Mtemi Mirambo VS Mtemi Mkwawa

Mtemi Mirambo VS Mtemi Mkwawa

pole sana homie, kama kawaida yako jana usiku hujala sio!!! nikupitishie viazi na karanga tena baadae najua haujashiba vizuri.

amenishangaza ujue, Milambo na waruguru wapi na wapi mh! haya mjukuu wa mtemi Milambo....ushinde salama.


Homie....!

Karibu matobolwa...😋 Na maziwa...😋
 
Habari zenu wakuu.

Kumekuwa na upotoshaji mkubwa wa historia hasa linapokuja suala la uwezo wa Mwafrika kutokupewa sifa zinazotakiwa kama ilivyo kwa hayati J.K. Nyerere na Nelson Mandela. Afrika inaaminishwa Mandela ni zaidi ya Nyerere hiki ni kituko.

Kuna hili pia la Chief Mirambo na chief Mkwawa eti sifa kubwa anapewa Mkwawa ili tumuone ndio shujaa wetu na pia alipambana akashindwa na wazungu. Nadhani wanataka kutujengea mazingira ya kuwasujudia na kuwaogopa. Itawezekanaje uniamnishe shujaa wangu wa kuigwa ni yule aliyepigwa wakati kuna waliopiga?

Baada ya kuifatilia historia ya mtemi Mirambo a.k.a. Napoleon wa Afrika kama alivyojulikana na wazungu nimegundua kuna upotoshaji mkubwa wa historia.

Chief Mkwawa japo naye si haba ila kwa chief Mirambo hatii mguu hata kucha.

Nguvu za jeshi la Mirambo kwa Afrika mashariki alikuwa hana wakumlingasha. Ndiye aliyetawala eneo kubwa kuliko machief wengine. Tabora mpaka Kigoma eneo lake lilipakana na ziwa Tanganyika japo aliona haitoshi akaingia mpaka Burundi akapiga himaya ya Urundi akasambaratisha.

Wakati Mkwawa anasilaha za jadi kabla hajaletewa bunduki moja na Mwarabu, Mirambo alikuwa anatengeneza bunduki yeye mwenyewe na alimiliki jeshi lilikowa na active personnel zaidi ya 10000.

Hapakuwa na cha mzungu wala mwarabu aliyeleta fyoko kwenye himaya yake aliua kama anau panzi tu ikabidi wafate masharti yake kila wanapopita kwenda Zambia na Kongo walimlipa kodi kwa kuikanyaga ardhi yake huna kodi mzigo wote unabaki na kuwa mali yake.
Wafipa walijichanganya hawakumjua vizuri kichwa chake kikoje. Huyu jamaa alikuwa hana masihara kabisaa!

Wazungu baada ya kubanwa sana waliomba nguvu ya jeshi kutoka kwa sultan wa Zanzibar wakimwambia kwamba Napoleon wa Afrika anataka kuiharibu biashara yako kwakuwa ndiye alikuwa mnunuzi mkubwa wa pembe za ndovu na watumwa kutoka Zaire na Zambia.

Sultan akatuma askari 3000 kuja kuongeza nguvu kwa wazungu wakishirikiana na jeshi la snitch wa Mirambo alikuwa anaitwa Chief Mkasiwa. Jamaa walinyoosha mikono sultan akaona anamaliza watu wake akaamuru jeshi lake lililosalia lirudi Zanzibar haraka walikuwa wamebaki 1500 ndio waliokuwa wamesalimika na jeshi la awali la Mtemi Mirambo lililokuwa likiitwa Luga Luga (walugaluga).

Mtemi Mirambo alikuwa na majeshi matatu ambayo aliyapanga kwa ubora kutoka la kwanza hadi la tatu. Jeshi kali kabisa lenye mafunzo na uwezo wa juu kabisa liliitwa Abaoko kama sijakosea herufi.

Sasa Mkwawa aliuza mali zake kwa Mwarabu pembe za ndovu na kuletewa nguo Mirambo hakuuza mali zake bali alichukua za wazungu walizokuwa wamekusanya sehemu mbalimbali.

Mirambo alichukua watumwa kutoka mikononi mwa wazungu na waarabu na kuwasajili kwenye jeshi lake. Yaani unapomtaja Mirambo jua unataja habari kubwa.

