Mtoto wa Museveni ana ajenda gani ya siri dhidi ya nchi za EAC?

Mtoto wa Museveni ana ajenda gani ya siri dhidi ya nchi za EAC?

Dat4

Member
Joined
Aug 24, 2022
Posts
96
Reaction score
148
Mkuu wa zamani wa Jeshi la Ardhini la Uganda Muhoozi Kainerugaba ambaye pia ni Mtoto wa Rais wa Uganda Yoweri Museveni, leo October 19,2022 amerejea tena kauli yake ya kuwahamiza Vijana wa Afrika Mashariki kuunga mkono hoja yake ya kutaka Nchi za Afrika Mashariki ziungane na kuwa Taifa moja.

“Vijana wenzangu wa Afrika, nikiwa kama Kiongozi wenu ambaye mmenichagua wenyewe, nawahimiza kuuona umuhimu wa kushinikiza kwa haraka muungano wa Nchi za Afrika Mashariki, huu ni mpango wetu mdogo wa kisiasa, mipango mingine nitawapa mwongozo”

Itakumbukwa October 04,2022 Muhoozi alisema ameongea na Baba yake Rais Museveni kuhusu mpango wa kuifanya Afrika Mashariki kuungana na akasema mipaka iliyopo iliwekwa na Wakoloni na hakuna haja ya kuendelea kuiacha badala yake Nchi za Afrika Mashariki zinapaswa kuifuta mipaka hiyo na kutengeneza Taifa moja huku akisema Afrika Mashariki ikiwa Taifa moja anapendekeza Baba yake Museveni ndiye awe Rais wa Muungano huo.

Kauli ya Muhoozi inakuja siku mbili tu tangu Baba yake Rais Museveni aseme amemzuia Mtoto wake kuzungumzia Mataifa mengine au kuongelea siasa kupitia akaunti yake ya Twitter lakini jana Muhoozi alijibu kwamba yeye ni Mkubwa (sio Mtoto) na hakuna yoyote anayeweza kumpangia cha kufanya.

Credit: Millard Ayo UPDATES
 
Wawekeze kwanza kwenye kujifunza ambayo itakuwa lugha ya taifa hilo. Yani Kiswahili.
 
Bangi zimemchanganya akili.
Sio kweli. Mataifa mengi tu yanaitamani ardhi ya Tanzania. Tungekuwa dhaifu, Idd Amini, angeimega, Malawi nao walikuwa wanapambana kuimega..
Na mataifa mengine ambayo nisingependa kuyataja.
Wakati sie hapa Tz tunalala usingizi, wengine wanakesha wakiwaza watawezaje kuwa sehemu ya Tanzania!
 
Wanachaguana chumbani yeye na mzee wake, nani kamchagua hapa africa vyeo vyote hivyo vya kupewa sebuleni🤓
 
Mkuu wa zamani wa Jeshi la Ardhini la Uganda Muhoozi Kainerugaba ambaye pia ni Mtoto wa Rais wa Uganda Yoweri Museveni, leo October 19,2022 amerejea tena kauli yake ya kuwahamiza Vijana wa Afrika Mashariki kuunga mkono hoja yake ya kutaka Nchi za Afrika Mashariki ziungane na kuwa Taifa moja.

“Vijana wenzangu wa Afrika, nikiwa kama Kiongozi wenu ambaye mmenichagua wenyewe, nawahimiza kuuona umuhimu wa kushinikiza kwa haraka muungano wa Nchi za Afrika Mashariki, huu ni mpango wetu mdogo wa kisiasa, mipango mingine nitawapa mwongozo”

Itakumbukwa October 04,2022 Muhoozi alisema ameongea na Baba yake Rais Museveni kuhusu mpango wa kuifanya Afrika Mashariki kuungana na akasema mipaka iliyopo iliwekwa na Wakoloni na hakuna haja ya kuendelea kuiacha badala yake Nchi za Afrika Mashariki zinapaswa kuifuta mipaka hiyo na kutengeneza Taifa moja huku akisema Afrika Mashariki ikiwa Taifa moja anapendekeza Baba yake Museveni ndiye awe Rais wa Muungano huo.

