Kwa Mtikila kujihusisha na mambo ambayo wengine tunaamini ni mwiko kwake si ajabu. Kama kukamatwa mara nyingi, kufikishwa kwa Pilato mara kadhaa na wala hivyo vyote havijamfanya aache kueleza kila ambacho mwenyewe anaamini ni ukweli. Nadhani angefaa kuwa mwana jamiiforums aliyetukuka maana amethubutu kwa muda mrefu kujieleza peupe bila kificho - where we dare to talk openly!. Siku zilizopita aliwahi kueleza mazito zaidi kama nilivyowahi kuonjeshwa hapa chini:
=============================================================================
Mzalendo Stan Katabalo amepoteza uhai katika kumtetea mama yetu Tanganyika, alipolipua uchi wa CCM‑MAFIA wa "ACCOR" na "TAHI", kashfa za kutisha zilizopelekea mpaka kuuawa kwa shirika la WALALAHOI la UTALII kwa ajili ya mlo wa wazee wa MAFIA. Katabalo alilikalia rohoni tena genge hili, katika kuliacha uchi katika LOLIONDOGATE, mpaka akapewa onyo la kuuawa, kwa simu, eti
asiguse machafu hayo ya CCM‑MAFIA!
Katabalo amepata pigo la mauti akiwa na bomu la INDOL mkononi, ambalo limewapa "wazee" wa CCM‑MAFIA mpaka na majumba ya fahari huko Afrika Kusini! Dhambi ina nguvu kuliko haki ya Mwenyezi Mungu? La hasha! Genge la CCM‑MAFIA ni binadamu wa damu, nyama na mifupa. Damu ya Mpendwa wa Mungu Stan Katabalo inawalilia mbinguni, na Mungu asema wazi kwamba kipimo kile kile walichompimia hayati Katabalo ndicho watakachopimiwa na wao, saa wasioijua wao. Wapendwa wetu Charles Kabeho na Wilfred Mwabulambo sasa hawapo kazini kwa sababu ya maradhi yatokayo mikononi mwa CCM‑MAFIA, kwa utekelezaji wake wa MAAZIMIO YA ABUJA. Itawalazimu hawa kupata kinga na tiba ya Nguvu za Mungu kwa neema kwa njia ya imani.
Kifo cha Mheshimiwa Mbano, Mbunge wa Kigoma ni jibu la herufi kubwa la CCM‑MAFIA kwa kufunuliwa machafu ya "mzee" wa ndani wa Genge hili, ambaye nafasi yake katika "mafia" alijipatia kwa kuwa tegemeo la genge hilo kwa upande wa nguvu za giza. Mzindakaya amefikia cheo cha juu cha KUTOKOSEA katika CCM‑MAFIA, ndiyo maana hata baada ya uchafu wake kumwagwa bungeni, alizungumzia kukubali kuhamishwa, la kufukuzwa halipo. Huyu ndiye aliyehusika na yale "mauaji ya shappervile" ya Kilombero, lakini alihamishwa tu. Ndugu yetu Mbano hakuwa peke yake, hivyo wazalendo wenzake pia wanakabiliwa na kiu ya damu ya genge la CCM‑MAFIA. Ulinzi wa Mungu uwe juu yao, Amina.
Madhambi ya genge la CCM‑MAFIA ni ya kutisha na ni mengi. Taarifa za ndani zinathibitisha kuwa idara ya " Maazimio ya Abuja" inao mlolongo wa wakubwa ambao wametakiwa kuondolewa duniani, pamoja na wale wanaothubutu kuleta pingamizi katika uporaji wa "wazee" na sindiketi zao za Madawa ya Kulevya. Lakini kwa wale wote wenye wito wa kuikomboa Tanganyika na kuwaokoa WALALAHOI na vizazi vyetu vyote vijavyo, nawatia moyo kuwa mwisho wa CCM‑ MAFIA umewadia, na Mkono wa Mungu umenyooshwa juu yao.
Sasa kuliko wote walio katika orodha ya kupoteza uhai, kila mtu ameelekeza jicho lake kwa Mchungaji Christopher Mtikila, mkombozi wa WALALAHOI na jemedari mkuu wa Operasheni "OKOA MAMA TANGANYIKA". Huyu ndiye adui mkuu wa genge la CCM‑MAFIA. Mchungaji Mtikila ni mwiba wa moto mkali sana katika roho za genge hili, hasa kwa vile kutokana na ahadi ya Mwenyezi Mungu, kila silaha itakayofanyika juu yake haitafanikiwa, hata akinywa kitu cha kufisha hakitamdhuru kabisa, na kwamba kila ulimi utakaoinuka juu yake katika hukumu atahukumiwa kuwa mkosa.
Seif Shariff Hamad ni mmoja katika wale ambao kufuatana na mwana "mafia" Salmini Amour, anacho kitanzi cha CCM‑MAFIA shingoni tayari. Safari zake zote za nje na ndani zina mitego ya kila aina. Kunatafutwa uwezekano wa kupewa watumishi na hata "wafuasi" watakaothamini kiasi chochote cha fedha kuliko damu ya Hamad ili utaratibu wa kumshusha kimyani ufanikiwe. Hii ndiyo CCM‑MAFIA!
Licha ya ubeberu wote aliofanyiwa Mchungaji Mtikila na CCM‑ MAFIA, ikiwa ni pamoja na kufungwa jela, kutupwa mara kwa mara katika Magereza ya mahabusu, kutiwa mbaroni na polisi bila sababu, na mikiki mingine mingi, nguvu yake ya ukombozi iko pale pale na huzidi siku kwa siku. Mikakati yote ya rushwa, vitisho na mauaji imeshindwa kupata nafasi kwa Mchungaji Mtikila. Lakini mwaka 1988 kulikuwapo mpango kabambe wa kumwua, lakini Mungu akawa ngao yake. Mzalendo Abdalla Salum Yolero, kada wetu wa Dodoma alikataa hongo la CCM‑MAFIA la shilingi milioni 50 ili amwekee sumu "spesheli" inayoua polepole, ambayo bila shaka ndiyo iliyowamaliza wapendwa wetu Rutihinda, Kibona na wengine.
WALALAHOI karibu watashinda na Mungu yuko upande wao. CCM‑ MAFIA ni wanadamu wa damu, nyama na mifupa tu. Wamateketeza wenzao mpaka wameloa damu inayowalilia hata mbele za Mungu usiku na mchana. Kufuatana na Neno la Mungu na hata historia, huu ndio mwisho wa genge la CCM‑MAFIA. Watanganyika wamejifunza kwa uchungu sana ushetani wa CCM, na kwamba Tanganyika yao mpya inahitaji fikra mpya zisizo hata na harufu ya damu ya CCM‑MAFIA.
SAA YA UKOMBOZI NI SASA!
=========================================================================
Dawa ya mjinga ni kuumia