Sasa historia za namna hii zinafichwa na kuoneshwa historia dhaifu ya kumtukuza mzungu kuwa ni bora.

Mtemi Mirambo alifariki kwa ugonjwa wa rovu miaka ya 1880.

Nimeweka hapa kwa kifupi sana. Kwa mwenye interest anaweza kufatilia ahakikishe mwenyewe.

MAGUFULI4LIFE.
Kwa nini umemaliza na neno magufuli4life?
 
Habari zenu wakuu.

Kumekuwa na upotoshaji mkubwa wa historia hasa linapokuja suala la uwezo wa Mwafrika kutokupewa sifa zinazotakiwa kama ilivyo kwa hayati J.K. Nyerere na Nelson Mandela. Afrika inaaminishwa Mandela ni zaidi ya Nyerere hiki ni kituko.

Kuna hili pia la Chief Mirambo na chief Mkwawa eti sifa kubwa anapewa Mkwawa ili tumuone ndio shujaa wetu na pia alipambana akashindwa na wazungu. Nadhani wanataka kutujengea mazingira ya kuwasujudia na kuwaogopa. Itawezekanaje uniamnishe shujaa wangu wa kuigwa ni yule aliyepigwa wakati kuna waliopiga?

Baada ya kuifatilia historia ya mtemi Mirambo a.k.a. Napoleon wa Afrika kama alivyojulikana na wazungu nimegundua kuna upotoshaji mkubwa wa historia.

Chief Mkwawa japo naye si haba ila kwa chief Mirambo hatii mguu hata kucha.

Nguvu za jeshi la Mirambo kwa Afrika mashariki alikuwa hana wakumlingasha. Ndiye aliyetawala eneo kubwa kuliko machief wengine. Tabora mpaka Kigoma eneo lake lilipakana na ziwa Tanganyika japo aliona haitoshi akaingia mpaka Burundi akapiga himaya ya Urundi akasambaratisha.

Wakati Mkwawa anasilaha za jadi kabla hajaletewa bunduki moja na Mwarabu, Mirambo alikuwa anatengeneza bunduki yeye mwenyewe na alimiliki jeshi lilikowa na active personnel zaidi ya 10000.

Hapakuwa na cha mzungu wala mwarabu aliyeleta fyoko kwenye himaya yake aliua kama anau panzi tu ikabidi wafate masharti yake kila wanapopita kwenda Zambia na Kongo walimlipa kodi kwa kuikanyaga ardhi yake huna kodi mzigo wote unabaki na kuwa mali yake.
Wafipa walijichanganya hawakumjua vizuri kichwa chake kikoje. Huyu jamaa alikuwa hana masihara kabisaa!

Wazungu baada ya kubanwa sana waliomba nguvu ya jeshi kutoka kwa sultan wa Zanzibar wakimwambia kwamba Napoleon wa Afrika anataka kuiharibu biashara yako kwakuwa ndiye alikuwa mnunuzi mkubwa wa pembe za ndovu na watumwa kutoka Zaire na Zambia.

Sultan akatuma askari 3000 kuja kuongeza nguvu kwa wazungu wakishirikiana na jeshi la snitch wa Mirambo alikuwa anaitwa Chief Mkasiwa. Jamaa walinyoosha mikono sultan akaona anamaliza watu wake akaamuru jeshi lake lililosalia lirudi Zanzibar haraka walikuwa wamebaki 1500 ndio waliokuwa wamesalimika na jeshi la awali la Mtemi Mirambo lililokuwa likiitwa Luga Luga (walugaluga).

Mtemi Mirambo alikuwa na majeshi matatu ambayo aliyapanga kwa ubora kutoka la kwanza hadi la tatu. Jeshi kali kabisa lenye mafunzo na uwezo wa juu kabisa liliitwa Abaoko kama sijakosea herufi.

Sasa Mkwawa aliuza mali zake kwa Mwarabu pembe za ndovu na kuletewa nguo Mirambo hakuuza mali zake bali alichukua za wazungu walizokuwa wamekusanya sehemu mbalimbali.

Mirambo alichukua watumwa kutoka mikononi mwa wazungu na waarabu na kuwasajili kwenye jeshi lake. Yaani unapomtaja Mirambo jua unataja habari kubwa.

