Mtoto Rayan aliyetumbukia kwenye kisima huko Morocco amefariki dunia

Mtoto Rayan aliyetumbukia kwenye kisima huko Morocco amefariki dunia

chizcom

JF-Expert Member
Joined
Jul 31, 2016
Posts
8,680
Reaction score
18,035
Ni habari ambayo imeleta simanzi sana kwa wazazi wake na hata watu waliokuwa wanafatilia habari kuhusu mtoto aliyekuwa anacheza pembeni na maeneo ya kisima kirefu na kudumbukia.

Kujulikana kama alikuwa kwenye kisima ni baada ya baba yake kumtafuta sana na kuja kugundua yupo kwenye kisima.

Mamia ya watu na juhudi za serikali zilijitolea usiku na mchana kuokoa uhai wa mtoto ndani ya siku tano.
urefu wa kisima ulikuwa na umbali na mazingira ya udongo yalikuwa si mazuri
IMG_4448.jpg

IMG_4462.jpg
 
Ni habari ambayo imeleta simanzi sana kwa wazazi wake na hata watu waliokuwa wanafatilia habari kuhusu mtoto aliyekuwa anacheza pembeni na maeneo ya kisima kirefu na kudumbukia.
kujulikana kama alikuwa kwenye kisima ni baada ya baba yake kumtafuta sana na kuja kugundua yupo kwenye kisima.

mamia ya watu na juhudi za serikali zilijitolea usiku na mchana kuokoa uhai wa mtoto ndani ya siku tano.
urefu wa kisima ulikuwa na umbali na mazingira ya udongo yalikuwa si mazuri View attachment 2109568
View attachment 2109570
25 cm wide amepita vipi kwenye upana kama huo? Maana haufiki hata urefu wa rula ile ndefu.
 
Ni habari ambayo imeleta simanzi sana kwa wazazi wake na hata watu waliokuwa wanafatilia habari kuhusu mtoto aliyekuwa anacheza pembeni na maeneo ya kisima kirefu na kudumbukia.
kujulikana kama alikuwa kwenye kisima ni baada ya baba yake kumtafuta sana na kuja kugundua yupo kwenye kisima.

mamia ya watu na juhudi za serikali zilijitolea usiku na mchana kuokoa uhai wa mtoto ndani ya siku tano.
urefu wa kisima ulikuwa na umbali na mazingira ya udongo yalikuwa si mazuri View attachment 2109568
View attachment 2109570
Wakati wa ajali ya Mv nyerere, mongela akiwa mkuu wa mkoa aliwaambia waokoaji giza limeingia waondoke watakuja kesho. As if waathirika nao wangebana pumzi hadi asubuhi.
 
Inauma jamani. Chanzo ni umaskini,shida ya maji inapelekea wachimbe visima virefu. Hizi accident ni nyingi sana pande hizo za jangwa. Ila pia wana watoto wadogo walitakiwa wasiache hata secunde moja hole ikiwa haina security. Hata kuzungushia miiba tu. R.I.P Rayan.
 
Ni upana mdogo for sure, labda mtoto alikuwa mwembamba sana...average shoulder to shoulder distance kwa mtoto wa umri huo huwa ni 30cm +
Shimo lilikuwa na upana wa inchi 18 tu kwa juu lakini kwa Chini lilikuwa Finyu sana, Dogo hakufika mwisho wa shimo kabisa alikwama umbali wa Mita 30 (futi 100) kwenda Chini na hakufikia maji. Shimo lote Lina urefu wa Mita 150 kwenda Chini.
 

Rayan: Mvulana wa Morocco aliyetumbukia kisimani afariki​

Saa 3 zilizopita
Rayan's parents leaving the scene after their son's body is taken away by ambulance

