mwengine alikuwa anaitwa Mawombekelo, huyu alikuwa alikuwa na uwezo wa kujaa ndani pindi anapogundua pombe anayokunywa ni tamu, kama ndani kuna watu wengi anajaa peke yake chumba kizima.
duh
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
mwengine alikuwa anaitwa Mawombekelo, huyu alikuwa alikuwa na uwezo wa kujaa ndani pindi anapogundua pombe anayokunywa ni tamu, kama ndani kuna watu wengi anajaa peke yake chumba kizima.
There will be any no any exception to compare Jesus with some Sukuma Magician whom his existence can not be concretely be established
Hakuna hifadhi mahali alipokanyaga Ng'wanamalundi.
Wednesday, 13 July 2011 20:34
Na Charles Kayoka.
Kwa Watanzania wa umri wangu waliopata kusoma historian au kusikia hadithi za makabila, hasa ya Wasukuma na Wanyamwezi, hawakukosa kusikia habari ya Ng'wanamalundi. Aliyezaliwa katika ukoo wa kiuganga na uchifu aliyehesabiwa kuwa ni mmoja ya watu wenye miujiza mingi.
Ng'wanamalundi anaelezewa kuwa na uwezo wa kufika mahali mbali kutoka nyumbani kwa muda mfupi, sijui alitumia nguvu gani? Aliweza kutibu watu kwa
uganga wake kwani alifahamika sana kwa hilo; na alikuwa anaweza kuvuka maji marefu kwa kuweka dawa na maji yakajitenga na yeye akapita.
Nilipokuwa ziarani wilayani Kahama hivi karibuni,nikifuatilia mahali alipofia Mtemi Mirambo wa Unyamwezini (nitaelezea habari zake katika moja ya makala zijazo), nikaambiwa "huko nilikotoka, kijiji cha Nyandekwa, kuna jiwe ambako Ng'wanamalundi alikuwa amelikanya na alama ya unyayo wake hadi leo uko.
Siku ya pili nikafunga safari hadi kijijini Nyandekwa, kiasi cha kilomita kumi kutoka makao makuu ya wilaya ya Kahama katika njia iendayo Urambo kupitia Uyogu.
Hapa nilipofika na wenzangu tukabahatika kukutana na kaka wa umri wa makamo aliyejitolea kutupeleka kwenye "jiwe" hilo.
Ni kiasi cha kilomita moja toka barabara ya Uyogu na hakuna barabara ya gari zaidi ya njia za wafugaji wa ng'ombe. Tukaifuata njia hiyo tukiwa ndani ya Landcruiser,maana sidhani kama unaweza ukaenda na gari dogo zaidi ya hilo likarudi salama, hasa kama mvua imenyesha.
Ninaeleza hivyo kwa sababu nilidhani hiki ni moja ya kivutio kikubwa sana cha kiutamaduni na historia na kingejengewa barabara ili watalii wa ndani na nje wangeweza kufika kutembelea.
Hapo ni mahali penye mwamba mkubwa wa jiwe. Tukaona watoto na akina mama wakianika nafaka kwenye jiwe hilo.
Tulipofika na kuwauliza kama wanajua habari za Ng'wamamalundi na uhusiano wake na jiwe lile walisema hawajui chochote, na mwingine alisema yeye ni
mgeni eneo lile.
Tulipanda mpaka juu na kuona alama tatu za nyayo za binadamu. Alama ya tatu imefutikafutika lakini mbili zilizobaki zilikuwa bado zinaonyesha vizuri. Moja
ilikuwa ndogo, kiongozi wetu alisema kuwa ile ndogo ilikuwa ya mke wa Ng'wanamalundi.
Na ingine iliyokuwa kubwa ilikuwa ndiyo ya Ng'wanamalundi mwenyewe. Na hadithi zinasema Ng'wanamalundi alikuwa na miguu mikubwa, huenda ndio sababu ya kuitwa Malundi- miundi- Miguu. Yaani mtu mwenye "mamiguu". Alama ya unyayo huu ilikuwa kubwa, na ilikuwa na alama ya kukatwa katikati.
