Mtoto mdogo aliepotea Mbeya tangu 2020 anaedhaniwa aliibwa imebainika yupo Songwe kupitia group la Facebook, wazazi wapo kwenye harakati kumrudisha

Mtoto mdogo aliepotea Mbeya tangu 2020 anaedhaniwa aliibwa imebainika yupo Songwe kupitia group la Facebook, wazazi wapo kwenye harakati kumrudisha

sky soldier

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2020
Posts
5,407
Reaction score
19,264
295603812_579824356963918_1370502500649432863_n.jpg


295250773_579824306963923_6592675010963469012_n.jpg




Ilikuwa ni tarehe 21-11-2020 siku ya Jumamos ambapo mtoto Nassir Jumanne mande mwangopola alipotea Chunya mjini, moja ya wilaya ya Mbeya.

Wazazi wa mtoto, baba yake Jumanne Mwangopola na mama yake Shamimu Shabani walifanya jitihada kubwa kumtafuta lakini jitihada hazikuzaa matunda.

Leo hii kupitia group maarufu la facebook la Mbeya, kuna mdau aliifowadi post ambayo aliiona kwa mtu anaeishi maeneo ya Tunduma mitaa ya Majengo, aliweka post kwamba kuna mtoto aliwahi kuja karibu na sehemu anayoishi na alikuwa harusiwi kutoka, ni mpaka hivi karibuni ndio alianza kuruhusiwa kutoka na akagundua ni mtoto anaetafutwa.

Kwa bahati nzuri wazazi wa mtoto ni wanachama wa hiki kikundi na walipoiona hio post kwa wakapeana mawasiliano na mtu aliefowadi,

Kuhusu kilichoendelea mpaka sasa hakijulikani ila huenda siku za karibuni tukajua
 

Attachments

  • 278804716_3148060918815653_316908319830750695_n.jpg
    278804716_3148060918815653_316908319830750695_n.jpg
    47.3 KB · Views: 9
Intelijensia yetu itafanyia kazi. Ata huyo mwana Mbeya Yetu atasaidia jeshi.
 
Intelijensia yetu itafanyia kazi. Ata huyo mwana Mbeya Yetu atasaidia jeshi.
kuna mambo mengi nyuma ya pazia, Huenda hata huyo mama anaeishi nae ni bibi yake aliona amlee mjukuu mwenyewe.

ila kama mtoto aliibiwa basi nadhani atasaidia kufichua huo mtandao
 
Intelijensia yetu itafanyia kazi. Ata huyo mwana Mbeya Yetu atasaidia jeshi.
Ni habari ya matumaini sana, sasa nenda polisi kuwataarifu juu ya tukio hili ili waweze kumdhibiti mama huyo kabla hajafanya njama yoyote; maana anaweza kumtorosha au kumfanya lolote ili kupoteza ushahidi. Fanya hima na Mungu amsimamie mtoto huyu.
 
kuna mambo mengi nyuma ya pazia, Huenda hata huyo mama anaeishi nae ni bibi yake aliona amlee mjukuu mwenyewe.

ila kama mtoto aliibiwa basi nadhani atasaidia kufichua huo mtandao

Unakuta mwanaume aliona mtu aliyezalisha nae hawezi toa malezi bora kwa mtoto. Akabeba mtoto na kupeleka kwa mwanamke anayemwamini.

Ngoja tuone ili swala linaishaje
 
Unakuta mwanaume aliona mtu aliyezalisha nae hawezi toa malezi bora kwa mtoto. Akabeba mtoto na kupeleka kwa mwanamke anayemwamini.

Ngoja tuone ili swala linaishaje
Kwa jinsi baba alivyojibu sidhani (but maybe)

1658865029745.png
 
Niliona hii taarifa , nilisikitika sana. Better kama mtoto kapatikana
 
Kuna mmoja alipotea akiwa darasa la saba dar nilisoma habari yake gazeti la mwananchi,mwaka wa nne natamani kufahamu kama alipatikana daah
 
Back
Top Bottom