CHANZO CHA PICHA,EPA
Maelezo ya picha,
Wazazi wa Rayan wakiondoka eneo la tukio baada ya mwili wa mtoto wao wa kiume kupelekwa kwa ambilansi
Mvulana mwenye umri wa miaka mitano aliyeanguka kwenye kisima kirefu kwa siku nne amefariki, licha ya juhudi za kumuokoa.
Taarifa ya ufalme wa Morocco ilitangaza kifo mara ya baada ya mvulana huyo kuondolewa kwenye shimo.
Juhudi za kumuokoa mvulana huyo, anayeitwa Rayan, zilifuatiliwa kote nchini, huku mamia ya watu wakikusanyika kwenye shimo na maelfu zaidi wakifuatilia shuguli ya uokozi ,kupitia mtandao.
Mvulana huyo alitumbukia katika iisma cha urefu wa mita 32 (futi104) , licha ya kwamba shimo hilo lilikuwa jembamba . Uokoaji ulitatizwa na hofu ya kuporomoka kwa ardhi juu ya shimo hilo.
Hatimaye waokoaji walimeta nje mvulana Jumamosi jioni.
Hakuna taarifa iliyotolewa kuhusu hali yake wakati huo, na uokoaji huo ulishangiliwa na umati wa watu.
Kwenye mitandao ya kijamii, watu walitumia msema wa alama ya leri- hashtag #SaveRayan,ambayo imekuwa ikisambaa kote nchini humo na nje ya mipaka ya nchi hiyo, huku watu wakielezea kufurahishwakuokolewa kwa mvulana huyo.
Lakini iligeuka kuwa dakika za kuvugunja moyo wakati taarifa ilipotangazwa kwamba Rayan alifariki.
Watumiani wa Twitter baadaye walianza kutoa salama zao za rambirambi na kuelezea huzuni kwa kutumia alama sawa ya leri.
"Kufuatia ajali ya mtoto Rayan Oram, Mfalme Mohammed VI aliwaita wazazi wamvulana aliyefariki baada ya kutumbukia ndani ya shimo " taarifa ya kasri ya rais ilisema.
Siku ya Jumamosi, vyombo vya habari viliripoti kwamba waokoaji walikuwa mita 1.8 kutoka alipokuwa mvulana huyo.
"Tumekaribia," mmoja wa viongozi wa operesheni hiyo, Abdesalam Makoudi, alisema Ijumaa mchana.
"Tumekuwa tukifanya kazi bila kukoma kwa siku tatu na uchovu unaanza, lakini timu nzima ya uokoaji bado iko hapa inaendelea na kazi."
Wakiongozwa na Kurugenzi ya Ulinzi wa Raia wa Morocco, shughuli za uokoaji katika mji mdogo wa kaskazini wa Tamorot, karibu kilomita 100 (maili 62) kutoka mji wa Chefchaouen, zilianza tangu Jumanne jioni.
Barabara zinazozunguka mji huo zilijaa magari na mabasi, huku maelfu wakishangilia waokoaji katika eneo la tukio.
People watch as Moroccan emergency services teams work on the rescue of five-year-old boy Rayan from a well shaft he fell into

CHANZO CHA PICHA,AFP
Maelezo ya picha,
Watu walikusanyika kutazama shughuli ya kumuokoa kijana hiyo inavyoendelea siku ya Jumamosi
'Sijalala kabisa'
Baba yake Rayan alikuwa akitengeneza kisima wakati wa ajali hiyo inatokea, na alisema yeye na mama yake Rayan walikuwa "wamefadhaika na wenye wasiwasi mwingi."
"Katika muda huo, nilikuwa nimeondoa macho yangu kwake kidogo tu, nahapo ndipo alipoanguka kisimani. Sijafumba hata jicho tangu mwanangu alipotumbukia," aliambia tovuti ya habari ya le360 siku ya Jumatano.
Akiongea na vyombo vya habari vya Morocco huku akibubujikwa na machozi, mama yake Rayan alisema: "Familia nzima ilitoka kumtafuta. Kisha tukagundua kuwa alikuwa ameanguka chini ya kisima. Bado nina matumaini kwamba tutampata akiwa hai."
Picha za Alhamisi kutoka kwa kamera iliyoshushwa kisimani zilionyesha kuwa mvulana huyo alikuwa hai na ana fahamu, ingawa alionekana kuwa na majeraha madogo kichwani.
Wafanyakazi wa uokoaji wameshusha barakoa ya oksijeni, chakula na maji ndani ya kisima na timu ya matibabu pia iko kwenye eneo la tukio, tayari kumtibu mvulana huyo.
Helikopta pia imefika eneo la tukio ili kumpeleka hospitali mara baada ya kutolewa kutoka kisimani.
......
SIJUI INGEKUWAJE HAPA NYUMBANI KWETU NAONA NI KAMA KABURI LINGEWEKWA KWA JUU TU..

_123146516_gettyimages-1238198639-1.jpg


_123141254_boy_well_morrocco_640x2-nc.png


Screenshot_20220206-123013_Video Player.jpg


Screenshot_20220206-005111_Instagram.jpg
 
Back
Top Bottom