Sasa historia za namna hii zinafichwa na kuoneshwa historia dhaifu ya kumtukuza mzungu kuwa ni bora.

Mtemi Mirambo alifariki kwa ugonjwa wa rovu miaka ya 1880.

Nimeweka hapa kwa kifupi sana. Kwa mwenye interest anaweza kufatilia ahakikishe mwenyewe.

MAGUFULI4LIFE.
Mirambo alikufaje??
Ni saratani ya koo au alinyongwa koo mpaka kufa??
Inaonekana alifariki katika umri mdogo miska 44
 
Mirambo alikufaje??
Ni saratani ya koo au alinyongwa koo mpaka kufa??
Inaonekana alifariki katika umri mdogo miska 44
"Near the end of his life he grew ill, and died, age 44. It is possible that he was strangled to death, since an old Nyamwezi custom was to strangle their mtemi when they became unfit to rule."
 
Why was he unfit to rule?
Nimeleta nukuu tu, sikuweza kuthibitisha chanzo cha habari. Naielewa hivyo.
Mirambo alikuwa kiongozi wa kivita, alipanusha himaya yake kwa njia ya vita. Mamlaka yake juu ya rugaruga ilitegemea uwezo wake kumshinda mpinzani wowote.
Sijui historia ya Wanyamwezi, lakini najua mifano mbalimbali kutoka tamaduni mbalimbali ambako mfalme aliuawa akizeeka mno au kuwa mdhaifu kutokana na ugonjwa. Maana hakufaa tena kama hana nguvu.
menginevyi nimekuta kwamba alikuwa na kansa. Vita yake ya mwisho dhidi Burundi alishindwa kuongoza menyewe akamtuma
Why was he unfit to rule?
 
Kitabu cha "Imperial Footprints: Henry Morton Stanley's African Journeys" cha mwaka 2004 kimesema " Mirambo passed away on December 2,1884 probably due to throat cancer and his empire died with him.

Angeuwawa sababu ya kunyonywa ili apatikane kiongozi mwingine jasiri basi inawezekana ngome yake isingekufa.

Mirambo.jpg
 
Ni kweli Mtemi Mirambo( Maana ya mirambo ni " maiti nyingi" alikuwa hatari sana...
1) Alikuwa anatengeneza silaha mwenyewe...Magobole ( Hata ile nyimbo ya Oooh Tanu yajenga nchi) imechukuliwa kutoka kwenye nyimbo ya walugaluga waliokuwa wakiimba Kinyamwezi kuwa risasi zinabomoa vichwa" bela mitwi"
2) Alikuwa ana wanajeshi hodari sana ( walugaluga) sifa yao hawa jamaa walikuwa wanavuta bangi kama wanavuta sigara...wakishapiga vitu vyao walikuwa ni wakali kama pilipili au sungusungu weusi
3) Alikuwa ana wataalam (wachawi) wa maana hasa, ambao walikuwa wana uwezo wa kuona mambo kabla hata hayajatokea. Hivyo hata kama kuna adui ana mipango ya kuja kumshambulia, anakuwa ameishaonekana na kujulikana atatokea pande gani.
4) Alikuwa ni chief mwenye nguvu za kiuchumi zaidi hata ya Mkwawa, kwasababu alikuwa kwenye route kuu ya kutoka nchi za Congo, Burundi na Rwanda, hivyo ilikuwa lazima kumlipa kodi. Waarabu, wazungu na wafanyabiashara mbalimbali walipokuwa wanapitisha dhahabu,almasi, pembe za ndovu na watumwa, walikuwa wanaacha mzigo wa kutosha! Hiyo ikamfanya awe mwenye nguvu Sana.
Ni kichekesho sana kumlinganisha Mkwawa na Mirambo
 
