Mtu aliyekataa kumuhudumia Mzazi wake hadi anakufa, je, afanye nini ili laana imuepuke?

Mtu aliyekataa kumuhudumia Mzazi wake hadi anakufa, je, afanye nini ili laana imuepuke?

Hapo inategemea
Kama alikua anatamani kumuhudumia alafu uwezo hana hata mzazi aache laana haitampata huyo mana Mungu ni mwaminifu!
Ukisema ufate kabisa maandiko yenyewe yanasema fedha na mali mtu hupewa na babaye ila siku hizi wanadamu tumeenda vise versa yani ela badala tupewe na wazazi sisi ndo tunatakiwa tuwape na ndo mana circle ya umaskini haiishi kabisa!
Mimi nnachojua cha hakika ukimdharau au kumtukana mzazi utapata laana ila kumhudumia sidhani as wengine uwezo hawana hata hizo laana zenyewe inabidi zione aibu kidogo!
Wazazi wengi hawajawekeza kwa watoto vizuri wanataka walelewe asilimia 100 na hawajawapa hata mia watoto au biashara au urithi
 
Hakuna laana yoyote Ile hizo ni fikra potofu tu binadamu tu nadanganywa. Kafa yeye hujamuua nakumsaidia mtu au kutokumsaidia ni uamzi wako nahakuna kitakachokupata hata usipowasaidia
Duh we Kweli ndio mpwayungu
 
ni miongoni mwa makosa makubwa sana kumtupa mzazi wako, hata kama huyo mzazi mlikuwa hampatani kabisa lakini unatakiwa umhudumie hata kama humpendi. ukimtupa mzazi wako kuna uwezekano mkubwa ukapata laana na hii ni kweli.

QURAN 17:23-25

23. "Na Mola wako Mlezi ameamrisha kuwa msimuabudu yeyote ila Yeye tu, na wazazi wawili muwatendee wema. Mmoja wao akifikia uzee, naye yuko kwako, au wote wawili, basi usimwambie hata: Ah! Wala usiwakemee. Na sema nao kwa msemo wa hishima. Na uwainamishie bawa la unyenyekevu kwa kuwaonea huruma. Na useme: Mola wangu Mlezi! Warehemu (wazazi wangu) kama walivyo nilea utotoni. Mola wenu anajua kabisa yaliyo nyoyoni mwenu. Ikiwa nyinyi mtakuwa wema, basi hakika Yeye ni Mwenye kuwasamehe kwa wanao tubia kwake."


Kama ni muislamu huyo aliemuasi mzazi wake, kwanza kabisa amuombe Mwenyezi Mungu msamaha kwa makosa hayo, hapa itambidi aamke usiku kuswali na ajutie kabisa makosa yake hayo.

Pili awaombee dua mara kwa mara hao wazazi au mzazi aliye fariki, na awatolee sadaka, sadaka hii unaweza kuwapa yatima au masikini au kuchangia ujenzi wa msikiti n.k

Na tatu awasaidie au awe karibu na ndugu za wazazi wake ambao wao hai kwa sasa, yani asiwatupe hao ndugu za baba au mama yake.

Hii inaweza kusaidia kupunguza laana au kuiondosha kabisa kama Mwenyezi Mungu atamkubalia toba yake. (Mwenyezi Mungu ni mjuzi zaidi)
 
Raana ni kuamini km unavyoamini ukienda kwa mwamposa utapata mme au mke
Sizan km kuna raana apo na sizan km ni lazima kwa mtt kumuhudumia mzazi ad ifike atua ya kutiana laana
 
Mashangazi tuliwashika mkono tukawaleta mjini mkiwa na tongotongo sasa mmepata pesa mnaongelea puani.

Mlete hizo hela huku, tukifa mnalo
 
Awalishe mayatima na wazee wasiojiweza kadiri anavyoweza
Kubwa zaidi amuombee MWENYEZIMUNGU apate kumsamehe
Na zaidi kila anapopata wasaa
Amuombee MZAZI kwa DUA ya kumuomba MWENYEZIMUNGU amsamehee mzazi wake aliyefariki DHAMBI zake
 
Laana ni Nini ?

Hakuna Laana wewe mwenyewe ndio unaji-laani ndio maana Chizi au mtu asiyejali laana hazimpati (Dua la Kuku; as they say)

Ila wewe ukiamini kwamba kuna laana kila unalofanya unakuwa unaji-second guess; kwamba huenda hili halijafanikiwa sababu ya mzazi wangu kunilaani... Ukizingatia confidence ni kitu muhimu sana katika shughuli zako za kile siku, kwa kukosa kwako confidence mambo yako yatakwenda Kombo...

Ushauri fanya kile unachoona wewe ni sawa, ili kwa matokeo yoyote usijilaumu... (Ndio maana wafanya mabaya wengi huwa wanaji-convince kwamba tunafanya for a good cause) Yaani hata wanajeshi wanavyobaka wanawake na kuua watoto wanajipa moyo kwamba wale sio watoto wala wanawake bali na wanyama na mashetani na tunafanya kazi ya nchi...
 
1) Mwabudu Mungu
2) Waheshimuni watumishi wa Mungu
3) Waheshimuni wazazi kama walivyo.

Laana utaiepuka
 
Mithali 30:17 'Jicho la mtu amdhihakiye babaye, Na kudharau kumtii mamaye; Kunguru wa bondeni wataling'oa, Na vifaranga vya tai watalila'
 
Back
Top Bottom