Mtu akifa anaenda wapi?

Mtu akifa anaenda wapi?

Alipomwambia yule muuaji msalabani, Leo hii utakuwa nami Mahali pema peponi, unaamini huko peponi hawatambuani?
Kwa nini siku mbili baadaye, wakati wa ufufuo, Yesu akathibitisha kwamba hakuwa amepaa kwenda kwa Baba (Yohana 20:17)?

Au huko peponi ni wapi asipokuwepo Baba?

Musa na Elia walipomtokea Yesu mlimani wakimtia moyo, ulidhani yalikuwa maigizo Yale?
Kwa maelezo yako, alikuwepo Eliya (mwili na roho) na Musa (roho)? Maana Eliya yeye hakufa.

Kwa taarifa Yako, Musa na Elia na Manabii wote wa AGANO la kale wa Mungu, wapo Mbinguni,
Kulikuwa na sababu gani basi ya manabii kama akina Ayubu, Danieli na kadhalika kutazamia siku ya ufufuo kama tumaini lao pekee?

Maana kama roho iko mbinguni tayari, kwa nini wasingeshangilia kwamba mara tu baada ya mauti yao wangeonana na Mungu uso kwa uso?

WATAKATIFU wote wafao katika Mungu baada ya kufufuka Yesu, wako Mbinguni. Hawakai tena Mahali pa kusubiri.
^Strange fire!^

MTU ni ROHO, anayo NAFSI na anaishi ndani ya MWILI.

Mtu Hafi, anabadili form, mwili ndio unaokufa na kuoza,
^Strange fire!^

Mtu aliumbwa kuishi milele,mtenda dhambi ukifa(ukibadili form) utateswa milele, mtakatifu ukibadili form( ukifa) unafurahia maisha milele.
^Strange fire!^

kuzaliwa duniani ni bahati hasa kuzaliwa binadamu so ishi dunia hapa ndo peponi hakuna sehemu utaenda ukifa zingne story za vijiweni
Kama hakuna ufufuo, kuna bahati gani kuwepo duniani? Mbona unajichanganya?

Maisha yana chanzo na kusudi.

Au uniambie mwanadamu chanzo chake nini? (Tuchukulie kwamba Mungu hayupo).
 
Kwa nini siku mbili baadaye, wakati wa ufufuo, Yesu akathibitisha kwamba hakuwa amepaa kwenda kwa Baba (Yohana 20:17)?

Au huko peponi ni wapi asipokuwepo Baba?


Kwa maelezo yako, alikuwepo Eliya (mwili na roho) na Musa (roho)? Maana Eliya yeye hakufa.


Kulikuwa na sababu gani basi ya manabii kama akina Ayubu, Danieli na kadhalika kutazamia siku ya ufufuo kama tumaini lao pekee?

Maana kama roho iko mbinguni tayari, kwa nini wasingeshangilia kwamba mara tu baada ya mauti yao wangeonana na Mungu uso kwa uso?


^Strange fire!^


^Strange fire!^


^Strange fire!^


Kama hakuna ufufuo, kuna bahati gani kuwepo duniani? Mbona unajichanganya?

Maisha yana chanzo na kusudi.

Au uniambie mwanadamu chanzo chake nini? (Tuchukulie kwamba Mungu hayupo).
Lazima uwe na upeo mkubwa kidogo kuelewa dunia pia sio wote mtaielewa dunia
 
hakuna NAFSI, hakuna ROHO,...kama vingekuwepo, basi tungelikuwa na kumbukumbu ya wapi tulikuwepo kabla HATUJAZALIWA...kwa ufupi hizo ni stori tu za kuendelea kuwashika WAJINGA...kule anakoenda Sisimizi au Mbuzi baada ya kufa ndiko mwanadamu aendako pia, mwanadamu huna u-special wowote zaidi ya kuwazidi viumbe wengine UJINGA tu...
 
Kwa nini siku mbili baadaye, wakati wa ufufuo, Yesu akathibitisha kwamba hakuwa amepaa kwenda kwa Baba (Yohana 20:17)?

Au huko peponi ni wapi asipokuwepo Baba?


Kwa maelezo yako, alikuwepo Eliya (mwili na roho) na Musa (roho)? Maana Eliya yeye hakufa.


Kulikuwa na sababu gani basi ya manabii kama akina Ayubu, Danieli na kadhalika kutazamia siku ya ufufuo kama tumaini lao pekee?

