Mtihani mkubwa kwa Rais Samia ni kuongeza mishahara ya Watumishi wa Umma. Je, ataweza?

Tena ingependeza angetoa increment za tokea 2015 ambazo hazijawahi kutolewa.
 
Anaweza kabisa, akiamua tu kusimamisha zoezi la uwekaji wa taa za barabarani kule kijijini kwa mwendazake na ule ujenzi wa Wembley stadium Atapata fedha za kutosha sio tu kuongeza mishahara bali pia hata kupandisha watumishi madaraja.
 
Hilo ni moja mitihani anayo mingi tu , malipo ya wastaafu , waliofungwa kwa uonezi kesi za uhujumu uchumi , utakatishaji fedha , fidia wahanga wa korosho , vyeti feki , walioporwa pesa zao mabenki , bureau de change n.k mambo Ni mengi atayamaliza tu moja baada ya jingine .
 
Mkuu hichi ulichoongea kina maana kubwa sana. Watanzania hawajui wajibu wao mpaka wafokewe fokew kama watoto. Na tuna ubinafsi hicho ndio kinatugharimu. Siku watanzania tukibadilika na kuanza kuifikiria Tanzania na kuipenda kutoka moyoni vizazi vijavyo vitaikuta Tanzania ikifanania na nchi za ulaya. Watanzania tuacheni ubinafsi na kujipenda tukaipende nchi yetu na kuijenga maana ndicho mungu ametupa. Mimi sio mwajiriwa serikali na wala sitegemei ajira serikali sio kwamba nina uwezo la hasha elimu yangu hairuhusu hilo kwa mujibu ya sheria za Tanzania. Tuikatazame Tanzania kwa ajili ya vizazi vyetu vijavyo.
 
Mkuu tulia..
Tuna letu. We waache tu.
 
Hili wala hakukuwa na haja ya kianzishia uzi
 
Unaita huo ni mtihani mgumu ?

Hivi hao watumushi wapo wangapi kwanza ?, Na wasio watumishi ni wangapi ?

Nadhani mtihani ni kuhakikisha wasio watumishi / hawana security yoyote nao wanapata ajira
 
Reactions: Ame
haya yoote yaende sambamba na Serikali kujali watumishi wake na Wananchi kwa ujumla. Huku sisi kama Watanzania tukaipende Tanzania yetu ta tuifanyie kitu. Ili baadae tuje kujivunia
 
Tumtumie hata kikwete atuelekeze alifanikiwa vipi kuyaweza yote!!!
Ila kusubir miradi itengamae ndo waongeze mishahara[emoji44][emoji44]hapa siafiki kwani miradi yenyewe ni hasara tu
Mfano hasara iliyosababishwa na ATCL Pekee kwa Mwaka mmoja zaidi ya bil 60!!!sasa wangeamua kuzitumia hizo kwenye maslahi ya watumishi hizi kelele zisingekuepo.
 
Namshukuru mungu japo akili za kawaida zimekurejea.
Hakuna ugumu wowote mishahara huongezwa kwa mujibu wa sheria. Raisi asiyefuata sheria hata kama ana nia njema kiasi gani huyo ni wa kulaaniwa
Mungu amlaani nyapara yule ampe anachostahili
Inshallah
 
Mwaka huu haiwezekani labda mwakani. Akiongeza mwaka huu vizuri ila atakua mkurupukaji maana hajajua chungu cha hazina kikoje.
 
Bajeti ilishaandaliwa kitambo tu sasa inasubiriwa kusomwa bungeni kwahiyo kama ipo ipo tu na kama haipo haipo tu
 
Watumishi mna njaa kali sana nadhani mama atasikia kilio chenu. Amesema huwa anapita humu kusoma upepo unaendaje
 
Katika Watu wenye Roho Mbaya Nchi hii basi ni Watumishi wa Umma.Sasa badala ya Kumwambia Mama Aajiri sisi Wadogo zenu tusio na Ajira ninyi mnawaza Kuongezewa Mshahara.Kuweni Wazalendo hii Nchi ni Yetu Sote.Nasi tunatamani Ajira.Tuna Njaa Kila siku Tuko Jukwaa la Ajira Tukiangalia Fursa.Nyie Watumishi tulieni kwanza
 
Reactions: Ame
Kama hali na mwenendo wa kiuchumi wa nchi utaruhusu natumaini ataliangalia hili.
 
Yaani wewe kukosa ajira kisiwe kigezo cha kuwanyima haki zao watumishi wa umma
 
Kama JK, alikuwa anaongeza mishahara kila mwaka na tuliambiwa nchi ilikuwa imeoza, sasa hivi atashindwa vipi wakati tunaambiwa serikali ina pesa za kutosha kuliko wakati wowote.
Duhh.. Watu mmetoka mafichoni
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…