Mtihani mkubwa kwa Rais Samia ni kuongeza mishahara ya Watumishi wa Umma. Je, ataweza?

Mtihani mkubwa kwa Rais Samia ni kuongeza mishahara ya Watumishi wa Umma. Je, ataweza?

Unaangalia uchache au athari za hao wachache? Unadhani watumishi ni walimu na manesi tu kuna madaktari wanajeshi polisi n.k na huwezi kwenda kinyume na hilo kundi kwa miaka mingi ukadhani Mungu atakupa kibali cha kuongoza kwa miaka mingi. Lazima tukupeleke chato kukuzika. Kwasababu haohao unaowaita wachache ndio aenye uwezo wa kukufanyia figisu yoyote au hata kushirikiana na mabeberu kukuangamiza bila wewe kujua. Upo au haupo?
Duh kweli uelewa nao ni tofauti kati ya mtu na mtu....

Hivi unadhani ni kazi kuchukua mapato huku na kule na kubana sekta zote ili kupelekea budget hata asilimia 95 kwa hizo sekta ? Huo sio mtihani mgumu ni uamuzi tu...

Mtihani ni kuhakikisha zinatengenezwa policies za kuweza kuinua kipato cha asilimia kubwa ya wananchi ambao wengi wao hawapo kwenye sekta za serikali...

Na kuonyesha ni jinsi gani fikra zako zilivyo unaangalia kwamba afanye kitu (sio kwamba kitu hicho ni manufaa ya nchi) bali afanye kitu ili yeye aendelee kukaa pale, fikra hizi na ubinafsi huu ndio umepelekea wanasiasa kufanya vitu vidogovidogo vinavyoonekana (short term plans) na sio vitu endelevu vyenye impact kubwa ambavyo vinachukua muda na huenda visionekane haraka (long term plans) kwa kuhofia kukosa kura/kula
 
Katika Watu wenye Roho Mbaya Nchi hii basi ni Watumishi wa Umma.Sasa badala ya Kumwambia Mama Aajiri sisi Wadogo zenu tusio na Ajira ninyi mnawaza Kuongezewa Mshahara.Kuweni Wazalendo hii Nchi ni Yetu Sote.Nasi tunatamani Ajira.Tuna Njaa Kila siku Tuko Jukwaa la Ajira Tukiangalia Fursa.Nyie Watumishi tulieni kwanza
Dogo jiongeze maisha sio kulia lia..utazeekea home na kushindwa kuhudumia familia ukikaa uasubiri ajira..graduates mko wengi hakuna serikali duniani inayoweza ajiri wote.

#MaendeleoHayanaChama

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mtihani mwingine Mkubwa Ni unyanyasaji wafanyakazi sekta binafsi na ulipwaji wa MAFAO.

Mfano Sekta binafsi, watu wengi wanapoteza kazi kwa sababu mbali Mbali. FAO LA KUJITOA ni muhimu.

Watu walipwe mafao yao, ili wafungue biashara zao na wawe walipa Kodi wapya.

Mtu akipoteza Kazi mfano wenye elimu, wengi wanapoteza mafao yao. Wanaambiwa wasubiri 55 years

Wabunge wa CCM wanapitisha miswada bungeni ya kunyanyasa Wanyonge'.

Hao watetezi wa Wanyonge' wako wapi?
Hivi waziri wa hii mifuko ni nani? Nimwandikie barua
 
Hilo linawezekana , suala ni utashi tu wa serikali! Zanzibar watumishi wameongezewa mishahara kwa miaka yote 5 ya Rais Shein na mwaka huu pia suala hilo lipo kwenye bajeti, je kwanini huku bara serikali ishindwe?
Maendeleo ya watu ndio kipimo sahihi cha maedeleo ya Taifa lolote duniani! Hivyo watumishi ni lazima sasa wakumbukwe kwani wengi sana kwa miaka hii 5 wamedumaa mno kimaendeleo!
 
Jitahidi kupambanua mambo kama Mtumishi wa Umma Duniani kote kuna mgawanyo wa majukumi-unaposema Watumishi wajiongezee kipato kutoka wapi?? Unataka wafanye kazi sehemu zingine au wafanye biashara??? Wakifanya hivyo maana take wataharibu hizo kazi za mishahara hazita kuwa productive tena.

Miradi ya Serikali ni endelevu,vizazi vyetu vitakufa na kuacha miradi ikiendelea,cha msingi ni kubalance vitu vya kufanya kwa kuweka vipaumbele huwezi kukamilisha kila kitu kwa awamu moja na ndio maana kuna kupokezana
Kabla ya kujibu tafuta kuelewa, siyo usome ili ujibu...Hakuna sehemu nimesema wajiongezee kipato nimesema waongeze ufanisi kwenye kazi zao ili zilete tija kisha kipato cha taifa kitapanda na wao wataweza kupata mafao mazuri zaidi ikiwemo mishahara mikubwa...Sasa unaongezaje ndiyo hapo waache kuamka asubuhi kwenda kazini na kufanya kazi kwa mazoea; wawe wabunifu...Nimetoa na mifano...
 
Kwahiyo bado hujaelewa watumishi ndiyo wakutengeneza ajira? Daah kazi kweli kweli!

Haya kazi na iendelee...
Watumishi kudai stahiki zetu na wengine kudai ajira mpya kuna uhusiano gani?

kama ningeelewa nisingeuliza kama unaelewa toa maelezo kama hueleweki unapita.
 