Maana kama roho iko mbinguni tayari, kwa nini wasingeshangilia kwamba mara tu baada ya mauti yao wangeonana na Mungu uso kwa uso?


^Strange fire!^


^Strange fire!^


^Strange fire!^


Kama hakuna ufufuo, kuna bahati gani kuwepo duniani? Mbona unajichanganya?

Maisha yana chanzo na kusudi.

Au uniambie mwanadamu chanzo chake nini? (Tuchukulie kwamba Mungu hayupo).
Elia hakufa, Musa alikufa,

Nami nikuulize, ikiwa ukifa habari ndio inaishia pale,

Waliokuwa wakiongea na YESU mlimali ni akina nani?
 
hakuna nafsi, hakuna roho,...kama vingekuwepo, basi tungelikuwa na kumbukumbu ya wapi tulikuwepo kabla hatujazaliwa...kwa ufupi hizo ni stori tu za kuendelea kuwashika wajinga...kule anakoenda Sisimizi au Mbuzi baada ya kufa ndiko mwanadamu aendako pia mwanadamu huna u-special wowote zaidi ya kuwazidi viumbe wengine UJINGA...
Usizidiwe Maarifa na wachawi,

Ikiwa Roho na NAFSI hazipo, wachawi hutumia nini kupaa angani, wanawezaje kutumia ungo mmoja kukaa watu zaidi ya 20 na wakasafiri bila shida yoyote?

Mtafute Mungu, tafuta Maarifa, utakuwa msindikizaji na mtumwa wa Ibilisi Hadi lini?
 
Usizidiwe Maarifa na wachawi,

Ikiwa Roho na NAFSI hazipo, wachawi hutumia nini kupaa angani, wanawezaje kutumia ungo mmoja kukaa watu zaidi ya 20 na wakasafiri bila shida yoyote?

Mtafute Mungu, tafuta Maarifa, utakuwa msindikizaji na mtumwa wa Ibilisi Hadi lini?
Unaweza nilitea picha ya wachawi 20, wakiwa kwenye ungo?......Munaweza kupaa na ungo tu,ila bado munatibiwa maralia kwa msaada wa watu wa Marekani..?..

WAAFRIKA ACHENI IMANI ZA KIPUMBAVU....
 
Unaweza nilitea picha ya wachawi 20, wakiwa kwenye ungo?......Munaweza kupaa na ungo tu,ila bado munatibiwa maralia kwa msaada wa watu wa Marekani..?..

WAAFRIKA ACHENI IMANI ZA KIPUMBAVU....
Kazi ipo
 
Unaweza nilitea picha ya wachawi 20, wakiwa kwenye ungo?......Munaweza kupaa na ungo tu,ila bado munatibiwa maralia kwa msaada wa watu wa Marekani..?..

WAAFRIKA ACHENI IMANI ZA KIPUMBAVU....
Nenda kamuulize mama Yako alipokuzaa, kitovu chako alipokikata alikitunza wapi ndipo uje useme Ulimwengu wa Nuru na Giza ni story!!

Siku utakapolala umefunga milango na ukaamka uko kwenye majaruba ndio utajua uchawi upo au la!!

Ndio ninyi mnaenda shule Kisha mnamkataa hata Mungu na kuzidi kutokomea gizani kuliko kupata Nuru.

Sorry Kwa lugha ngumu!!
 
HABARI YA PASAKA JF,Je Ulishawahi Kujiuliza Unaenda Wapi Ukisha kufa? Fuatana na Mimi Asubuhi Upate Elimu.

MTU AKIFA ANAENDA WAPI?
Mwili hushushwa ardhini baada ya pumzi kurudi kwa muumba,yaani baada ya nafsi kufa!

Kifo kinauma sana,na ukizingatia wengi hatujui nini kinafuatia baada ya kifo.Hatujui kama wapendwa wetu wanaunguzwa kwenye moto,wamepumzika paradisoni au wanahangaika peponi.Haya maswali yanasumbua watu wengi,mtu akifa nini kinafanyika?Lakini kwa bahati nzuri majibu tunayo....ebu tujifunze.

Tunakwenda wapi tukifa? Mbinguni? Jehanum? Toharani? (Toharani ni mahali ambapo baadhi ya watu hudai marehemu hupitia kupata mateso ili aruhusiwe kuingia ahera) au Ahera? Ndugu zetu waliokufa wako wapi? Je, tunaweza kuwaona?Hata Biblia linauliza hili swali, “Mtu akifa, je! atakuwa hai tena?” (Ayubu 14:14).

