Mtoto wa umri gani anapaswa kuvaa barakoa?

Mtoto wa umri gani anapaswa kuvaa barakoa?

Status
Not open for further replies.

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Joined
Aug 7, 2018
Posts
685
Reaction score
1,124
0001-17768990505_20210304_103325_0000.png


Watoto wenye umri wa miaka 5 kushuka chini hawatakiwi kuvaa barakoa

Hii ni kwa sababu ya usalama na uwezo wa mtoto kutumia barakoa ipasavyo bila msaada wa mtu mzima.

WHO na UNICEF wanashauri kwamba uamuzi wa kutumia barakoa kwa watoto wenye umri wa miaka 6-11 unapaswa kuzingatia mambo yafuatayo:

Ikiwa kuna maambukizi mengi katika eneo analoishi mtoto

Uwezo wa mtoto kutumia barakoa kwa usalama na ipasavyo

Usimamizi wa kutosha wa watu wazima na maelekezo kwa mtoto juu ya jinsi ya kuvaa na kuvua barakoa

Mwingiliano wa mtoto na watu wengine ambao wako katika hatari kubwa ya kupata ugonjwa wa Korona, kama vile wazee na wale walio na matatizo mengine ya kiafya.

Aidha inashauriwa kwamba watoto wenye umri wa miaka 12 na zaidi wanapaswa kuvaa barakoa kama watu wazima, haswa katika mazingira ambayo hawawezi kuhakikisha umbali wa mita 1 kutoka kwa wengine
 
Upvote 0
Asante,, watoto wanakosa kupumua kwanza wanazitafuna njaa ikiwauma.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom