Mtoto wa kike wa miaka 9 kulala na babake

Umri sio akili huyo mtoto ni mkubwa kiumri ila akili yake bado ya mtoto mdogo ndio maana haoni tatizo, wangu ana miaka nane ila chumbani kwao nikienda lazima nipige hodi na muda mwingine ananikatalia kuingia, amejifunza sababu kuna chumba cha watoto wa kike na cha watoto wa kiume na chumba cha wazazi, kila chumba kinaheshimiwa.
Hapo watoto wako wawili tu likizo mpelekeni nyumba yenye watoto wengine atajifunza pia kwa kuona wengine wanaishije, anavyoendelea kukua ataelewa tu. Ukaribu wa mzazi na mtoto sio tatizo awe wa jinsia yoyote sema tu heshima inatakiwa iwepo na mipaka iwepo, mumeo pia asie tu humble kwa mtoto kuna muda mtoto ajue nani baba na nani mama, kumbuka sisi ni wa Afrika tunaasili yetu hata uishi maisha ya kizungu siku zote mjasiri aachi asili ni vyema kutazama hilo pia
 
Uttarra,
Wazo la kuachwa au kuachana uliondoe hapo mnaonekana mnafit, ila jambo la msingi ni kuongea na kumshauri baba wa mtoto ndiyo yeye atumike zaidi kumfanya aache kulala naye, na wewe cheza sehemu yako kama mama yake kwa sasa kuonyesha upendo wa hali ya juu kujua nini anapenda nje na kupenda kulala na baba yake ndiyo umkamatie hapo ili upendo wake kwako uwe mkubwa na kukuamini.
Kingine ni kumshirikisha MUNGU tu.
Hakuna jambo gumu mbele ya MUNGU lenye nia nzuri.
 
Malezi ni kitu kikubwa sana cha kujifunza na ni muendelezo wa maisha
Kuna watu wanaandaa chumba cha mtoto kabla hajazaliwa na siku akizaliwa ana chumba chake hii nimeona kwa wazungu akinyonya na kushiba anapelazwa chumba chake.
Kwa sisi mtoto akifika miaka 7 lazima atengwe hata na kaka yake
Na kuanza kufundishwa sala na maadili mengine
Mtoto lazima awe independently na kuanza kujiamini na kuishi maisha yake kujisafisha na kufanya mengi peke yake kwa msaada wa mama
Hajachelewa lakini lazima alale peke yake
 
Eti mama wa kambo dah humu jf raha sana wajameni nimecheka mpaka dareva wa mwendo kasi kasimamisha gali eti
 
Embu tuache utani uyo mtoto ameshakuwa mkubwa sana fanyeni mchakato alale chumba chake mana asije akajifunza vitu vya ajabu
 
Solution huyo mtoto apelekwe boarding school naamini huko atajua kujitegemea mwenyewe
 
Mimi nimeacha kulala na wazazi nani mi 4 halafu wala hatuna luxury things eti urembewe chumba ili uvutiwe ukalale huko.
 
MTAENDELEA KUENDELEZA KIZAZI CHA USINGLE PARENT NILIVYOSOMA TU PARAGRAPH YA KWANZA NIKAJUA USINGLE PARENT PART TWO UNATOKEA, BUT INABIDI UJADILI NA SINGLE PARENT MWENZANKO MFUNGE NDOA KWANZA MJENGE EMPIRE YENU #. USHAURI WA BURE
 
MTAENDELEA KUENDELEZA KIZAZI CHA USINGLE PARENT NILIVYOSOMA TU PARAGRAPH YA KWANZA NIKAJUA USINGLE PARENT PART TWO UNATOKEA, BUT INABIDILI UJADILI NA SINGLE PARENT MWENZANKO MFUNGE NDOA KWANZA MJENGE EMPIRE YENU #. USHAURI WA BURE
wakuu,mmegoma kulala au mko USA nin?
 
Joti kanichekesha juzi kati wakati nipo youtube kapotray kama single mother dahhh TINNIE WHITE KULA SANA MAKOFI KAIGIZA DIZAINI ILE YA MADEMU WA USWAZI KILA MTOTO ANA BABA YAKE HAHAHAH DAH NACHEKA KAMA VIZURI HIVI ILA ITS A TRUE REALITY NA TATIZO LA WANAWAKE WENGI WANAPENDWA KUDANGAMYWA UKIMWAMBIA NAKUPENDA AHHH SIJUI HIVI SIJUI VILE AKIDANGANYWA ANAJAA MIMBA IYO DAH WABADILIKE WAACHE TAMAA ILA NDIO IVYO HAWAJITAMBUI WENGI WAO WANAJITAMBUA MTOTO AKISHAZALIWA
wakuu,mmegoma kulala au mko USA nin?
Bongo hii hii shida nini mkuu?
 
Watoto wa kike Wanakuwa attracted na baba vivyo hivyo watoto wa kiume wanavitiwa na kuwa karibu na mama, hii ni psychology tu, hizi hisia Huwa zinaisha katika umri huo wa Mika kabla ya balehe/ kuvunja ungo, na mtoto anakuwa na wivu balaa , huyo Binti atakuwa anakuona nuksi kabisa pindi upo na baba yake, fanyeni mpango aanze kulala peke yake maana anakaribia kubalehe huyo na sisi wanaume tuna udhaifu mkubwa yasije yakatokea majanga halafu mkajilaumu, Yaani atake asitake iwe Kwa diplomasia ama Kwa amri akalale peke yake , hata akilia chapa fimbo akalale peke yake hautakuwa unamuonea Bali unamsaidia, mtoto hapaswi kabisa kuchungulia tupu ya MZAZI wake, baba anaweza kurudi kalewa halafu akajiachia mambo ni mengi
 
mkuu umeangalia kwanza ni post ya mwaka gani?:si ajabu sahv huyo bint yuko form2
 
Sio kutubana tu, pia anatakiwa kujitegemea. Kulala peke yake ni moja ya hatua katika kuendea kujitegemea. Una ushauri wowote?
nadhani akipevuka atajitenga automatical.

Ila pia baba yake ndo wakuanza kumzoesha tabia za independence… aanze kumjenga kisaikolojia kisha vitendo vifuatie.

Ukiangalia wazungu mtoto mchanga anaanza kulala kwenye kitanda cha pekee yake akiwa mchanga kabisa. Mama ananyonyesha kisha anamwacha kwenye kakitanda kake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…