifa ya ITV, ukichunguza kwa umakini utagundua kuna mhanga wa hili tukio, mwili wake umelala kwenye kiti, ingawa polisi wapo wakirandaranda kila kona, hakuna tukio lolote kubwa linalofanyika la kiuchunguzi zaidi ya kuchukua maelezo ya mashahidi na (labda kupiga picha), na hatimaye wataondoka na miili ya marehemu.

Video iko hapa


Hii imekuwa ni kama kawaida ya jeshi la Polisi Tanzania inapofanya uchunguzi wa kifo. Tukio kubwa wanalokuja kulifanya ni kubeba miili ya marehemu tu. Huwa hawako serious. Ndio maana baadhi ya kesi huwasumbua sana mahakamani wakikutana na wakili mzuri kwani baadhi ya evidence wanakuwa waliziacha kwenye eneo la tukio la uhalifu (crime scene).

Ukiangalia namna Polisi Tanzania wanavyo treat crime scene utajua hawana mafunzo ya kutosha ya kufanya uchunguzi wa makosa ya jinai. Na kama kuna mafunzo wanayapata huko vyuoni kwao, basi ni bora hayo mafunzo yafutwe tu kwani hayana tija. Polisi Tanzania wanapofanya uchunguzi wa matukio ya kihalifu, wanafanana na kijana wa mtaani anayetafuta mgoni wake, lakini tofauti ni kwamba wao Polisi wana access ya kupata taarifa maeneo mengi kama TCRA, NIDA, Bank na sehemu nyingine ambazo raia wa kawaida hana.

Ukiangalia video za matukio yote ya mauaji hapa Tanzania utashangaa kuna uchunguzi gani unafanyika zaidi ya wao kwenda kwa spidi kukusanya mwili au miili ya wahanga.

Hakuna video ambayo waweza ona hata kamba tu ya kutenga eneo la tukio la mauaji ili kutolichafua imewekwa. Huoni hata alama za utambulisho (identification markers) kama stendi za plastiki zenye namba, au bendera inayoonesha alama za ushahidi katika eneo la tukio la uhalifu. Polisi naamini wanajua kwamba vitu vidogo kama hizo identification markers husaidia kufunua, kurahisisha, kupanga na kubaini vitu vingi vya ushahidi unaopatikana kwenye eneo la matukio la uhalifu. Inapotumiwa vizuri inawaruhusu hata wengine kuelewa kwa urahisi tukio zima.

Wito kwa Polisi Tanzania na Vyuo Vikuu vya Tanzania, kujenga ushirikiano na vyuo vikuu vya kigeni ili kuanzisha kozi ambazo mwisho wa siku zitawafanya Polisi Tanzania wawe wameiva katika usindikaji na ufungaji wa ushahidi, mbinu za uchunguzi wa eneo la uhalifu, kusimamia na kufanikiwa kumaliza uchunguzi wa mauajib, mbinu za upigaji picha za uchunguzit, stadi za mahojiano na kuandaa taarifa n.k

Hapa ndipo tunapohitaji kuwa na vijana wenye ufaulu mzuri kutoka kidato cha 6 wanaopaswa kujiunga Polisi Tanzania kwa ajili ya mafunzo kama haya. Na mafunzo haya yanapaswa kutolewa kwa mamia ya Polisi nchini Tanzania, na si kupeleka mtu mmoja au wawili nje ya nchi halafu anaishia kuhamishiwa makao makuu ya Polisi Tanzania.

Chini nimeweka video ya Sinza na picha ndogo za mfano wa jinsi Polisi Kenya wanavyofanya uchunguzi wa eneo la tukio la uhalifu kwa kupitia tukio la karibuni la Polisi Caroline Kangogo anayesadikika kujiua (wengine wanaamini kauawa) baada ya kuua watu wawili.

2847343_images_1.jpeg

Kangogo-photo-.jpg


images (1).jpeg
 
Kimsingi watanzania tuache kufanya matendo ambayo yatakuja kugharimu maisha yetu yote, control hisia zako hasa wivu wa mapenzi,hizo bastola usizipendo kama unaona maisha yako hayapo hatarini kisa jamaa yako anayo na we una miliki kila siku unaenda nayo bar, kuhusu uchunguzi wa maeneo ya matukio tuwaachie mamlaka husika nadhani kama sio member wa hizo mamlaka huwezi jua wanafanyaje chunguzi zao.
 
Wote wamekufa sasa hapo Polisi watachunguza nini?

Muuaji naye kajiua kesi imeisha hapo.
 
Nimefurahi tukio kutokea.
Dini imekataza ulevi
 
Nikiri kwamba andiko hili limepata nguvu kutokana na mauaji yaliyofanyika katika Bar ya Lemax, Sinza, kama yalivyoletwa na Tusker Bariiiidi. Kupitia taarifa ya ITV, ukichunguza kwa umakini utagundua kuna mhanga wa hili tukio, mwili wake umelala kwenye kiti, ingawa polisi wapo wakirandaranda kila kona, hakuna tukio lolote kubwa linalofanyika la kiuchunguzi zaidi ya kuchukua maelezo ya mashahidi na (labda kupiga picha), na hatimaye wataondoka na miili ya marehemu.
Hawa Polisi ambao mtu anawadanganya Mbowe ni gaidi wanakimbia kumkata bila kwanza kutafuta supporting evidence? Wapumbavu sana hawa.
 
