Mtoto aliyefariki mwaka 2017 adaiwa kufufuka

Mtoto aliyefariki mwaka 2017 adaiwa kufufuka

Idugunde

JF-Expert Member
Joined
May 21, 2020
Posts
6,404
Reaction score
6,969
Leonard Morisha (11), mkazi wa Kijiji cha Ngemo, Mbogwe mkoani Geita, aliyefariki dunia na kuzikwa Juni 27, 2017, anadaiwa kufufuka baada ya Oktoba 2020 kuonekana wilayani Kahama na wazazi wake wamempata Desemba 12, 2021 akiwa amekatwa mishipa ya ulimi na hawezi kuongea.
IMG_20211217_112658.jpg
 
#HABARI Leonard Morisha (11), mkazi wa Kijiji cha Ngemo, Mbogwe mkoani Geita, aliyefariki dunia na kuzikwa Juni 27, 2017, anadaiwa kufufuka baada ya Oktoba 2020 kuonekana wilayani Kahama na wazazi wake wamempata Desemba 12, 2021 akiwa amekatwa mishipa ya ulimi na hawezi kuongea. https://t.co/LJiMPb5A9CView attachment 2047247
Kinachofanyika ni mazingaombwe ambao wachawi wanafanya wakati wa kuzika mnaona mnamzika marehemu kumbe wanga washamchukua wanaenda kumfanyisha mikazi huko cku akitoroka huko ndyo hvyo
 
MTOTO MIAKA 11 AFUFUKA MKOANI GEITA.

Mtoto Leonard Morisha Mwenye umri wa Miaka 11 Mkazi wa kijiji na kata ya Ngemo wilaya ya Mbogwe Mkoani Geita aliyefariki June 27 ,2017 katika hospitali ya Geita amefufuka baada ya kuzikwa kwa kipindi cha miaka 5 mpaka kufufuka kwake huku ikidaiwa kukatwa ulimi.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita, Kamishina Henry Mwaibambe amesema mtoto huyo alionekana usiku katika kijiji cha Segese kata ya Msalala wilaya ya kahama akiwa anaranda randa katika Maduka.

Kamanda amesema mtoto huyo baada ya kuonekana katika Maduka hayo alikuwepo mlinzi katika Maduka hayo aitwae Emmanuel Busiga alimchukua na kumpeleka kwao badae alifikisha taarifa katika uongozi wa kijiji.

"Mtoto huyo ana afya njema lakini baada ya kufanyiwa uchunguzi katika kituo cha afya cha Masumbwe alibainika kukatwa ulimi kwa kiwango kikubwa mishipa ya ulimi wake na kusababisha ashindwe kuongea, " Mwaibambe.

Mwaibambe amesema baada ya kupata taarifa hizo Jeshi la polisi lilipata kibali kutoka katika Mahakama kwa ajili kufukuwa kaburi lake ambalo mtoto huyo alikuwa kazikwa na kukuta kaptura pamoja na suruali ya Baba mzazi wake aliyefariki mwaka 2019.

#KitengeUpdates
maulidkitenge-20211217-0001.jpg
 
Kichwa cha habari "MTOTO MIAKA 11 AFUFUKA MKOANI GEITA"

content "mtoto huyo alionekana usiku katika kijiji cha Segese kata ya Msalala wilaya ya kahama akiwa anaranda randa katika Maduka."

Mtoto kumbe alikua misele, we unapotosha unasema kafufuka
 
MTOTO MIAKA 11 AFUFUKA MKOANI GEITA.

Mtoto Leonard Morisha Mwenye umri wa Miaka 11 Mkazi wa kijiji na kata ya Ngemo wilaya ya Mbogwe Mkoani Geita aliyefariki June 27 ,2017 katika hospitali ya Geita amefufuka baada ya kuzikwa kwa kipindi cha miaka 5 mpaka kufufuka kwake huku ikidaiwa kukatwa ulimi.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita, Kamishina Henry Mwaibambe amesema mtoto huyo alionekana usiku katika kijiji cha Segese kata ya Msalala wilaya ya kahama akiwa anaranda randa katika Maduka.

Kamanda amesema mtoto huyo baada ya kuonekana katika Maduka hayo alikuwepo mlinzi katika Maduka hayo aitwae Emmanuel Busiga alimchukua na kumpeleka kwao badae alifikisha taarifa katika uongozi wa kijiji.

"Mtoto huyo ana afya njema lakini baada ya kufanyiwa uchunguzi katika kituo cha afya cha Masumbwe alibainika kukatwa ulimi kwa kiwango kikubwa mishipa ya ulimi wake na kusababisha ashindwe kuongea, " Mwaibambe.

Mwaibambe amesema baada ya kupata taarifa hizo Jeshi la polisi lilipata kibali kutoka katika Mahakama kwa ajili kufukuwa kaburi lake ambalo mtoto huyo alikuwa kazikwa na kukuta kaptura pamoja na suruali ya Baba mzazi wake aliyefariki mwaka 2019.

#KitengeUpdatesView attachment 2047442
Naomba unieleweshe;
-alizikwa akiwa na miaka 11?
-na baada ya miaka 5 amefufuka.Je,muonekano(umri)ni uleule wa miaka 11 au amebadilika na kuwa wa miaka 16?
Akili yangu nyembamba imekwama kuelewa hapo.
 
Back
Top Bottom