Mtembea kwa miguu aliyegongwa na basi la mwendokasi atolewa ICU

Mtembea kwa miguu aliyegongwa na basi la mwendokasi atolewa ICU

Nyendo

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2017
Posts
1,336
Reaction score
4,731
apona-jpg.2527428

Mtembea kwa miguu aliyegongwa na Basi la Abiria la "Mwendokasi" wiki iliyopita ambaye ndiye alikuwa Majeruhi pekee wa ajali hiyo aliyesalia katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI), ameondolewa katika Chumba cha Uangalizi Maalum (ICU) na kuhamishiwa wodi nyingine ya HDU baada ya afya yake kuzidi kuimarika.

Meneja Uhusiano wa MOI, Patrick Mvungi amesema pamoja na mambo mengine Majeruhi huyo ameanza kuongea na amejitaja kwa jina moja kwamba anaitwa Osam na Makazi yake ni Manzese, Dar es salaam “Tunaomba Ndugu, Jamaa na Marafiki wanaomfahamu wajitokeze ili kushirikiana nasi kumuhudumia na kumfariji”


Chanzo: Ayo Tv

Pia soma:


UPDATE

Ndugu na mke wa wa majeruhi wa mwendokasi wamejitokeza na kumtambua

Zaidi soma: Aliyegongwa na mwendokasi atambuliwa na mkewe na ndugu yake
 
Mtembea kwa miguu aliyegongwa na Basi la Abiria la "Mwendokasi" wiki iliyopita ambaye ndiye alikuwa Majeruhi pekee wa ajali hiyo aliyesalia katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI), ameondolewa katika Chumba cha Uangalizi Maalum (ICU) na kuhamishiwa wodi nyingine ya HDU baada ya afya yake kuzidi kuimarika.
Kuna wapuuzi walishazusha kuwa kafa, MUNGU anawaumbua

USSR
 
apona-jpg.2527428

Mtembea kwa miguu aliyegongwa na Basi la Abiria la "Mwendokasi" wiki iliyopita ambaye ndiye alikuwa Majeruhi pekee wa ajali hiyo aliyesalia katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI), ameondolewa katika Chumba cha Uangalizi Maalum (ICU) na kuhamishiwa wodi nyingine ya HDU baada ya afya yake kuzidi kuimarika.

Meneja Uhusiano wa MOI, Patrick Mvungi amesema pamoja na mambo mengine Majeruhi huyo ameanza kuongea na amejitaja kwa jina moja kwamba anaitwa Osam na Makazi yake ni Manzese, Dar es salaam “Tunaomba Ndugu, Jamaa na Marafiki wanaomfahamu wajitokeze ili kushirikiana nasi kumuhudumia na kumfariji”


Chanzo: Ayo Tv

Pia soma:

Mungu ni mwema! Shukrani kwa madktari waliompambania afya yake
 
Back
Top Bottom