Kauli ya Muhoozi inakuja siku mbili tu tangu Baba yake Rais Museveni aseme amemzuia Mtoto wake kuzungumzia Mataifa mengine au kuongelea siasa kupitia akaunti yake ya Twitter lakini jana Muhoozi alijibu kwamba yeye ni Mkubwa (sio Mtoto) na hakuna yoyote anayeweza kumpangia cha kufanya.

Credit: Millard Ayo UPDATES
Muhoozi ni taswira ya nidhamu ya jeshi la Uganda.

Hapo mkiangakia mtu na aba yake mnakosea. Hapo ni mwanajeshi na Amiri Jeshi Mkuu.

Siasa za afrika zina ufala mwingi sana
 
Mkuu wa zamani wa Jeshi la Ardhini la Uganda Muhoozi Kainerugaba ambaye pia ni Mtoto wa Rais wa Uganda Yoweri Museveni, leo October 19,2022 amerejea tena kauli yake ya kuwahamiza Vijana wa Afrika Mashariki kuunga mkono hoja yake ya kutaka Nchi za Afrika Mashariki ziungane na kuwa Taifa moja.

“Vijana wenzangu wa Afrika, nikiwa kama Kiongozi wenu ambaye mmenichagua wenyewe, nawahimiza kuuona umuhimu wa kushinikiza kwa haraka muungano wa Nchi za Afrika Mashariki, huu ni mpango wetu mdogo wa kisiasa, mipango mingine nitawapa mwongozo”

Itakumbukwa October 04,2022 Muhoozi alisema ameongea na Baba yake Rais Museveni kuhusu mpango wa kuifanya Afrika Mashariki kuungana na akasema mipaka iliyopo iliwekwa na Wakoloni na hakuna haja ya kuendelea kuiacha badala yake Nchi za Afrika Mashariki zinapaswa kuifuta mipaka hiyo na kutengeneza Taifa moja huku akisema Afrika Mashariki ikiwa Taifa moja anapendekeza Baba yake Museveni ndiye awe Rais wa Muungano huo.

Kauli ya Muhoozi inakuja siku mbili tu tangu Baba yake Rais Museveni aseme amemzuia Mtoto wake kuzungumzia Mataifa mengine au kuongelea siasa kupitia akaunti yake ya Twitter lakini jana Muhoozi alijibu kwamba yeye ni Mkubwa (sio Mtoto) na hakuna yoyote anayeweza kumpangia cha kufanya.

Credit: Millard Ayo UPDATES
Asikusumbue He is blocked Mentally.
 
Kipi kibaya au kipya hapo amekisema huyo mtoto wa Museven?
Suala la nchi za Afrika kutakiwa kuungana ndio wazo lililokuwepo tangu miaka ya 1960s tena likipiganiwa na kina Nyerere, Kwame Nkuruma, Nelson Mandela, Kenneth Kaunda, Patrice Lumumba. Kipi cha ajabu?

Lengo la Afrika kuwa nchi moja lilipoletwa upya miaka ya 2000s na rais wa Libya (Ghadaf) mbona wengi tuliliona la kishujaa. Kwanini leo likisemwa na mtoto wa Museven tunaona ni ukichaa?

Lengo la uwepo wa Jumuiya ya Afrika mashariki kihistoria lilikuwa ni kuja na nchi mmoja katika ukanda huu. Nini kipya au Kipi cha ajabu?

Kuna ubaya gani kwa yeye kutoa maoni yake kuhusu baba yake kufaa kuwa rais wa Afrika mashariki ikiwa nchi za ukanda huu zikiungana? Nyinyi mnataka Samia, Kagame, Ruto au nani aje awe rais?
 
Back
Top Bottom