Tumtumie hata kikwete atuelekeze alifanikiwa vipi kuyaweza yote!!!
Ila kusubir miradi itengamae ndo waongeze mishahara
emoji44.png
emoji44.png
hapa siafiki kwani miradi yenyewe ni hasara tu
Mfano hasara iliyosababishwa na ATCL Pekee kwa Mwaka mmoja zaidi ya bil 60!!!sasa wangeamua kuzitumia hizo kwenye maslahi ya watumishi hizi kelele zisingekuepo.
Am listening🤔
Watumishi kudai stahiki zetu na wengine kudai ajira mpya kuna uhusiano gani?

kama ningeelewa nisingeuliza kama unaelewa toa maelezo kama hueleweki unapita.
Huo utumishi maana yake ni nini?

Unamtumikia nani basi kama huwezi kuwasaidia kwa mahitaji yao including kuwatengenezea ajira?
 
Mimi pia ni mtumishi wa umma, na kama tupo serious basi wakati huu si wakati wakutia pressure kuongezewa mishahara, bali kuwezesha madaraja kuwa katika nafasi zake kwanza. Hii serikali inaliweza iwapo watumishi pia watakuwa na sense of humour...Watumishi wa umma waache ku duplicate activities na wawe wabunifu ili kuongeza pato la taifa bila hivyo hii miradi tuliyoianza inaweza shindwa kuendelea na tukajikuta tumepata hasara mara mbili, kwakujifunga mikanda miaka yote mitano kisha tusifikie ile target ambayo ingefikiwa itaongeza uchumi zaidi ya mara kumi...Tukifikia target mishahara itaongezeka mara hata 10 kwakua miundombinu ya nchi itakuwa imekamilika...

Tatizo ni hata kwa ambayo imeshakamilika bado haijatendewa haki na watumishi hao hao wa umma, haiongezi tija...Soko la Morogoro kwa mfano, ndani ya mwezi moja limesha kuwa chafu, sakafu ni kama imejengwa 5 years ago na hapo tuna mabwana afya etc...Hivi huyo unamwongezea mshahara kwa lipi? Masinki yameshaanza kubadili rangi, for serious?

Mie nilitegemea ongezeko la ajira kwakua usafi ungefanywa kwa status ya jengo na lina implications kwenye uchumi, wauzaji wana uniform hiyo ingeongeza ajira kwa mafundi cherehani; mazao yapo kwenye angalau packages zenye kueleweka locally made na wasuka mikeka etc...Lakini wapi, no creativity watu wamehamia kwenye nyumba bora wakiwa na tabia zilezile za matopeni...Basi wangewapiga hata semina kidogo, what was a need ya kujenga hilo jengo? Kama watu wako vilevile biashara zipo vilevile kisha eti mtumishi anawaza kuongezewa mshahara, kweli watumishi wenzangu?

Hivi tunajithamini kweli? Itatoka wapi hiyo pesa ya nyongeza kama wewe hujaongeza ufanisi?
Umesikika mtumishi wa Umma kutoka stand ya Msamvu.
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Umesikika mtumishi wa Umma kutoka stand ya Msamvu.
Na hapo pia pafanyieni ubunifu...Kweli vyumba vya ticket mmeviweka chini nani atapanda juu kwenye hayo maduka ya juu mliyokuwa mmepanga yawe huko?

Tutumie mali zetu tulizoachiwa urithi kwa ubunifu kama anavyotuhimiza mama, Mh. Rais wetu Samia Suluhu Hassan; hii ni ili kuongeza ufanisi na tija kwa uchumi ili hata madai yetu yapate maaana...

Uchumi una dai kuwa lazima ule ulichokizalisha na siyo ule mbegu, siyo endelevu wajameni watumishi wa umma...Tumepewa keki ya taifa kwanza ili tupate nguvu za kuwatengenezea na wenzetu walio wengi cake zao...Tuache mazoea na tuache ubinafsi...Nchi hii ni yetu na hakuna mjomba wakuja kutusaidia...

Nitakutembelea, maana nipo tu hapo jirani na wewe!
 
Am listening🤔

Huo utumishi maana yake ni nini?

Unamtumikia nani basi kama huwezi kuwasaidia kwa mahitaji yao including kuwatengenezea ajira?
Skuelewi unachobishia!!una maanisha ni heri kuwa na lundo la watumishi serikalini hata Kama wanalipwa vijisenti ambavyo havitoshi hata kula tu?!!kama unamaanisha hivo basi ww unasumbuliwa na Wivu ulioambatana na uvivu wa kufikiria

Hakuna serikali Duniani ambayo itaajili nusu ya raia wake,serikali kazi yake ni kuandaa mazingira ya watu kujiajiri na kuajiriwa private sectors! serikali haiwez kumuajili kila graduate wa chuo kikuu😲😲

Tumia elimu yako kupata pesa,ukifanya hivo hata hiyo ajira ya setrikali utaiona haina maana.
 
Skuelewi unachobishia!!una maanisha ni heri kuwa na lundo la watumishi serikalini hata Kama wanalipwa vijisenti ambavyo havitoshi hata kula tu?!!kama unamaanisha hivo basi ww unasumbuliwa na Wivu ulioambatana na uvivu wa kufikiria

Hakuna serikali Duniani ambayo itaajili nusu ya raia wake,serikali kazi yake ni kuandaa mazingira ya watu kujiajiri na kuajiriwa private sectors! serikali haiwez kumuajili kila graduate wa chuo kikuu😲😲

Tumia elimu yako kupata pesa,ukifanya hivo hata hiyo ajira ya setrikali utaiona haina maana.
🙏

Na hutuweza kunielewa kwakua tupo level za tofauti...Kila la heri
 
Back
Top Bottom