Kufuta mtihani wa darasa la saba ni step nzuri kabisa, ila kufanya kiswahili kama medium ya kila kitu kuanzia chini hadi secondary ni kitu ambacho hata wasijaribu kufanya, tushachelewa kwenye world market, english imetawala kila kona.
Bora ngeli ianzie darasa la kwanza kabisa kwenda hadi juu, mtoto ni rahisi sana kushika lugha kuliko mtu mzima, mbona nilitupwa Kenya darasa la kwanza miaka hiyo kila mtu anaongea ngeli ndani ya miezi nikawa nawakimbiza kila somo pamoja na kwamba kila kitu kilikua kingereza..
Inawezekana sana mtoto kusoma kwa kingereza kuanzia chini kuliko kukomaa na kiswahili afu unakuja kuanza kutranslate kila terminology ukifika ngazi za juu... Ndo maana hata wanigeria wanatula kichwa, ngeli inawasaidia sana kuvuka boda hawa jamaa. Yani viongozi wa bongo, ukifikiria + wanafikiria -, ukifikiria - wanafikiria +, wako tofauti siku zote... Hii nchi niliahidi kuchukua uraia nchi nyingine endapo wataendelea na ujinga, naona wakati umekaribia.
Afu kwa nini wasiwe wanakaa na wataalam, wafanye discussions, wafanye research methods zipi zitafanya kazi... Yani wanaenda kwa kiongozi wa elimu, wanamwambia tunataka tufanye hivi, anafikiria hapohapo anatoa jibu fasta, tayari wanaandaa watu kuanza kuandika madocument ya kitakachofanywa, hamna hata kusema wafuatilie wajue njia ipi itawork.. Tunaongozwa na watu tunaowazidi akili