Lakini pia Biblia linatupa jibu thabiti ambalo halina utata. Majibu yake yanaeleweka, yanaridhisha, na zaidi ya yote, yanafariji.

MTU ANAPOKUFA, HUWA KUNATOKEA NINI?
“Nayo mavumbi kuirudia nchi kama yalivyokuwa, nayo roho kumrudia Mungu aliyeitoa.” Mhubiri 12:7.Tukumbuke kitu kimoja hapa, neno "roho" iliyotumika hapa haina tofauti na "pumzi".Mara nyingi sana imetumika neno hilo roho kwenye Biblia kama tafasiri ya neno "spirit" pamoja na neno "breath".Yaani neno breath limetumika mara chache....

Mwili huyarudia mavumbi na pumzi/roho humrudia Mungu aliyeitoa. Pumzi ya mtu aliyekufa, awe mwenye haki au mwovu – humrudia Mungu wakati wa kufa,kwakuwa ni yeye aliitoa na sasa anakuwa ameitwaa.

ROHO AU PUMZI INAYOMRUDIA MUNGU NI KITU GANI?
Biblia inasema “Mwili pasipo roho(pumzi) umekufa.” Yakobo 2:26. “Roho(pumzi) ya Mungu i katika pua yangu.” Ayubu 27:3.

Roho inayomrudia Mungu wakati wa kufa ni ile pumzi ya uhai. Hakuna mahali katika Biblia ambapo tunaambiwa kuwa roho(pumzi) inakuwa na uhai, hekima au hisia baada ya mtu kufa. Ni “pumzi ya uhai”, na si ya kifo.Yaani kukosa pumzi matokeo yake ni KIFO!

NAFSI NI NINI?
“BWANA Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai.” Mwanzo 2:7. Nafsi ni muunganiko wa vitu viwili: Mwili(nyama, mifupa, damu, mishipa n.k) na pumzi(roho). Nafsi haiwezi kuwepo bila mwili na pumzi kuunganishwa. Neno la Mungu linafundisha kuwa sisi ni nafsi.

NAFSI HUFA?
Ndiyo,nafsi hufa.
Biblia inathibitisha hili kwenye Warumi 7:24," Ole wangu, maskini mimi! Ni nani atakayeniokoa na mwili huu wa mauti?" na kwenye Waebrania 9:16, "Maana agano la urithi lilipo, lazima iwepo mauti yake aliyelifanya."Pia Ezekiel 18:20,"Roho(spirit) itendayo dhambi, ndiyo itakayokufa.”

Kulingana na Neno la Mungu, nafsi inaweza kufa! Sisi ni nafsi na nafsi zinaweza kufa. Mwanadamu hufa. Mungu pekee hapatikani na mauti (1 Tim. 6:15,16). Dhana ya nafsi isiyokufa inapingana na Biblia inayofundisha kuwa nafsi hazina budi kufa.

MTU ALIYEKUFA ANAWEZA KUJUA AU KUELEWA KITU?
Hapana! “Walio hai wanajua ya kwamba watakufa; lakini wafu hawajui neno lo lote, wala hawana ijara tena; maana kumbukumbu lao limesahauliwa. Mapenzi yao na machukio yao, na husuda yao, imepotea yote pamoja; wala hawana sehemu tena katika jambo lo lote linalofanyika chini ya jua.” “Lolote mkono wako utakalolipata kulifanya, ulifanye kwa nguvu zako; kwa kuwa hakuna kazi, wala shauri, wala maarifa, wala hekima, huko kuzimu (kaburini) uendako wewe.” Mhubiri 9:5,6,10. “Sio wafu wamsifuo Bwana.” Zab. 115:17.

Mungu anasema wafu hawajui kitu chochote.

WAFU WANAWEZA KUWASILIANA NA WALIO HAI?
Hapana! "Ni vivyo mwanadamu hulala chini, asiinuke; hata wakati wa mbingu kutokuwako tena, hawataamka, wala kuamshwa usingizini.” “Wanawe hufikiria heshima, wala yeye hajui; kisha wao huaibishwa, lakini yeye hana habari zao.” Ayubu 14:12,21. “Wala hawana sehemu tena katika jambo lolote lililofanyika chini ya jua.” Mhubiri 9:6.

Wafu hawawezi kuwasiliana na walio hai. Wamekufa. Mawazo yao yamepotea (Zab. 146:4).