Ni kweli Mtemi Mirambo( Maana ya mirambo ni " maiti nyingi" alikuwa hatari sana...
1) Alikuwa anatengeneza silaha mwenyewe...Magobole ( Hata ile nyimbo ya Oooh Tanu yajenga nchi) imechukuliwa kutoka kwenye nyimbo ya walugaluga waliokuwa wakiimba Kinyamwezi kuwa risasi zinabomoa vichwa" bela mitwi"
2) Alikuwa ana wanajeshi hodari sana ( walugaluga) sifa yao hawa jamaa walikuwa wanavuta bangi kama wanavuta sigara...wakishapiga vitu vyao walikuwa ni wakali kama pilipili au sungusungu weusi
3) Alikuwa ana wataalam (wachawi) wa maana hasa, ambao walikuwa wana uwezo wa kuona mambo kabla hata hayajatokea. Hivyo hata kama kuna adui ana mipango ya kuja kumshambulia, anakuwa ameishaonekana na kujulikana atatokea pande gani.
4) Alikuwa ni chief mwenye nguvu za kiuchumi zaidi hata ya Mkwawa, kwasababu alikuwa kwenye route kuu ya kutoka nchi za Congo, Burundi na Rwanda, hivyo ilikuwa lazima kumlipa kodi. Waarabu, wazungu na wafanyabiashara mbalimbali walipokuwa wanapitisha dhahabu,almasi, pembe za ndovu na watumwa, walikuwa wanaacha mzigo wa kutosha! Hiyo ikamfanya awe mwenye nguvu Sana.
Ni kichekesho sana kumlinganisha Mkwawa na Mirambo
Kuna ushahidi gani kuwa alikuwa anatengeneza magobore?
 
Mkutano wa Berlin uliharibu mno mfumo wetu wa maisha - sasa hivi tungekuwa na tawala nyingi tu ambazo tungeshindana kwa maendeleo badala ya hii dola moja ambayo tunasonga hatusongi miaka inayoyoma.
 
Uzi wa mihemko tu..huna tofaut na wanaovutia upande wao wale wale tu.

Kuhusu mandela na nyerere

Y wanampa recognition sana mandela ni sabab aliyofanya mandela hakuna mwanadamu ambae ameshafanya mpaka muda huu dunian

Uwe jela kwa makosa ya uhaini ugaidi kwa miaka zaid ya 20s na bado unaendeleza harakat huko hukk jela ili uendelee kukaa huko huko.yaan wanakuja kuku offer uache harakat utoke jela wew hutak unaendeleza harakat halaf siku unatoka..unakuja kuwa rais yan mwenye mamlaka...na unawasamehe waliokutesa maisha yako yote .na unatamka tusahau yanyuma na tugange yajayo

Hakuna mtu anaweza fanya hvo...

Mtoa mada kiufupi hujui kitu.
Kwahiyo hilo unaona ni ushujaa?
 
Kuna ushahidi gani kuwa alikuwa anatengeneza magobore?
Sasa kutengeneza magobori si teknolojia kubwa wakati wa karne ya 19 . . . Kama angeishi miaka 6,7 zaidi angekutana na askari Wasudani wa Wajerumani asingekuwa na uwezo wa kupinga tena.
 
Rungwe huko Mjerumani na watu wake walichapwa mpaka sijui wakaangukia Nyasaland huko tena kimyakimya.
Nenda uliza kilichofanyika mwakaleli na Rungwe.
 
Google tu Germany east africa kyusaland.
Ee kaka sasa unakimbia. Labda ulisikia jambo bila uhakika sasa huwezi kutuambia kitu tuende google?
Wanyakyusa wakati wa mwanzo wa ukoloni hawakuwa na nguvu maana walikuwa na machifu wadogowadogo tu. Merere wa Usangu aliwavamia bado mwaka 1892 akapora mifugo na wanawake.
Wajerumani walifika baada ya 1890 tu, maana walianza utawala pwani walipopambana an Abushri na baadaye na Wahehe. Hapakuwa njia hadi Tukuyu kenye nchi kavu. Wamisionari wa kwanza walifika 1891 kupitia Ziwa Nyasa.
Hali halisi eneo lilikuwa nje ya upeo wautawla wa kikoloni kwa miaka, na mwaka 1900 tu serikali ya koloni iliunda kituo cha utawala Neu Langenburg (leo Tukuyu) bila mapigano, baadaye walianzisha kituo cha kijeshi Masoko ambo waliweka kombania moja, lakini hapakuwa na mapigano.
Je vita yako ilitokea wapi na lini?
 
Back
Top Bottom