Mtu anapomtukana mwenzake anafaidi nini?

Mtu anapomtukana mwenzake anafaidi nini?

GoldDhahabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2023
Posts
7,189
Reaction score
10,375
Hata kama amekasirishwa, kutukana kutamsaidia?

Nimo kwenye basi naelekea mkoa fulani. Njiani, mama mmoja kapitilizwa na konda kituo alichopaswa kushukia.

Kutokana na kukerwa na hiyo hali, aliposhuka, hakulalama tu, bali pia alisindikiza manung'uniko yake na tusi la nguoni. Alitukana kwa kutaja sehemu za siri za mwanamke.

Kwa kuwa aliyefanya hiivyo ni mwanamke, atakuwa amemtukana konda ambaye ni mwanaume au kajitukana mwenyewe?

1. Kama ni uke, yeye naye anao! Siyo kwamba amejitukana?

2. Hakuna kitu cha ajabu kwa mwanamke kuwa na uke. Kila mwanamke wa kawaida yuko nao. Kulikoni watu wanapokasirika hutumia huo msamiati kama fimbo ya kuwaadhibu waliowakasirisha?

3. Mwanaume anapomtukana mtu mwingine kwa kumtukania sehemu za siri za mama yake, naye si kwamba kajitukana? Kwani yeye mama yake hana?

Huwa nawaona wanaowatukana wenzao kwa kuwatukania sehemu za siri za mama zao kama wana tatizo la kiakili. Huo ndiyo mtazamo wangu.
 
tusi ni pigo la hisia ni kama kakukanda ngumi ya pua! so kama litakuwa limekuuma lazima utarudisha.. we are mostly developed creatures emotionally,hata wewe nikikushushia lundo la matusi unaweza ukahimili awali lakini nikiendelea nawe hisia zinaweza kukushika ukaanza nawewe kuyashusha na hata ngumi ikibidi..🤣
tusi ni emotional expression.
 
Kuna relief anaipata, ww hujawahi kujikwaa?? Nini kilitokea?? 😜
Kuna muda tusijifanye watakatifu wakati wote ni mashetani 😂😂😂


Inategemea Kinachotokana mdomoni ni kile ulichoishibisha AKILI yako.

Kwa MTU smarter hata itokee nini hawezi toa matusi

Ni viwango vya ukuaji ,na mazingira unayopendelea kukaa .

Matusi ni Alama kuwa Afya ya akili sio nzuri.
 
Ukiona mtu anatukana basi hayo matusi huakisi jinsi mtukanaji alivyo.

Kwa mfano; mtu akikuambia wewe mshenzi, maana yake yeye ndio mshenzi na huo ushenzi upo kwake sasa anajaribu kufanya wewe ufanane naye.

Golden rule ninayotumia mtu akinitukana huwa nakaa kimya, natabasamu na kuendelea na mambo mengine kama hakijatokea kitu.

Dunia imejaa vichaa wengi sana siku hizi tujitahidi kuwaepuka kadiri tuwezavyo ili mradi usiruhusu katu katu wavuke mipaka wasije kukutoboa jicho au kukuumiza.
 
Kuna relief anaipata, ww hujawahi kujikwaa?? Nini kilitokea?? 😜
Kuna muda tusijifanye watakatifu wakati wote ni mashetani 😂😂😂
Nooo madam!

Siyo wote ni mashetani mkuu! Mimi nitoe humo.

Isitoshe, kimtokacho mtu kinywani mwake ndicho kilichojaa moyoni mwake!

Ukilibinya chungwa, litatoa juisi ya chungwa, limao - juisi ya limao.

Mtu naye hisia zake "zikiguswa", kilichomo moyoni mwake humwagika kupitia kinywa chake.
 
Nooo madam!

Siyo wote ni mashetani mkuu! Mimi nitoe humo.

Isitoshe, kimtokacho mtu kinywani mwake ndicho kilichojaa moyoni mwake!

Ukilibinya chungwa, litatoa juisi ya chungwa, limao - juisi ya limao.

Mtu naye hisia zake "zikiguswa", kilichomo moyoni mwake humwagika kupitia kinywa chake.
Wewe toka uzaliwe hujawahi kutukana?? Hata kimoyo moyo bila watu kukuona??
 
Mimi naona ni kama, taswira aliyo nayo mtu kuhusu kile akionacho na kuhisi. Ina tegemea na level za akili ya mtu husika. Mimi mtu akitukana najua bado hajakua kiakili, sio mijinga ila bado hana experience ya maisha.
 
Inategemea Kinachotokana mdomoni ni kile ulichoishibisha AKILI yako.

Kwa MTU smarter hata itokee nini hawezi toa matusi

Ni viwango vya ukuaji ,na mazingira unayopendelea kukaa .

Matusi ni Alama kuwa Afya ya akili sio nzuri.
Ushawahi kujikwaa lakini?? 😂😂😂
 
Back
Top Bottom