SASA KWANINI SISI TUNAPATA NDOTO KUTOKA KWA WAFU KAMA HAWAELEWI KITU CHOCHOTE?
Natoa mfano hai kwenye Biblia,kwa sababu Biblia haifichi mambo. Mfalme Sauli na majeshi yake walikuwa vitani kaskazini mwa Israeli. Walikabili jeshi lenye kuogopesha la Wafilisti. Sauli alipoona majeshi ya Wafilisti, “akaogopa, na moyo wake ukaanza kutetemeka sana.” Wakati huo, Sauli alikuwa tyari ameacha ibada ya kweli. Kwa sababu hiyo, Yehova hakumjibu sala zake. Sauli angefanya nini ili apate msaada? Samweli, nabii wa Mungu naye alikuwa ameshafariki(1 Samweli 28:3, 5, 6).

Sauli aliamua kumtafuta mwongozo kutoka kwa mwanamke mmoja aliyekuwa na uwezo wa kuwasiliana na pepo huko En-dori. Alimsihi mwanamke huyo “nipandishie Samweli” kutoka kwa wafu. Mwanamke huyo alipandisha mzuka(mapepo) na kuweza kumuona “Samweli”. Na huyo Samweli aliyetokea aliongea na Sauli na kumwambia kuwa Wafilisti wangeshinda vita na kwamba Sauli na wanawe wangekufa vitani. (1 Samweli 28:7-19) Je, huyo alikuwa Samweli aliyeonekana alikuwa wa kweli aliyerudi kutoka wafu?Jibu ni hapana,lakini majibu ya huyo mama yalikuwa ya ukweli mtupu! Hii inawezekanaje?

Fikiria jambo hili kwa makini zaidi. Biblia inasema kwamba mtu anapokufa ‘anarudi kwenye udongo wake’ na kwamba “mawazo yake hupotea.” (Zaburi 146:4).Biblia haijichanganyi hata siku moja. Sauli na Samweli wote walijua kwamba Mungu anachukizwa sana na mawasiliana kati ya binadamu na mapepo(Mambo ya Walawi 19:31).

Kilichotokea,na kinachotokea mara kwa mara hata mpaka leo hio ni mawasiliano kupitia kwa malaika waasi,ambao ni viumbe vya kiroho(spirits),na ambao waliasi mamlaka ya Mungu mapema katika historia ya wanadamu(Mwanzo 6:1-4; Yuda 6). Mashetani hawa wanaweza kututazama na kuona binadamu hai.Wanajua mawazo yetu,uwezo wetu na madhaifu yetu.Pia wanajua ndugu zetu walikwisha kufa tangia walipokuwa hai,wanajua mahusiano kati ya hao marehemu na watu waliopo duniani. Kwa hiyo wanajua jinsi mtu alivyokuwa anazungumza, alivyotenda, na sura yake alipokuwa hai. Wanataka kuendeleza dhana kwamba Biblia na Mungu ni uwongo(dhana ambalo shetani alilianzisha tangia shamba la Edeni). Biblia inatuonya tusiwe na mawasiliano yoyote na roho kama hao! (Kumbukumbu la Torati 18:10-12) Mashetani hao bado wanatenda kazi leo na wataendelea mpaka muda wao utakapoisha.

Sasa tunaweza kuelewa ni kwa nini wengi wanasema kwamba “wamewaona” wapendwa wao waliokufa au “kusikia” sauti yao. Ingawa wafu hao wanapotokea kama mizuka wanaweza kuonekana kuwa na nia nzuri, kumbuka kwamba roho waovu wameazimia kuwadanganya watu (Waefeso 6:12),hata kwa habari njema.

Kila binadamu anapokuwa hai hapa duniani,ni kiumbe cha kiroho ndani ya mwili wa nyama.Ni pumzi ndani ya mwili.Ndiyo maana anaweza kuwasiliana aidha na Mungu au shetani kiroho na siyo kimwili.Binadamu yuko huru kufanya mawasiliano kupitia roho mtakatifu wa Mungu au roho mtakavitu na chafu wa shetani.Mungu ni roho,na anataka tumuabudu kwa ROHO na KWELI (Yohana 4:24)"Mungu ni Roho, nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli."

Hii inamaanisha kuna kuabudu kwa ROHO na WONGO pia,right?Ni wewe uchague uko pande ipi....Mungu halazimishi ila matokeo ya chaguo lako hayaepukiki.