Tuliambiwa kuwa ni mkewe ndiye aliyeikata ile lama, hatukuelezwa ni kwa kusudi gani. Lakini fikiria binadamu kuwa na uwezo wa kukanyaga kwenye jiwe na kuweka alama iliyodumu kwa zaidi ya miaka sabini.
Pembeni yake palikuwa na jiwe la mviringo ambalo huwezi kulinyanyua, labda uwe na nguvu za Ng'wanamalundi mwenyewe. Jiwe hili lilikuwa na mashimo yaliyokuwa katika mistari iliyonyooka na nilipochunguza nilihisi kuwa ni mashimo ya kuchezea bao,ule mchezo wa kienyeji unaochezwa na watu wawili hadi wanne kwa kutumiamawe kwenye mashimo.
Niliona kuwa kulikuwa na mashimo ya kutosheleza watu wanne kucheza- yaani mabao mawili.
Tulielezwa kuwa hapo ndipo Ng'wanamalundi alipopenda kucheza bao na rafiki zake. Alitengeneza lile bao kwa kufinya mkono wake wenye nguvu za ajabu
kwenye lile jiwe na mashimo kutokezea.
(Hii sio hadithi ya kwanza kusikia, hata huko milima ya Uluguru kuna mahali ambapo Chifu Kingalu na wenzake walikuwa wakishindana kuonyeshana nguvu za uchawi KWA kutengeneza mashimo ya bao kwenye mawe kwa kutumia visigino vya miguu.
Moja ya bao hilo liko hadi leo pembeni ya mto huko milimani- Morogoro- picha ninazo). Na wengi kule Kahama wanasema kuwa mashimo kama hayo ya
Ng'wanamalundi aliyatengeneza sehemu nyingine nyingi, maeneo ya Shinyanga na Mwanza.
Mahali hapo pamesahaulika, huenda kwa waganga wachache wanapopakumbuka hapo kwa ajili ya matambiko yao. Lakini hakuna ulinzi, hakuna kumbukumbu, na miguu hii ya Ng'wanamalundi na mkewe inafutika kutokana na upepo, mchanga, jiwe kutumika na binadamu na mvua.
Huu ni utalii wa kihistoria lakini hautumiwi. Wiki ijayo tutazungumzia jiwe la "nyasaolo"katika kijiji cha Busolo, ambako ukifanya tambiko na kuliomba likatikisika ujue maombi yako yamekubalika.
utaliiupdate@gmail.com , 0766959349
Pole mkuu!Mchawi bandle
Mkuu umeongea kwa uchungu sanatunahitaji na utamaduni wa hawa watu...wadumishajo wa mila MASAI.
Kule kigoma vijijini Kibondo kuna kijiji maarufu Makere ushingo...mbona ulikua mtu unaenda kuununua urozi tu. Na hapo hapo unafanya majaribio! Hizo zote ni hazina tunazo lakini wazungu walivyo wajanja wakaleta dhana zao na misaada yao ili watu wachukie maarifa yao...sasa vitu hivyo kwishneiii!
Hata mabwawa ya mvua tunashindwa kuyajaza kwa karama za babu zetu. Mimea na ukame kibao. Tumerogwa sana na hawa wazungu lakin hatujawajua .
Aibu kubwa sana. Hii ni uchawi mimi naona inafaa sana tena waipe kipau mbele mashindano mara kwa mara yafanyike ili tuwapate wataalam wakubwa. Bado tunahitaji hizi taaluma sio kuwadanganya watu eti uchawi unafanywa na wasio akili au maskini....nani anawadanganya? Wafalme zamani au ili kiongozi lazima uwe mtaalam ndio unaupata uongozi. Halafu kama hamjui maana ya MAgick = wiseman.
Tubadilike na tukubali mambo ni mengi tunayasahau na kuyadharau ajili ya kupewa pewa vijizawadi vya magari ya fahari na mambo mengine kwa mashart mabaya . Inaniuma sana!!!
Una Uzi wakeMsitu wa njombe una maajabu gani?
😂😂😂😂 Kama mchawiWalikuwa na miujiza kama ya manabii ila kwa kuwa alizaliwa Afrika walimchukulia kama mchawi tu.mfano alinyoosha kidole kwenye miti ambayo hai na kukauka ili wake wake akate kuni.
Mengine kesho