Nikiri kwamba andiko hili limepata nguvu kutokana na mauaji yaliyofanyika katika Bar ya Lemax, Sinza, kama yalivyoletwa na Tusker Bariiiidi. Kupitia taarifa ya ITV, ukichunguza kwa umakini utagundua kuna mhanga wa hili tukio, mwili wake umelala kwenye kiti, ingawa polisi wapo wakirandaranda kila kona, hakuna tukio lolote kubwa linalofanyika la kiuchunguzi zaidi ya kuchukua maelezo ya mashahidi na (labda kupiga picha), na hatimaye wataondoka na miili ya marehemu.

Video iko hapa


Hii imekuwa ni kama kawaida ya jeshi la Polisi Tanzania inapofanya uchunguzi wa kifo. Tukio kubwa wanalokuja kulifanya ni kubeba miili ya marehemu tu. Huwa hawako serious. Ndio maana baadhi ya kesi huwasumbua sana mahakamani wakikutana na wakili mzuri kwani baadhi ya evidence wanakuwa waliziacha kwenye eneo la tukio la uhalifu (crime scene).

Ukiangalia namna Polisi Tanzania wanavyo treat crime scene utajua hawana mafunzo ya kutosha ya kufanya uchunguzi wa makosa ya jinai. Na kama kuna mafunzo wanayapata huko vyuoni kwao, basi ni bora hayo mafunzo yafutwe tu kwani hayana tija. Polisi Tanzania wanapofanya uchunguzi wa matukio ya kihalifu, wanafanana na kijana wa mtaani anayetafuta mgoni wake, lakini tofauti ni kwamba wao Polisi wana access ya kupata taarifa maeneo mengi kama TCRA, NIDA, Bank na sehemu nyingine ambazo raia wa kawaida hana.

Ukiangalia video za matukio yote ya mauaji hapa Tanzania utashangaa kuna uchunguzi gani unafanyika zaidi ya wao kwenda kwa spidi kukusanya mwili au miili ya wahanga.

Hakuna video ambayo waweza ona hata kamba tu ya kutenga eneo la tukio la mauaji ili kutolichafua imewekwa. Huoni hata alama za utambulisho (identification markers) kama stendi za plastiki zenye namba, au bendera inayoonesha alama za ushahidi katika eneo la tukio la uhalifu. Polisi naamini wanajua kwamba vitu vidogo kama hizo identification markers husaidia kufunua, kurahisisha, kupanga na kubaini vitu vingi vya ushahidi unaopatikana kwenye eneo la matukio la uhalifu. Inapotumiwa vizuri inawaruhusu hata wengine kuelewa kwa urahisi tukio zima.

Wito kwa Polisi Tanzania na Vyuo Vikuu vya Tanzania, kujenga ushirikiano na vyuo vikuu vya kigeni ili kuanzisha kozi ambazo mwisho wa siku zitawafanya Polisi Tanzania wawe wameiva katika usindikaji na ufungaji wa ushahidi, mbinu za uchunguzi wa eneo la uhalifu, kusimamia na kufanikiwa kumaliza uchunguzi wa mauajib, mbinu za upigaji picha za uchunguzit, stadi za mahojiano na kuandaa taarifa n.k

Hapa ndipo tunapohitaji kuwa na vijana wenye ufaulu mzuri kutoka kidato cha 6 wanaopaswa kujiunga Polisi Tanzania kwa ajili ya mafunzo kama haya. Na mafunzo haya yanapaswa kutolewa kwa mamia ya Polisi nchini Tanzania, na si kupeleka mtu mmoja au wawili nje ya nchi halafu anaishia kuhamishiwa makao makuu ya Polisi Tanzania.

Chini nimeweka video ya Sinza na picha ndogo za mfano wa jinsi Polisi Kenya wanavyofanya uchunguzi wa eneo la tukio la uhalifu kwa kupitia tukio la karibuni la Polisi Caroline Kangogo anayesadikika kujiua (wengine wanaamini kauawa) baada ya kuua watu wawili.

2847343_images_1.jpeg

View attachment 1857865

View attachment 1857863
Ukiwaambia ukweli huu ni wabishi balaa polisi Tanzania inajua kuhoji kwa kusulubu persecution interrogation sio critical investigation. Zamani ukipeleleza kesi ukashindwa mahakamani ulikuwa unajaziwa F kwenye faili lako la ajira na ilikuwa inakunyima fursa ya kwenda kozi ya kupanda renki, siku hizi tunaangalia vigezo vingine vya ukoo, siasa, elimu kwa maana ya cheti hata kama hakina ubora mwisho hata syllabus ya vyuo imebaki hilehile ya mwaka 47. Ukweli ni kwamba upolisi ni taaluma nyeti ambayo inatakiwa kufundishwa kwa kiwango cha digrii na isipatikane kirahisi mpaka mhitimu amefanya utafiti wa aina fulani ya uhalifu na kuja na innovation ya kuondoa uhalifu huo.
 
Back
Top Bottom