Kumbuka kwamba siyo ndoto zote ni mbaya au dhambi,kuna ndoto zinazotoka kwa Mungu kwajili ya watu wa Mungu.Alafu kuna ndoto zingine zinazotokea kwa ibilisi kwajili ya watu wake.Kuna mifano mingi mno ndani ya Biblia.

Ukisoma Matendo ya Mitume 2:17 inathibitisha kwamba hata siku za mwisho watu wataota ndoto kutoka kwa Mungu,inasema hivi,"Itakuwa siku za mwisho, asema Mungu, nitawamwagia watu wote Roho yangu, na wana wenu na binti zenu watatabiri; na vijana wenu wataona maono; na wazee wenu wataota ndoto."

#MunguNiRoho
Ni vigumu kujua kwa sababu waliokufa hawajawahi kurudi ili watujulishe walikoenda, ila labda tukuue wewe unayetaka kujua, ukipenda japo si lazima urudi kutujulisha ulikuwakuta wenzako.
 
hakuna NAFSI, hakuna ROHO,...kama vingekuwepo, basi tungelikuwa na kumbukumbu ya wapi tulikuwepo kabla HATUJAZALIWA...kwa ufupi hizo ni stori tu za kuendelea kuwashika WAJINGA...kule anakoenda Sisimizi au Mbuzi baada ya kufa ndiko mwanadamu aendako pia, mwanadamu huna u-special wowote zaidi ya kuwazidi viumbe wengine UJINGA tu...
Hili jambo nimewahi kujiuliza. Binadamu ana utofauti upi na viumbe wengine? Kwanini masuala ya mbinguni hayahusishi ng'ombe, vyura na viroboto?

Jibu ni kuwa ukishasema mambo ya kwenda mbinguni umehusisha masuala ya imani, imani ya binadamu sio ya ng'ombe.

Ila kama utaondoa mambo ya imani, hakuna tofauti yoyote kati ya mwanadamu na viumbe wengine zaidi tu kuwa binadamu ubongo wake una uwezo mkubwa kuliko wa wanyama kama ambavyo ubongo wa nyani ulivyo na uwezo mkubwa kuliko wa bata.
 
Nenda kamuulize mama Yako alipokuzaa, kitovu chako alipokikata alikitunza wapi ndipo uje useme Ulimwengu wa Nuru na Giza ni story!!

Siku utakapolala umefunga milango na ukaamka uko kwenye majaruba ndio utajua uchawi upo au la!!

Ndio ninyi mnaenda shule Kisha mnamkataa hata Mungu na kuzidi kutokomea gizani kuliko kupata Nuru.
Ndo akili zenu WAAFRIKA, upumbavu tu, ndo maana mzungu alipowaachia Dini tu akamaliza kila kitu, munahangaika na vitovu ilihari munanuka umasiki wa kutupa,kitovu kina maana na kazi gani tena ilihari Kazi yake ilishakwisha baada ya mtu kuzaliwa,
Tumieni basi hayo maimani yenu ya kipumbavu kuleta maendeleo munabaki munabung'aa macho tu....

Hivi munapata wapi hata muda wa kudanganyana kuhusu maisha baada ya kifo wakati, maisha ya hapa DUNIANI tu yamewashinda, munaishi kama wanyama?...
 
Hili jambo nimewahi kujiuliza. Binadamu ana utofauti upi na viumbe wengine? Kwanini masuala ya mbinguni hayahusishi ng'ombe, vyura na viroboto?

Jibu ni kuwa ukishasema mambo ya kwenda mbinguni umehusisha masuala ya imani, imani ya binadamu sio ya ng'ombe.

Ila kama utaondoa mambo ya imani, hakuna tofauti yoyote kati ya mwanadamu na viumbe wengine zaidi tu kuwa binadamu ubongo wake una uwezo mkubwa kuliko wa wanyama kama ambavyo ubongo wa nyani ulivyo na uwezo mkubwa kuliko wa bata.
Na tuumbe mtu Kwa Mfano wetu.

Mtu ni mfano wa Mungu,

Mtu ni ROHO, alitoka Kwa Mungu ambaye ni ROHO.

Akili na uwezo wa uwezo wa kufanya maamuzi,ndicho kinamtofautisha mtu na mnyama.

