Angesema lugha ya kufundishia ni kiingereza kuanzia shule za awali ningeunga mkono, lakini kwa hili hapana.
"lazima ujue kuandika na kuongea kiingereza" nafasi nyingi za kazi hili ni sharti lao kuu,
sere nzuri ya wao kuendelelea kututawala maana watoto wao watasoma hizo shule kama faiza na santi meri sisi wa kwetu za kata
ina maana wao wataendelea kututawala maana sisi tutakuwa hatuna elimu...
ntakula nao sahani moja
wamelileta hili wakati muafaka kabisa, hii ni sababu tosha kabisa ya kuwaondoa hawa wehu.
Majanga,
Najiuliza tu ma-housegirl... mimba nk miaka saba tu shughuli sasa unaweka mpaka form four.., saidia fundi watapatikana wapi? Mi mawazo yangu ni kuwa na wasomi haswa na kuwa vocational skilled labour force haswa.
Hivi ni shule gani za msingi cum secondari zitakazoweza kuwafundisha elimu ya ufundi haswaaa. Vifaa watavipata wapi?Bunsen burner tu wameshindwa kununua je wataweza kununua lathe machine?
Nilifikiri elimu ya msingi iwe mpaka darasa la tano, then unakuwa na wale wanaoenda michepuo ya vocational na wale wanaoendelea na pure shule hivyo hivyo mpaka secondary, na iwe compulsory.
Tatizo letu sasa tuna wasomi wavaa tai wasiojua kufunga tai. Graduates weeengiii lakini weupeeee , matokeo yake wachina wanakuja na nyundo za kunyoosha magari na wanapiga hela ya hatariii.
Dah, yani mi hata sielewi dunia watakayoishi watoto wetu.
Wototo wote wanahaki ya kupata Elimu. Suala la usomi in wachache sana wanahitajika hao ndo wangangane na international languages ambapo ofcos Swahili is among them
Wakifanya hivyo, watoto wa wenye hela watasoma English medium. Hapo sasa mtoto wa kapuku ataishia kuwa karani. kutumwa tumwa chai. Nan atamuajiri mtu asiyetema yai?
Hii ni sera inayolenga watawala wetu wa sasa waendelee kutawala vizazi na vizazi kwani watoto wa watawala hawasomi kwenye hizi shule ambako sera hii itakuwa implemented. Nchi ambazo wanatumia lugha zao wenyewe wanayo base nzuri kiuchumi na wana viwanda vinavyozalisha vitu mbali mbali vinavyotakiwa katika maisha ya kawaida ya mwanadamu. Sisi tunataka kiswahili kitumike mpaka University wakati hata uwezo wa kutengeneza mswaki wa meno hatuna.
Hebu tujiulize, leo tumenunua machine ya kuchambua pamba ambayo operating manual yake ni Kiingereza, huyo mwenye degree ya kiswahili ataweza kuoperate hiyo machine? Hii ya kusema kiingereza kitafundishwa tu kama lugha hebu angalia ni wangapi wanaomaliza darasa la saba (baada ya kusoma kiingereza kwa miaka saba kama lugha) wanaweza hata kuandika sentensi sahihi ya kiingereza.
Wakati watoto wa wanyonge watakuwa wanasoma kwenye mfumo huu wa elimy, watoto wa watawala watakuwa wako marekani na uingereza wakisoma kwa lugha hiyo hiyo ambayo sera hii inaikataa.
Kwangu mimi, sera hii ni upuuzi mtupu ni ni kikwazo cha watoto wa wanyonge kupata ajira nje ya Tanzania.
Tiba
Ushafika UN? waulize kina kikwete kama kwenye zile Headphones wanazovaa wakiwa UN/AU tafisiri ya kiswahili haipo?
Ushafika UN? waulize kina kikwete kama kwenye zile Headphones wanazovaa wakiwa UN/AU tafisiri ya kiswahili haipo?