Mtu ni WA milele,
 
Jibu hoja. Acha kujificha kwenye kichaka cha karanga.
Sasa nishajua mtu huna upeo ni kujibu while najua huta elewa ni kupoteza muda..... kuwa msomi/mwerevu ni pamoja na kujua unabishana kihoja na mtu wa aina gani .....kama mjinga mwambie asipolewa achana nae ...ila kama mpumbavu achana nae maana kiswahili mtu mpumbavu ni yule hata ukimwambie hawezi elewa
 
Hili jambo nimewahi kujiuliza. Binadamu ana utofauti upi na viumbe wengine? Kwanini masuala ya mbinguni hayahusishi ng'ombe, vyura na viroboto?

Jibu ni kuwa ukishasema mambo ya kwenda mbinguni umehusisha masuala ya imani, imani ya binadamu sio ya ng'ombe.

Ila kama utaondoa mambo ya imani, hakuna tofauti yoyote kati ya mwanadamu na viumbe wengine zaidi tu kuwa binadamu ubongo wake una uwezo mkubwa kuliko wa wanyama kama ambavyo ubongo wa nyani ulivyo na uwezo mkubwa kuliko wa bata.
hizi imani zinawafanya watu kuwa matahira sasa,.hili BARA lina watu wapumbavu sijawi ona....yani ni Binadamu tu ndo uwe na nafsi mara ROHO.., ila viumbe vingine havina?...
 
Na tuumbe mtu Kwa Mfano wetu.

Mtu ni mfano wa Mungu,

Mtu ni ROHO, alitoka Kwa Mungu ambaye ni ROHO.

Akili na uwezo wa uwezo wa kufanya maamuzi,ndicho kinamtofautisha mtu na mnyama.

Mtu ni WA milele,
According to imani upo sahihi.
 
Na tuumbe mtu Kwa Mfano wetu.

Mtu ni mfano wa Mungu,

Mtu ni ROHO, alitoka Kwa Mungu ambaye ni ROHO.

Akili na uwezo wa uwezo wa kufanya maamuzi,ndicho kinamtofautisha mtu na mnyama.

Mtu ni WA milele,
Ikiwa mtu ni wa milele maana yake pia alikuwepo hata kabla hajazaliwa, na pia atakuwepo hata baada ya kufa....

sasa wewe una kumbuka ulikuwa wapi kabla hujazaliwa?...
 
hizi imani zinawafanya watu kuwa matahira sasa,.hili BARA lina watu wapumbavu sijawi ona....yani ni Binadamu tu ndo uwe na nafsi mara ROHO.., ila viumbe vingine havina?...
Hili bara la kijinga sana mkuuu werevu kama wewe au mimi ni wachache mno ....wakutafuta na tochi.....
 
hizi imani zinawafanya watu kuwa matahira sasa,.hili BARA lina watu wapumbavu sijawi ona....yani ni Binadamu tu ndo uwe na nafsi mara ROHO.., ila viumbe vingine havina?...
Ukifata imani ndivyo ilivyo. Ila ukiiweka imani pembeni wewe na kunguni hamna tofauti. Mpo duniani kula, kunya na kufa, mengine mbwembwe.

Hata hivyo, Nje ya imani ubongo wa binadamu kupitia sayansi unafanya kazi kwa upekee sana. Pengine ukaja na dawa ya kutokufa huko mbeleni.

Nje ya imani wewe ni nani?

Wewe ni kumbukumbu ya yale uliyofanya na yale uliyofanyiwa na wengine.

Hizo kumbukumbu zimebebwa na mashine iitwayo mwili yenye kifaa maalum kiitwacho ubongo.

Sasa siri hapa ni namna ya kuzihamisha hizo kumbukumbu kwenye vifaa visivyoharibika au vifaa vingine tofauti na mwili au kuhakikisha kile kinachochakaza mwili hakichakazi.

Wanasayansi wapo kazini. Wameshafanikiwa kiasi kwenye uchakavu wa umbile la nje yaani sura. Sasa hivi ukiwa na pesa unaweza kuwa na miaka 60 ila ukaonekana kama una upo 20's.

Tunavyojadili hapa kuna program za kulipia za kugandisha mwili ikiaminika kwamba miaka mingi mbeleni tech itakuwa imekuwa juu kiasi cha kuurudisha mwili hai tena, hivyo si lazima uzikwe ukiwa na pesa, unaweza lipia ukagandishwa kwa vifaa maalum. Au kama ni mgonjwa na sasa hakuna dawa unaweza lipa ukasubiri miaka 200 ijayo dawa ikipatikana.
 
Back
Top Bottom